Polepole: Walitaka kumhonga Rais Magufuli Sh. Bilioni 300 ili asifanyie kazi taarifa ya mchanga

Maneno haya yangetamkwa na kiongozi wa upinzani, angekuwa yumo ndani kwa tuhuma za uchochezi.
 
Basi yasitangazwe...kutaka kumhonga rais ni tusi kashfa na dharau kubwa
Hapa ndio pa kuonyesha meno na makucha yake makali
Kuishia kusema ALITAKA lakini AKAKATAAA ni kuongeza ukakasi kwenye sakata zima
Kama kuna mambo ya kuweka wazi bila kificho na kwa haraka hili ni mojawapo
Brother Mshana usiashangae sana hawa hawajui walitendalo. Unamuhongaje amiri jeshi mkuu halafu ukaendelea kula ugali? Au kahongwa na Trump nini? maana ndo mtu pekee ambae hatuwezi mkamata... wengine niliona wakipewa persona non granta wakafukuzwa sasa huyo ana immunity gani ya kuzuia his/her prosecution?
 
Tumempatia jeshi Hugo aliyeleta rushwa mbona hajawapeleka mahakama ya mafisadi
 
unajua ikifikia hatua hii ya kuanza kuletewa ujinga na propaganda za dizaini hii na akina Polepole na CCM yao, tutambue mara moja kuwa hata wao wameshatambua kuwa wamelikoroga na sasa wanatafuta pa kutokea !!!

Tundu Lissu aliwaambia mapema kuwa, acheni kutafuta umaarufu a. k. a "kick za kisiasa" katika mambo yanayohitaji mtumie akili zenu kufikiri kabla ya kuamua, lakini Magufuli na kamati yake eti ya "maprofesa" wakaja na ushauri uchwara na Mr President kama kawaida yake ya kukosa uvumilivu, kutokutafakari kwanza kabla ya maamuzi, jazba, na kukurupuka juu akaanza kuharibu réputation za watu......

Sasa acheni siasa zenu uchwara nyie kina Polepole na CCM, kaeni mkao wa kunyolewa bila maji na partners wenu wa biashara za wizi (wawekezaji) na msubiri na sisi wananchi wenu tuje tuwakate viwembe kabisa kwenye vichwa upara vyenu baada ya kunyolewa bila maji....!!!
 
Humphrey Polepole kasema kuwa Magufuli alitaka kuhongwa Billioni 300 ili asifanyie kazi taarifa ya mchanga wa madini .

Polepole ambaye ni Katibu wa Uenezi wa CCM,amesema hayo kwa uchungu akitoa msimamo wa chama juu ya uchunguzi uliofanyika

Hoja: Kina nani walitaka kumhonga rais?Wamechukuliwa hatua gani?
Huyo polepole alikuwepo au alisimuliwa na nani? Atoe taarifa kamili jibu la Magufuli lilikuwa nini?
 
Si akamatwe huyo mtoa rushwa au kakukuru hawapo
Vitu vingine vinatia aibu. Hivi mtu unaweza kujitokeza hadharani ukatamka nilitaka kuhongwa wakati vyombo vyoote vya usalama unavimiliki! Wasitake kutufanya sisi hamnazo kwa kuamini hadithi za alfu lela ulela.
 
Mlimwangalia machoni alipokuwa akitatamka hayo maneno? Anadhani sisi bado ni mataahira?
 
Report iliposomwa bwana yule akiomba ten minutes kupitia. Kwahiyo hizo 300 b zilitoka in those ten minutes? Kweli? Mbona Nape pamoja na goli la mkono hakuwa hivyo? Wewe unajidanganya mwenyewe?Kwa mdololo huu wa uchumi na ukame mlio nao kwanini zisichukuliwe hizo badala ya rambirambi? No that's 5much boy
 
Sijui kama tutafika kweli, kwani ambaye alitaka kutoa rushwa amekamatwa au bado?
 
Only in Tanzania, mtu anataka kumhonga Rais na hakamatwi, na wala hatutakaa tumjue...siasa ni ujinga na wajinga huwaamini wansaiasa
 
Kama hawatatajwa waliotaka kutoa rushwa na kuchukuliwa hatua, tutaaminije kama ni kweli? Acheni KIKI
 
Wakati mwingine watu mnajipambanua mlivyo wajinga na msiojielewa. Hivi mnajua Taasisi kama Urais, Takukuru, Polisi n.k? Vinafanyaje kazi? Mbadhani kila tukio ni Takukuru au Polisi na kukamata na kuhoji? Uelewa mdogo ni Dhambi.
Kumbe mnajua kuna utaratibu wa kufanyia kazi mambo haya.sasa mnatangaza kuwa amekataa rushwa ya b.300 ili iweje? Mlidhani ni sifa. ?
 
