Polisi aliyemdhibiti Malima ajivunia kupata mafunzo CCP

chakii

JF-Expert Member
Sep 15, 2013
19,685
22,694
Shahidi wa kwanza katika kesi ya kuzuia polisi kutekeleza majukumu yao na kushambulia inayomkabili Naibu Waziri wa Fedha wa zamani, Adam Malima amesema alilazimika kupiga risasi hewani ili kuwatambulisha wananchi kuwa yeye ni askari aliyepata mafunzo Chuo cha Moshi.

Shahidi huyo, H 7818 PC Abdul wa Kituo Kikuu cha Polisi alieleza Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kuwa lengo lilikuwa ni kujinusuru na watu waliotaka kumvamia wakati wa kumkamata Malima. Mbali ya Malima, katika kesi hiyo mshtakiwa mwingine ni Ramadhan Mohammed anayekabiliwa na kosa la kuzuia polisi kutekeleza majukumu yao na kushambulia.

Akiongozwa na Wakili wa Serikali, Mutalemwa Kishenyi mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Respicius Mwijage, shahidi huyo alidai anakumbuka Mei 15 alikuwa na jukumu la operesheni iliyohusisha Kampuni ya Priscane Business.

Alidai walikwenda maeneo ya Masaki Kinondoni Dar es Salaam, akiambatana na Konstebo Edger na Msimamizi wa Kampuni ya Priscane, Joseph Mwita.

Aliendelea kuwa baada ya kumkamata Malima na vurugu kutokea eneo la Double Tree Msasani, wananchi walianza kumsogelea na kulazimika kupiga risasi tatu hewani ili wamtambue kuwa yeye ni polisi aliyepitia mafunzo Chuo cha Polisi Moshi.

Baada ya kumaliza ushahidi wake, Hakimu Mwijage aliahirisha kesi hadi Oktoba 3, itakapoendelea. Malima anawatetewa na Wakili Peter Kibatala.

Chanzo : Mwananchi
 
hivi angefanya mwingine si angekuwa korokoroni, wananchi hawana hata peni mfukoni unawafyatulia risasi, haya tutafika
 
Hivi kila mtu akifaya kituko cha namna hii ili kutambuliwa mafunzo yao hawa askari watastahimili kweli? Bila shaka CCP waongeze nguvu katika ufubdishaji wa somo la Communication skills pamoja na utu na saikolojia,kuwafundisha askari kutambuliwa kwa kutumia mitutu pekee hakutalisaidia Taifa maana bila shaka askari yule hakua na mkanda wa risasi na baada ya kupiga zile risasi 3 wengine alikua ameshaishiwa na wananchi wangeweza kumvamia vile vile na kumdhuru
 
hakuna mwananchi alifyatuliwa risasi,zilienda hewani zote.
Yule mpuuzi alilenga kutia hofu wananchi ila yeye na wenzie wafahamu kua masikio yana tabia ya kuzoea sauti mbali mbali hivyo kadri wanavyozidi kutumia silaha kupiga hewani hata pasipotakiwa kutumia bunduki ndivyo wananchi wanavyozea kusikia risasi na mabomu masikioni mwao kiasi kwamba baada ya muda hakuna atayeshtuka hata wakizisikia
 
Yule mpuuzi alilenga kutia hofu wananchi ila yeye na wenzie wafahamu kua masikio yana tabia ya kuzoea sauti mbali mbali hivyo kadri wanavyozidi kutumia silaha kupiga hewani hata pasipotakiwa kutumia bunduki ndivyo wananchi wanavyozea kusikia risasi na mabomu masikioni mwao kiasi kwamba baada ya muda hakuna atayeshtuka hata wakizisikia
sheria iko upande wake bado.

baada ya pale wangeonyesha kuwa wamezoea milio ya risasi,angeelekezewa mtu mguuni.
 
hivi angefanya mwingine si angekuwa korokoroni, wananchi hawana hata peni mfukoni unawafyatulia risasi, haya tutafika

Unataka kujifananisha na Askari?
Kila kazi Ina Mtu wake!
Mbona Wewe haupo Nairobi 'kumlinda' Lissu?
 
Hio ilikua inajukikana kabisa kwasbb pale Kosa liilikua wazi linajionesha na kibaya zaidi kukaidi amri ya polisi....
Siku ya kwanza Naona hio.clip nikajisemea tu kimoyoni huyu askari anastahili wa promote kwa cheo cha juu zaidi ya alicho nacho hapo
 
Hio ilikua inajukikana kabisa kwasbb pale Kosa liilikua wazi linajionesha na kibaya zaidi kukaidi amri ya polisi....
Siku ya kwanza Naona hio.clip nikajisemea tu kimoyoni huyu askari anastahili wa promote kwa cheo cha juu zaidi ya alicho nacho hapo
Fact
 
Hahah tukisema tunakoelekea Ni kubaya mnatuona wachochezi..ila kama kujitambulisha kwa askari mkalifu Ni kufyatua risasi basi Mungu atunusuru
 
Back
Top Bottom