Poleni wauza dawa .

Erythrocyte

JF-Expert Member
Nov 6, 2012
117,323
217,336
Ugomvi wa wakubwa wenu Pharmacy board dhidi ya Tfda sasa unawaumiza , makubaliano mliyoyafikia kati yenu na Tfda wakati ule wa yale mafunzo yenu ya ADDO yamepuuzwa ! Bila shaka mnayakumbuka , sasa mnanyang'anywa dawa zenu mlizonunua kwa mikopo ya FINCA kama vile mliiba ! msubiri kufungwa kwa madeni ! Pharmacy board haitambui hizo ADDO zenu japo vyeti vyenu vilitoka Wizara ya afya , maajabu ya mwaka ! Kuna tetesi kwamba kila kilichofanywa na tfda , pharmacy board itakipinga ! Harufu ya ARV feki inanukia , kwamba wenye ARV wana ushawishi mzito kwenye board na kwa vile tfda ndiyo ilifichua hayo mambo , tutaona ! ( tuchukulie kama tetesi ) bali mwenye kuyajua zaidi atufunue , hakuna haja ya matusi , nawasilisha.
 
Katika sekta yenye wafanyakazi wasiopendana nadha Afya inaongoza,samahani sana wakuu kama nitakuwa nimewakwaza!Naamini hata mgomo wamadaktari ili lakudharauliana lilikuwepo mno!Umimi huu usipoondolewa secta hii itaendelea kuwapa shida watanzania!THI imezimwa sababu madeni ila ukichunguza utakuta vita yawatu wa Afya wao kwawao imo!
 
Erythrocite, nimefuatilia hili jambo binafsi na nimekuta yafuatayo:
1. Kulikuwa na upotoshaji wa makusudi kwa watu waliotaka kupewa mafunzo ya watoa dawa, hususani hapa dar. Miongozo ya ADDO inasema maduka hayo ni maalum kwa vijijini na maeneo madogo ya mji. Hapa Dar, baadhi wa waratibu au wawezeshaji wa ADDO waliwaambia wauzaji na wamiliki kushiriki mafunzo hayo, na wataruhusiwa palepale walipo kupewa vibali vya maduka ya ADDO, jambo ambalo ni kinyume na kanuni. Na walifanya hivyo kwa maslahi binafsi, ya kukusanya pesa. Ndugu yangu alishiriki hayo mafunzo,alilipa 5000 usaili na mafunzo alilipa 250,000. Nasikia usaili kulikuwa na watu zaidi ya 3000, na mafunzo yalikuwa na zaidi ya watu 2000, sasa piga hesabu ni sh. ngapi.

2. Lakini nimeambiwa pia, sheria ya Baraza la Famasi ilipitishwa mwaka 2011, ila mafunzo yalifanywa na TFDA. Sasa, hawa jamaa wa Baraza wao wanaangalia vigezo. Na ndipo yalipo masikitiko ya wauzaji na wamilki, maana kulikuwa na haja gani kuwahimiza watu kusoma hayo mafunzo wakati unajua kabisa kuwa eneo alipo halistahili kupewa kibali kwa mujibu wa kanuni za ADDO???

3. Kuhusishwa na ARV feki za madabida na Baraza la wafamasia, nadhani ni kuishiwa hoja, sababu anayetakiwa kufanya ukaguzi wa viwandani si ni TFDA?? Nina amini kabisa, kama TFDA wangefanya kazi yao vizuri na si kuendekeza rushwa, wangegundua tatizo la ARV feki tangu kiwandani, au hata kwenye maghala ya MSD, wasikwepe lawama za uzembe huo. Kama tatizo la ARV feki limetokea kwa kiwanda cha hapa nchini, vipi dawa zinazotengenezwa nje ya nchi???
Lakini pia nimefuatilia huyu madabida ni nani Baraza. Kumbe, hana mamlaka yeyote yale ni mjumbe tu wa Baraza, katika Baraza mwenyekiti wao ni Dr. Mbwasi, na ndiye mwenye maamuzi yote!
Cha msingi nadhani taasisi hizi zifanye kazi zao kwa maslahi ya wananchi. Huenda kuna waliokuwa wananufaika na mfumo uliopita, na yawezekana pia hata watu wa Baraza nao wakawa na kisasi kwa wenzao wa TFDA. Ni vizuri wakaa chini na kufanya kazi.
 
Back
Top Bottom