Polisi awania uongozi NEC ya CCM, akamatwa...

Sasa ni wakati muafaka kuhoji ya wakuu wa wilaya wanajehi na mapolisi, na majibu ya Pinda kuhusu ukada wao wa chama tawala. Vinginevyo polisi huyu hana hatia.
 
Mnashangaa nini hapo? Mbona makamanda wa polisi nchi nzima ni wanachama hai wa CCM? Huwezi kuteuliwa kuwa kamanda wa police mkoa au hata wilaya Tanzania kama wewe sio mwanachama hai wa chama tawala. Mwema pale alipo anakadi ya chama tawala, ni moja ya sifa ya kuwa IGP! Hivyo kujidanganya kuwa polisi hawana vyama ni kupoteza muda bure!
 
dah! hii kali jamaa alitaka kujiandikia historia ya kuwa mjumbe wa kwanza wa nec moro kupitia jeshi la polisi
 
Wapo wengi kana TIBAIGANA, OMARY MAHITA wote hawa wameishawahi kuingia kwenye mchakato wa kugombea ubunge bahati nzuri walikosa.
 
dah! hii kali jamaa alitaka kujiandikia historia ya kuwa mjumbe wa kwanza wa nec moro kupitia jeshi la polisi

Sio historia pekee inawezekana ameishaifanyia mengi CCM kama Kumuua Ally Zona pale Moro pia inawezekana ni yule aliyehusika kumlipua Mwangosi kule Nyororo kwani tuliambiwa kuna polisi wageni walipelekwa. Wekeni picha tulinganishe na ile ya Nyororo.
 
Ndio ujue siasa ni ajira inayolipa tz ndio maana watu wanauwana wakiangia huko.

Acha police wawanie nafasi yoyote ndani ya vyama,kwani watu wanaposema kuwa polisi wanafanya kazi kwa mazoea unadhani wanawasingizia? Ukifanikiwa kusoma maadili ya polisi japo ubeti mmoja ndipo utagundua kuwa askari wa cheo cha chini ameandaliwa mazingira magumu ki utendaji na anabanwa na viongozi wa juu kutenda hata ambayo hayapo ktk maadili na sheria za jeshi hilo na katiba kwa ujumla,wakati huo mkuu wa jeshi anahimiza polisi jamii ulinzi shirikishi,basi haya ndiyo matokeo yake kwa sababu lengo la polisi jamii ni kutaka kumfanya askari aonekane kama mtu mwingine wa kawaida.acha agombee bwana hiyo ndiyo polisi jamii bwana

  • :israel:...

 
Hivi inapo fikia hatua ya kila mtu kutaka kukimbilia kwenye siasa, hii inatoa picha gani kuhusu TAIFA letu in general? wanatafuta umaharufi/kujulikana au utajiri wa haraka haraka - ni TAIFA gani duniani limepiga hatua ya maendeleo kwa kuendekeza mambo ya SIASA?

Mimi naona hatuko justified kumlahumu askali wa watu, naye anajaribu bahati yake - maanake mambo ya siasa yanaonekana kama mchezo wa kamari - PATA,POTEA. God help US.
 
Wapo wengi kana TIBAIGANA, OMARY MAHITA wote hawa wameishawahi kuingia kwenye mchakato wa kugombea ubunge bahati nzuri walikosa.

Wamwachie tu dogo labda kosa hapo kutumia jina la Joel Bendera katika surname wakati analotumia kazini ni lingine
 
Labda ni mtoto wa nyumba ndogo ya Joel Bendera. Bendera ni mwanamichezo na kada wa CCM, sifa tosha kumiliki nyumba nyingi. Mkuu weka picha yake tuwafananishe na J Bendera
Inawezekana, asingejiamini kiasi cha kuandika jina la mtu bila sababu.
 
Mnashangaa nini hapo? Mbona makamanda wa polisi nchi nzima ni wanachama hai wa CCM? Huwezi kuteuliwa kuwa kamanda wa police mkoa au hata wilaya Tanzania kama wewe sio mwanachama hai wa chama tawala. Mwema pale alipo anakadi ya chama tawala, ni moja ya sifa ya kuwa IGP! Hivyo kujidanganya kuwa polisi hawana vyama ni kupoteza muda bure!
Hilo tunalijua na ndo maana hatuna imani na jeshi la Polisi, Hizo kadi zao na uanachama wataukana ifikapo 2016 pale chama wanachokiabudu kitakapokuwa out of system kwani nafikiri nguvu ya Umma ndiyo kiboko yao.
 
Hivi inapo fikia hatua ya kila mtu kutaka kukimbilia kwenye siasa, hii inatoa picha gani kuhusu TAIFA letu in general? wanatafuta umaharufi/kujulikana au utajiri wa haraka haraka - ni TAIFA gani duniani limepiga hatua ya maendeleo kwa kuendekeza mambo ya SIASA?

Mimi naona hatuko justified kumlahumu askali wa watu, naye anajaribu bahati yake - maanake mambo ya siasa yanaonekana kama mchezo wa kamari - PATA,POTEA. God help US.

Hapo nilipo-bold nimekumbuka kuna quotation ya @M.M.Mwanakijiji niliwahi kuiona sehemu ikisema "tunatoa ruzuku kwa vyama vya siasa ili viweze kututawala ila tunashindwa kutoa ruzuku kwa shirika la ndege la Tanzania ambalo lipo kwa ajili ya faida" (nimeinukuu kiana si kama alivyoileta mwanakijiji mwenyewe). Kwa kuwa hela za kwenye siasa zinatoka kiurahisi sishangai kuona kila mtu anataka kuingia kwenye siasa kwani sijaona wabunge / wanasiasa katika vyama vyao wameshindwa kulipwa hela zao kisa hazina haina hela ila kwa walimu na kada zingine ni kawaida tu tena hela zenyewe ni ndogo tu.

my take; huwa nasikitika ninapoona hela nyingi kutumika kwenye shughuli za siasa kuliko maendeleo, kama watu wana moyo wa kutoa rushwa ili wachaguliwe maana yake kila mmoja akienda jimboni kwake akasema kila kata atachangia laki 5 tu kama mwananchi wa kawaida (hii kama harambee flani) maana yake atasaidia wananchi wake kuibua miradi kibao ya maendele katika jimbo lake kiasi kwamba kila mwananchi kwa uwezo wake atatoa alichonacho (mwingine kuku, mwingine buku 2)siku akirudi kuomba kura hana haja ya kutoa rushwa kwani ameweza kuhamasisha wananchi wake kuona umuhimu wa kuchangia shughuli za maendeleo
 
Mishahara midogo ndo inawafanya askari kujihusisha na mambo ya siasa wakati huo pesa za serikari zinatumiwa vibaya na chama tawala aka CCM,sasa kwa nini kijana wa watu asifate rasilimali za nchi huko kwa magamba? ngoja Katiba ibadilishwe mtaona mengi, IGP upo?

  • :israel:

 
Pamoja na njaa kali za askari pia shetani aliekuwa anawasitiri magamba ameamua kuwaweka necked kabisa,siku zote tunapiga kelele kuwa haya majamaa ni policcm wanajifanya hawajui...leo shetani nae kachoka kuwalea kawaumbua!!!!
 
Back
Top Bottom