Polepole hana ushawishi wa kisiasa kama aliokuwa nao Nape, ameunda vikundi vya kukihami chama na kutisha wananchi

Quinine

JF-Expert Member
Jul 26, 2010
21,271
47,271
Najaribu kuangalia tofauti kati ya Katibu Mwenezi wa CCM aliyepo Humphrey Polepole na Katibu Mwenezi aliyepita Nape Nnauye. Inavyoonekana Polepole ameishiwa mbinu au hana kabisa mbinu za ushawishi kwa wananchi.

Polepole alipoteuliwa tu alianza kuwarubuni wapinzani hasa viongozi kwa kuwahonga pesa na vyeo mbinu ambayo ilikuwa haina tija sana kisiasa, tofauti na wenzake waliokuwa wakishinda vijijini kushirikiana na wananchi kwenye ujenzi mbalimbali wa maendeleo, sasa ameanzisha vikundi vya kihalifu vya kujilinda ndani ya kitengo cha vijana vikundi ambavyo ni kinyume na katiba ya vyama vya siasa. Ni dalili ambayo siyo afya kwa chama, ni dalili ya kuanza kujihami, ni dalili ya kuleta vurugu ina viashiria vya uhalifu.

Polepole anaona fahari vikundi hivyo vinapofanya uhalifu na kuvihujumu vyama vingine, anafurahia anaposikia ofisi ya upinzani imechomwa moto, au kiongozi wa upinzani amepigwa risasi, anaona fahari vyama vingine vinaponyimwa vibali vya kufanya mikutano na kuandamana, anapoona anaruhusiwa kuandamana peke yake anatamba kwenye mitandao anafikiri hiyo ndiyo siasa.

FB_IMG_1560832121313.jpg


Mkiti mstaafu wa CCM JK aliwahi kusema Chama kikitegemea polisi kitashindwa. Napenda kumwambia Polepole kwamba cheo hicho kimekuwa kizito kwake hana mbinu zaidi za kukiongoza chama kikubwa kama hicho bila kuegemea ukuta wa polisi, hakisaidii chama wala Mkiti wake, atafute mbinu za kisiasa kama mwenzake Nape na Kinana walivyokuwa wakifanya bila msaada mkubwa wa jeshi la polisi.
 
Najaribu kuangalia tofauti kati ya Katibu Mwenezi wa CCM aliyepo Humphrey Polepole na Katibu Mwenezi aliyepita Nape Nnauye. Inavyoonekana Polepole ameishiwa mbinu au hana kabisa mbinu za ushawishi kwa wananchi.

Polepole alipoteuliwa tu alianza kuwarubuni wapinzani hasa viongozi kwa kuwahonga pesa na vyeo mbinu ambayo ilikuwa haina tija sana kisiasa, tofauti na wenzake waliokuwa wakishinda vijijini kushirikiana na wananchi kwenye ujenzi mbalimbali wa maendeleo, sasa ameanzisha vikundi vya kihalifu vya kujilinda ndani ya kitengo cha vijana vikundi ambavyo ni kinyume na katiba ya vyama vya siasa. Ni dalili ambayo siyo afya kwa chama, ni dalili ya kuanza kujihami, ni dalili ya kuleta vurugu ina viashiria vya uhalifu.

Polepole anaona fahari vikundi hivyo vinapofanya uhalifu na kuvihujumu vyama vingine, anafurahia anaposikia ofisi ya upinzani imechomwa moto, au kiongozi wa upinzani amepigwa risasi, anaona fahari vyama vingine vinaponyimwa vibali vya kufanya mikutano na kuandamana, anapoona anaruhusiwa kuandamana peke yake anatamba kwenye mitandao anafikiri hiyo ndiyo siasa.

View attachment 1130423

Mkiti mstaafu wa CCM JK aliwahi kusema Chama kikitegemea polisi kitashindwa. Napenda kumwambia Polepole kwamba cheo hicho kimekuwa kizito kwake hana mbinu zaidi za kukiongoza chama kikubwa kama hicho bila kuegemea ukuta wa polisi, hakisaidii chama wala Mkiti wake, atafute mbinu za kisiasa kama mwenzake Nape na Kinana walivyokuwa wakifanya bila msaada mkubwa wa jeshi la polisi.
Haya maandamano ya CCM yana kibali kweli.
 
Huyo polepole alipata uungwaji mkono wakati wa katiba mpya kwani alisimamia haki. Kwa sasa wale walimsupport hayuko nao na alidhani hata aliyemteua alifikiri atahama na huo mvuto. Ili kuficha aibu ya kukosa mvuto ndio maana amehamia kwenye siasa za hujuma. Ila asichofahamu Polepole, ni kuwa ccm ilikuwa haihitaji msaada wake sehemu ya mabavu kwani tayari mabavu walikuwa nayo na hayakuwapa uungwaji mkono. Walitarajia awasaidie kuvuta kundi la vijana kwa ushawishi, lakini inaonekana kabeba tabia ya mwenyekiti wake ya kutumia mabavu badala ya ushawishi.
 
Polepole yuko smart, Nape alikua bingwa wa mipasho.
Polepole anafanya kazi kisomi, kwa kuisimamia serikali na chama katika kutekeleza Ilani,
Mambo ya mipasho hayana nafasi kwa sasa, zama zake zilipita
 
Machadema akili zenu mmemkabithi mbowe..

Hivi msemaji wa Chadema ni nani vile..?! mnaanzaje nakuangaika na kada ambae hawahusu, CCM tumeridhika nae nyinyi mnawashwa washwa kwanini..?!!?
 
Polepole yuko smart, Nape alikua bingwa wa mipasho.
Polepole anafanya kazi kisomi, kwa kuisimamia serikali na chama katika kutekeleza Ilani,
Mambo ya mipasho hayana nafasi kwa sasa, zama zake zilipita

Ilani ya chama inasimamiwa kisomi kwa matumizi ya nguvu, au mimi ndio sielewi maana ya usomi?
 
Back
Top Bottom