BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,790
- 288,005
Polisi Dar yatangaza vita dhidi ya majambazi
Yasema hakuna jambazi atakayeponyoka
na Happiness Katabazi
Tanzania Daima~Sauti ya Watu
JESHI la Polisi, Kanda Maalum ya Dar es Salaam, limetangaza vita dhidi ya majambazi na kuwataka wananchi wazidi kutoa ushirikiano kwa kuwapa taarifa za siri ili kufanikisha kukabiliana na matukio ya ujambazi yanayorejea kwa kasi jijini.
Kauli hiyo ya polisi imetokana na tukio la juzi ambapo majambazi walivamia kituo cha mafuta cha Gapco, kilichopo karibu na makutano ya Barabara ya Kawawa na Mandela na kupora zaidi ya sh milioni 200 pamoja kusababisha kifo cha mhasibu wa kituo hicho aliyeuawa kwa kupigwa risasi na majambazi hayo.
Kaimu Kamanda Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP), Evarist Mangalla, alisema katika mkutano wake na waandishi wa habari jana kuwa jeshi lake limejipanga kukabiliana na hali hiyo na kuwaonya watakaojihusisha na matukio ya ujambazi kuwa lazima watakamatwa.
Jeshi la polisi linazidi kutoa pongezi kwa raia wema wanaolisaidia jeshi hilo kwa kutoa taarifa ambazo zinaleta mafanikio katika kuutokomeza mtandao wa ujambazi, tunaahidi tutaendelea kusimama imara ili kukabiliana na majambazi hayo, alisema Kamanda Mangalla.
Alisema taarifa za siri kutoka kwa wananchi, ndizo zilizoisadia polisi juzi kuzima tukio lingine la ujambazi, lililopangwa kufanyika katika kiwanda cha Cello Plastick, kilichopo barabara ya Mbozi, eneo la Changombe ambapo majambazi watatu waliuawa.
ACP-Mangalla alisema walifanikiwa kuzima tukio hilo kwa sababu Octoba 5 mwaka huu, walipata taarifa kutoka kwa raia wema kwamba kuna kikundi cha majambazi kimekula njama za kutaka kuvamia na kupora fedha kiwandani hapo.
Baada ya taarifa hizo, polisi wetu walianza kufuatilia ili kubaini kundi hilo la majambazi na kuweka mtego wa kuwanasa na walifanikiwa, alisema Kamanda Mangalla.
Alisema katika ufuatiliaji zaidi, polisi walibaini mpango wa uporaji huo; uporaji huo ungelifanyika juzi asubuhi na baada ya taarifa hizo kubainika, waliandaa mtego kuwanasa.
Kweli, juzi saa 5:45 majambazi yaliyotarajiwa kufika katika eneo hilo, yalifika yakiwa na magari mawili na moja kati ya magari hayo namba zake zilisomeka T.619 AMD na jingine halikuweza kusomeka namba kwani baada ya kugundua wamezingirwa, walitoa bunduki walizokuwa nazo na kuanza kuwafyatulia askari ili wawadhuru na wapate nafasi ya kutoroka, alisema Mangalla.
Alisema polisi kuona maisha yao yako hatarini, walijibu mapigo na kuyafyatulia risasi majambazi hayo na kuyajeruhi; yalikufa yakiwa njiani kuelekea katika hospitali ya Amana.
Alisema majamabzi hayo yalipopekuliwa, yalikutwa na bunduki aina ya bastola yenye namba 016080 aina ya Browning iliyotengenezwa nchini Czechoslovakia.
Aidha alisema gari aina ya Toyota Chaser iliyokuwa inatumiwa na majambazi hayo ilibandikwa namba za bandia zilizosomeka T.989ATB na zilipobanduliwa namba za juu, ndani zilikutwa namba nyingine zilizosomeka T.447 AKM.
Kati ya majambazi hao, wawili wametambuliwa kwa majina ya John Philipo Komba ambaye alikutwa na shahada ya kupigia kura mfukoni mwake iliyotolewa Desemba 3 mwaka huu.
Hata hivyo alisema katika tukio hilo, hakuna askari aliyejeruhiwa kwa risasi isipokuwa askari watatu walipata maumivu kutokana na msukosuko wa kujigonga kwenye magari waliyopanda wakati wa mapambano hayo.
Aliwataja askari hao kuwa ni D.2927 D/SGT Joseph,D.8408 D/CPL Peter na F.5371 D/C Issa ambao walitibiwa na kuruhusiwa na hali zao zinaendelea vizuri.
Tukio hilo lilitokea siku moja na lile la uvamizi wa kituo cha mafuta cha Magomeni. Uvamizi huo, ni wa kwanza kwa ukubwa kutokea tangu Kamanda Suleiman Kova akabidhiwe Kanda Maalum ya Dar es Salaam, na kusababisha kifo cha mfanyakazi mmoja wa kituo hicho.
Mapema wiki hii polisi mjini Arusha walipambana na majambazi kwa zaidi ya saa 6 katika nyumba moja walimokuwa wamejificha na kusababisha vifo vya majambazi wawili, huku polisi mmoja akijeruhiwa na kushonwa nyuzi sita kichwani.