You d
Polepole kijana wangu,usilibebe hili jambo "kisiasa" zaidi.Hili jambo tuende nalo "kiuweledi" zaidi,ili huko mbele ya safari tusije tukapoteza na kumpotezea Rais wetu heshima kimataifa.Kila mtu anamuunga mkono Mh.Rais,wengi wanachotofautina naye labda ni "Approach" ya suala hili.

Ndio maana Tundu Lisu kasema tujitoe kwanza huko kwenye "MIGA" ndio tuanze "harakati" za kudai "mapanki" yetu ya dhahabu.Kama hatutakuwa tumejitoa,basi hao "mababeru" lazima watuadabishe,sbb tutakuwa tumevunja mikataba ambayo sisi wenyewe,kwa utashi na akili zetu timamu,tuliikubali na kuanguka saini.

Tukishamaliza huko,tuje tujitoe kwenye hizi "Bilateral Treaties" ambazo tuliingia kwa "mbwembwe" na USA,Canada na UK.Tukimaliza hapo,tuje kwenye bunge letu na tupeleke mswaada kwa hati ya dharura ili kufanya marekesbisho ya sheria ya Uwekezaji ya mwaka 1997 na sheria ya Misamaha ya Kodi za madini ya 1998 na ile Sheria ya Madini ya 2010 iliyoletwa Bungeni sbb ya "Buzwagi Saga-2007"

Vinginevyo,tutabaki kupiga kelele na kujazana upepo tu.
Salute
 
kwanza ni aibu Rais kutangaza kuwa aliongwa ni kushusha thamani ya Urais kma watu wana uwezo wa ku attempt kumuonga Rais basi cheo cha Urais hakiheshimiki
Wewe askari muoga: haya huwa yanatokea sana katika nchi zetu masikini zenye utajiri mkubwa wa asilimali. Nchi hizi hadi huwa zinanunuliwa na wakubwa. Rasilimali zetu ndizo zilisababisha tufanywe makoloni ya wakubwa hawa. Tulipewa uhuru wa bendera lakini wakubwa hao wanahakikisha rasilimali zetu wanaendelea kuzichota kama awali kwa mbinu zingine kama hizi (neocolonialism).

Polepole anaweza akawa amevujisha ukweli. Na kama ni kweli tukio hilo lazima litakuwa limenaswa na kamera za ikulu. Muda mwafaka zinaweza kuwa presented kwenye hiyo International arbitration court ambayo wakina Tundu Lissu wanatuaminisha itatunyoa bila maji.

Ila I'm just imagining kama angekuwa Mr Grey H, angekuwa na gut kweli hizo USD 150 million sawa na hizo tsh billion kuzikataa? Ingewezekana kweli akuzikataa huyo jamaa yetu? Wewe jee ungezikataa kama ungekuwa kwenye nafasi ile? Impossible, angezikubali tu, tena na kuwataka waongeze kidogo angalao ifike USD 200 million. Wengi wanagombania kupata kura za kuingia ikulu kwa sababu ya mambo kama hayo. Na wala siyo kwa sababu wanatuhurumia sana sisi boda boda, mama ntilie na masikini wengine wa nchi hii.
 
Wewe askari muoga haya huwa yanatokea sana katika nchi zetu masikini zenye utajiri mkubwa wa asilimali. Nchi hizi hadi huwa zinanunuliwa na wakubwa. Polepole anaweza akawa amevujisha ukweli. Na kama ni kweli tukio hilo lazima litakuwa limenaswa na kamera za ikulu. Muda mwafaka zinaweza kuwa presented kwenye hiyo International arbitration court ambayo wakina Tundu Lissu wanatuaminisha itatunyoa bila maji.

Ila I'm just imagining kama angekuwa Mr Grey H. angekuwa na gut kweli hizo USD 150 million sawa na hizo tsh 300 billions angezikataa kweli? Ingewezekana kweli akazikataa?
B.300 kwa CCM hiyo ni hela ya mboga.kwani tangu 1998 mpaka juzi mliposimamisha uchimbaji wa dhahabu mmekula sh.ngapi?
 
Back
Top Bottom