esther mashiker
JF-Expert Member
- May 29, 2018
- 616
- 552
Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM , Ndugu Humphrey Polepole amemwambia Kiongozi wa Chama cha ACT Wazalendo ambaye pia ni mbunge wa Kigoma Mjini Zitto Kabwe, akatafute kazi nyingine ya kufanya ifikapo 2020.
Polepole amesema hayo katika mkutano wake na waandishi wa habari ambapo ameeleza kuwa Wananchi wa jimbo hilo hawamuelewi utendaji kazi wake.
Aidha Polepole amemkosoa Zitto kwa kumwambia anaupotosha umma juu ya uchumi wa Tanzania na namna ambavyo Serikali ya Awamu ya Tano inavyotekeleza miradi ya maendeleo kwa kutumia fedha za ndani.