Opportunity Cost
JF-Expert Member
- Dec 10, 2020
- 9,035
- 6,907
Mkufunzi wa shule ya uongozi Eng. Hamfrey Polepole amevishutumu vyombo vya kibeberu IMF na World Bank kwa kusababisha umasikini mkubwa na utegemezi wa milele kwa kutoa mikopo kandamizi kwa nchi masikini Kama Tanzania, na ameionya Serikali iliyopo madarakani kuwa makini na mikopo hiyo.
Wananchi wa Kenya waliandamana kupinga mkopo uliokopwa imf nchini Kwao Ila hata Tanzania juzi imekopeshwa mkopo mkubwa wa Tsh 1.3 trilioni na pole pole anasema huko ni kuingia katika mdomo wa mamba yaani ukoloni mamboleo chini ya mabeberu.
Mkufunzi huyo mzalendo ambaye alidai serikali imepigwa photocopy alienda mbali na kumkemea Amos makala RC wa Dar kuwa aache kunyanyasa masikini wamachinga, Bali atende haki. Huyu hapo chini
Kwa nini wanamchekea huyu jamaa asifanywe kama kina Nape na Kinana? Kucheka na nyani utavuna mabua..
Hili tatizo walilisabanisha wao na mwendazake kama mtaji wa kura wakiwaita wanyonge huku wakiwatoza pesa za vitambulisho bila kuwasaidia kutoka kwenye unyonge .