Fundi Madirisha
Senior Member
- Jun 30, 2020
- 184
- 987
Nina mashaka kabisa kama kweli tuna jeshi la polisi hapa Tanzania kama siyo sehemu ya chama cha mapinduzi. Kwa sasa polisi bila haya wanatumika kisiasa kuilinda na kuitetea CCM huku wakikandamiza vyama viingine vya kisiasa.
Kama CCM wanakagua utekelezaji wa Ilani yao, ni kazi ya upinzani pia kufuatilia na kutoa mawazo mbadala kwenye miradi ile ile, hakuna aliye juu ya sheria katika taifa hili. Huwezi ukawa unatumika kulinda chama kimoja kufanya mikutano ya kisiasa lakini wengine wakikutana hata mikutano ya ndani unawaambia ni mikusanyiko eti kuna Corona, Mikutano ya CCM hakuna Corona? Haya mambo hayakubaliki kamwee!
Iko siku tutasema hapana mtupige na mtufunge wote wapinzani nchi nzima mtumalize. Tutasema sasa inatosha na unyanyasaji bado.
Kama CCM wanakagua utekelezaji wa Ilani yao, ni kazi ya upinzani pia kufuatilia na kutoa mawazo mbadala kwenye miradi ile ile, hakuna aliye juu ya sheria katika taifa hili. Huwezi ukawa unatumika kulinda chama kimoja kufanya mikutano ya kisiasa lakini wengine wakikutana hata mikutano ya ndani unawaambia ni mikusanyiko eti kuna Corona, Mikutano ya CCM hakuna Corona? Haya mambo hayakubaliki kamwee!
Iko siku tutasema hapana mtupige na mtufunge wote wapinzani nchi nzima mtumalize. Tutasema sasa inatosha na unyanyasaji bado.