Uchaguzi 2020 Polepole kuwa na staha kwa viongozi wenzako kutoka vyama vingine

James Martin

JF-Expert Member
Apr 2, 2016
1,206
1,509
Nimekuwa nikifuatilia kwa karibu sana kampeni za uchaguzi huu na mmoja wa watu wanaoshiriki sana kwenye kampeni ni Humphrey Polepole.

Mimi si mwanachama wa CCM lakini nadiriki kusema Polepole ni mkomavu kwenye mambo ya siasa na ni hazina kwa chama chake cha CCM.

Ila kuna kitu kimoja kinanichefua kwenye kampeni zake: kuwatukana na kuwakejeli viongozi wenzake wa vyama vya upinzani. Huko nyuma aliwahi kumtukana Godbless Lema kwa kusema eti kuna mambo mengine yaliyomtokea jela hakuyahadithia. Polepole una bahati sana, yaani uniambie mimi maneno hayo wakati ule nipo kijana lazima zipigwe tu!

Sasa kama hiyo haitoshi, jana kwenye mkutano wake na waandishi wa habari alimwita mwenyekiti wa CHADEMA, Mh. Freeman Mbowe kuwa ni mlevi.

Kwenye upande mwingine, Tundu Lissu hajawahi kumtukana mtu kwenye kampeni zake zaidi ya kukosoa sera za CCM na mapungufu ya Magufuli kwenye utendaji wake serikalini.
 
Kuna watu ndani ya CCM hata kama kutakuwa na Truth and reconciliation commission, wao itabidi wawekwe "conderm", kunyongwa! Bashiru, Polepole , Makonda, Mambosasa, and a few others johnthebaptist unasemaje rafiki
 
  • Nzuri
Reactions: BAK
Kuna watu ndani ya CCM hata kama kutakuwa na Truth and reconciliation commission, wao itabidi wawekwe "conderm", kunyongwa! Bashiru, Polepole , Makonda, Mambosasa, and a few others johnthebaptist unasemaje rafiki

Tabia ya kutukana ni mbaya, lakini siwezi kusema wanyongwe kwasababu ya kutukana tu. Nina uhakika hata Lissu mwenyewe akiwa rais hawezi kwenda mbali kiasi hicho.
 
Polepole pia ni mgonjwa, siku akisahau kumeza dawa zake basi analopoka hovyo!!!
 
Nimekuwa nikifuatilia kwa karibu sana kampeni za uchaguzi huu na mmoja wa watu wanaoshiriki sana kwenye kampeni ni Humphrey Polepole.

Mimi si mwanachama wa CCM lakini nadiriki kusema Polepole ni mkomavu kwenye mambo ya siasa na ni hazina kwa chama chake cha CCM.

Ila kuna kitu kimoja kinanichefua kwenye kampeni zake: kuwatukana na kuwakejeli viongozi wenzake wa vyama vya upinzani. Huko nyuma aliwahi kumtukana Godbless Lema kwa kusema eti kuna mambo mengine yaliyomtokea jela hakuyahadithia.

Polepole una bahati sana, yaani uniambie mimi maneno hayo wakati ule nipo kijana lazima zipigwe tu! Sasa kama hiyo haitoshi, jana kwenye mkutano wake na waandishi wa habari alimwita mwenyekiti wa CHADEMA, Mh. Freeman Mbowe kuwa ni mlevi.

Kwenye upande mwingine, Tundu Lissu hajawahi kumtukana mtu kwenye kampeni zake zaidi ya kukosoa sera za CCM na mapungufu ya Magufuli kwenye utendaji wake serikalini.
Ndio siasa hiyo
 
Pole pole atanyoosha tu maelezo.
Leo imekuwa kura za magroup ya WhatsApp ambayo yana idadi ya watu 250.
Yaani kura 250 kati ya 20million.
Kichekeshio cha karne.
Hoja yako ni ipi? unajiliwaza, pole
 
Back
Top Bottom