Erythrocyte
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 117,601
- 217,992
Akizungumza na Wanahabari leo Mkoani Dodoma , RPC wa eneo hilo alidai kwamba , kiongozi wa Bavicha Twaha Mwaipaya alikamatwa kwa makosa ya Mtandao yaliyosababisha Taharuki kwa wananchi .
Mtukufu RPC ameshindwa kuyataja Makosa hayo aliyoyaita ya Mtandao , Wala hakutaja majina na Idadi ya Wananchi ambao amedai Walipata Taharuni kutokana na Mambo ya Mitandaoni yaliyowekwa na Mwaipaya .
Sasa sisi swali letu kwa nyinyi watu wa JF ni dogo tu , NI NANI KATI YENU ANAMFAHAMU MTU YEYOTE ALIYEPATA TAHARUKI KUTOKANA NA MAANDISHI YA TWAHA MWAIPAYA MITANDAONI ? tafadhali kama ni binamu yako , dada yako , mumeo au mkeo au jirani yako alipata hiki kinachoitwa Taharuki tuambie ili Tumkanye Mwaipaya asirudie tena .
Bado mimi na wengine wachache tunaamini kwamba kuna haja Mahsusi ya KULIVUNJILIA MBALI JESHI LA POLISI NA KULIUNDA UPYA , Hawa Polisi watunga uongo na wanaotumwa tumwa kusumbua vijana wa Upinzani , watasababisha Matatizo , ni Muhimu sana kuwang'oa kwa Masilahi mapana ya Taifa , Wala haitakuwa ajabu , mbona Nyerere aliachana na Polisi wa Kikoloni baada ya Uhuru wa Tanganyika ?
Mtukufu RPC ameshindwa kuyataja Makosa hayo aliyoyaita ya Mtandao , Wala hakutaja majina na Idadi ya Wananchi ambao amedai Walipata Taharuni kutokana na Mambo ya Mitandaoni yaliyowekwa na Mwaipaya .
Sasa sisi swali letu kwa nyinyi watu wa JF ni dogo tu , NI NANI KATI YENU ANAMFAHAMU MTU YEYOTE ALIYEPATA TAHARUKI KUTOKANA NA MAANDISHI YA TWAHA MWAIPAYA MITANDAONI ? tafadhali kama ni binamu yako , dada yako , mumeo au mkeo au jirani yako alipata hiki kinachoitwa Taharuki tuambie ili Tumkanye Mwaipaya asirudie tena .
Bado mimi na wengine wachache tunaamini kwamba kuna haja Mahsusi ya KULIVUNJILIA MBALI JESHI LA POLISI NA KULIUNDA UPYA , Hawa Polisi watunga uongo na wanaotumwa tumwa kusumbua vijana wa Upinzani , watasababisha Matatizo , ni Muhimu sana kuwang'oa kwa Masilahi mapana ya Taifa , Wala haitakuwa ajabu , mbona Nyerere aliachana na Polisi wa Kikoloni baada ya Uhuru wa Tanganyika ?