Yasema hakuna jambazi atakayeponyoka
na Happiness Katabazi
Tanzania Daima~Sauti ya Watu
JESHI la Polisi, Kanda Maalum ya Dar es Salaam, limetangaza vita dhidi ya majambazi na kuwataka wananchi wazidi kutoa ushirikiano kwa kuwapa taarifa za siri ili kufanikisha kukabiliana na matukio ya ujambazi yanayorejea kwa kasi jijini.
Kauli hiyo ya polisi imetokana na tukio la juzi ambapo majambazi walivamia kituo cha mafuta cha Gapco, kilichopo karibu na makutano ya Barabara ya Kawawa na Mandela na kupora zaidi ya sh milioni 200 pamoja kusababisha kifo cha mhasibu wa kituo hicho aliyeuawa kwa kupigwa risasi na majambazi hayo.
Kaimu Kamanda Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP), Evarist Mangalla, alisema katika mkutano wake na waandishi wa habari jana kuwa jeshi lake limejipanga kukabiliana na hali hiyo na kuwaonya watakaojihusisha na matukio ya ujambazi kuwa lazima watakamatwa.
Jeshi la polisi linazidi kutoa pongezi kwa raia wema wanaolisaidia jeshi hilo kwa kutoa taarifa ambazo zinaleta mafanikio katika kuutokomeza mtandao wa ujambazi, tunaahidi tutaendelea kusimama imara ili kukabiliana na majambazi hayo, alisema Kamanda Mangalla.
Alisema taarifa za siri kutoka kwa wananchi, ndizo zilizoisadia polisi juzi kuzima tukio lingine la ujambazi, lililopangwa kufanyika katika kiwanda cha Cello Plastick, kilichopo barabara ya Mbozi, eneo la Changombe ambapo majambazi watatu waliuawa.
ACP-Mangalla alisema walifanikiwa kuzima tukio hilo kwa sababu Octoba 5 mwaka huu, walipata taarifa kutoka kwa raia wema kwamba kuna kikundi cha majambazi kimekula njama za kutaka kuvamia na kupora fedha kiwandani hapo.
Baada ya taarifa hizo, polisi wetu walianza kufuatilia ili kubaini kundi hilo la majambazi na kuweka mtego wa kuwanasa na walifanikiwa, alisema Kamanda Mangalla.
Alisema katika ufuatiliaji zaidi, polisi walibaini mpango wa uporaji huo; uporaji huo ungelifanyika juzi asubuhi na baada ya taarifa hizo kubainika, waliandaa mtego kuwanasa.
Kweli, juzi saa 5:45 majambazi yaliyotarajiwa kufika katika eneo hilo, yalifika yakiwa na magari mawili na moja kati ya magari hayo namba zake zilisomeka T.619 AMD na jingine halikuweza kusomeka namba kwani baada ya kugundua wamezingirwa, walitoa bunduki walizokuwa nazo na kuanza kuwafyatulia askari ili wawadhuru na wapate nafasi ya kutoroka, alisema Mangalla.
Alisema polisi kuona maisha yao yako hatarini, walijibu mapigo na kuyafyatulia risasi majambazi hayo na kuyajeruhi; yalikufa yakiwa njiani kuelekea katika hospitali ya Amana.
Alisema majamabzi hayo yalipopekuliwa, yalikutwa na bunduki aina ya bastola yenye namba 016080 aina ya Browning iliyotengenezwa nchini Czechoslovakia.
Aidha alisema gari aina ya Toyota Chaser iliyokuwa inatumiwa na majambazi hayo ilibandikwa namba za bandia zilizosomeka T.989ATB na zilipobanduliwa namba za juu, ndani zilikutwa namba nyingine zilizosomeka T.447 AKM.
Kati ya majambazi hao, wawili wametambuliwa kwa majina ya John Philipo Komba ambaye alikutwa na shahada ya kupigia kura mfukoni mwake iliyotolewa Desemba 3 mwaka huu.
Hata hivyo alisema katika tukio hilo, hakuna askari aliyejeruhiwa kwa risasi isipokuwa askari watatu walipata maumivu kutokana na msukosuko wa kujigonga kwenye magari waliyopanda wakati wa mapambano hayo.
Aliwataja askari hao kuwa ni D.2927 D/SGT Joseph,D.8408 D/CPL Peter na F.5371 D/C Issa ambao walitibiwa na kuruhusiwa na hali zao zinaendelea vizuri.
Tukio hilo lilitokea siku moja na lile la uvamizi wa kituo cha mafuta cha Magomeni. Uvamizi huo, ni wa kwanza kwa ukubwa kutokea tangu Kamanda Suleiman Kova akabidhiwe Kanda Maalum ya Dar es Salaam, na kusababisha kifo cha mfanyakazi mmoja wa kituo hicho.
Mapema wiki hii polisi mjini Arusha walipambana na majambazi kwa zaidi ya saa 6 katika nyumba moja walimokuwa wamejificha na kusababisha vifo vya majambazi wawili, huku polisi mmoja akijeruhiwa na kushonwa nyuzi sita kichwani.