Poleni wananchi kwa kujiokoa wenyewe: Mafuriko na Moto

Kamundu

Platinum Member
Nov 22, 2006
6,550
8,643
Nasikitika kuona Tanzania kutokuwa na idara imara ya kuokoa maisha ya watu.

Ndugu mmoja kaniambia kaokolewa na majirani kwenye mafuriko Dar cha ajabu hakuna kikosi cha zimamoto wala watu kutoka idara yoyote ya serikali imeenda kumsaidia kumuangalia wala nini.

Sasa tujiulize hizi idara zinafanya kazi gani. Ni kwamba hazijapewa pesa, hatuna vifaa au ni kwamba wana kila kitu lakini hawajui kazi yao?

Serikali wamekuwa wakaguzi tu lakini sio waokoaji. Tatizo lingine kila mapungufu tulionayo kuna watu watatetea badala ya kulalamika.

Zile namba zilizofunguliwa za ukipata tatizo unapiga zinafanya kazi gani?
 
Kamundu,
Siku hizi fedha zote za serikali ni mali ya Rais, hivyo matumizi yote yanaamuliwa na yeye hata kama hayajaidhinishwa na bunge! Kwa hiyo acha kulaumu watumishi wa serikali, kwani na wao wanasubiria maelekezo.
 
Nasikitika kuona Tanzania kutokuwa na idara imara ya kuokoa maisha ya watu. Ndugu mmoja kaniambia kaokolewa na majirani kwenye mafuriko Dar cha ajabu hakuna kikosi cha zimamoto watu idara yetote y serikali imeenda kumsaidia kumwangalia wala nini. Sasa tujiulize hizi idara zinafanya kazi gani. Ni kwamba hazijapewa pesa, hatuna vifaa au ni kwamba wana kila kitu lakini hawajui kazi yao. Serikali wamekuwa wakaguzi tu lakini sio waokoaji. Tatizo lingine kila mapungufu tulionayo kuna watu watatetea badala ya kulalamika. Zile namba zilizofunguliwa za ukipa tatizo unapita zinafanya kazi gani?
Tatizo jingine wakiambiawa msijenge mabendeni hawakubali yakiwapata mafuriko wanalalama hakuna msaada wakati walikwishaambiwa au kujenga kiholela ili majanga ya moto yakitekea basi zimamoto wawezekufika kwa haraka lakini hawakubali.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wataendelea kulaumu na kufa pia kama hawataki kutoka sehemu hatarishi,kila siku serikali inasisitiza watu wahame ila hawataki sa serikali ifanyaje?
NB: Wanaweza kuendelea kuishi maana hata serikali yenyewe imejenga kituo Jangwani wakati wanajua hapafai.

macson
 
Mimi nafikiri hakuna ubunifu kuna JKT, kuna asikari kibao pale Lugalo wanashinda kupalilia bustani pale siku nzima wakati wananchi wanaowalipa wako kwenye mafuriko, magari ya jeshi yame park na kutengenezwa kwa kuchakaa mengi bila kutumika, tunafumdisha ukakamavu JKT kwanini yakitokea majanga wasiletwe hata kwa muda mbona korosho walienda kubeba wataahidwa kubeba watoto
 
Tatizo jingine wakiambiawa msijenge mabendeni hawakubali yakiwapata mafuriko wanalalama hakuna msaada wakati walikwishaambiwa au kujenga kiholela ili majanga ya moto yakitekea basi zimamoto wawezekufika kwa haraka lakini hawakubali.

Sent using Jamii Forums mobile app
Nadhani kuna tatizo la kukariri pia. Siku hizi mvua zikinyesha Dar popote pale panaweza kufurika, mfano makutano Nssf, Kijitonyama, Mbezi-chini n.k.
 
Yaani huyu baba yangu mdogo imebidi anipigie simu USA kuoma pesa kapoteza kila kitu na anasema majirani ndiyo waokoaji hakuna serikali wala nini

Kumbe umehadithiwa na mtu anayekuomba hela??? Wewe mpe tu ikiwezekana muhamishe hapo kigogo tofauti na hapo kila mwaka atakupigia simu kukuonba pesa mvua ikinyesha
 
Mimi nafikiri hakuna ubunifu kuna JKT, kuna asikari kibao pale Lugalo wanashinda kupalilia bustani pale siku nzima wakati wananchi wanaowalipa wako kwenye mafuriko, magari ya jeshi yame park na kutengenezwa kwa kuchakaa mengi bila kutumika, tunafumdisha ukakamavu JKT kwanini yakitokea majanga wasiletwe hata kwa muda mbona korosho walienda kubeba wataahidwa kubeba watoto

Hao wanaoishi kando ya mito wamefanya ubunifu gani sasa???
 
Wakati watanzania wengine wako kwenye mafuriko watu wengi wanajali zaidi siasa wakati hawa ni walipa kodi
 
Wakati watanzania wengine wako kwenye mafuriko watu wengi wanajali zaidi siasa wakati hawa ni walipa kodi

mjomba kakuomba tena hela???
Mi nilikushauri pale anapoishi ni mtoni usipomuhamisha kwa mwaka si chini ya mara3 atakuomba tu hela
 
Hili tatizo lipo tokea enzi ya Baba yake January,Mzee wetu Yussuf Makamba alipokuwa RC wa Dar,imagine ni miaka mingapi imepita na ma RC wangapi wamepita.
Tusiwape lawama waliopo madarakani awamu hii,tujilaumu wenyewe kwa mengi na wala siyo kuishi mabondeni peke yake..
Tuwaambie bila kumumunya maneno hii ni mbaya na hii ni nzuri.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nasikitika kuona Tanzania kutokuwa na idara imara ya kuokoa maisha ya watu.

Ndugu mmoja kaniambia kaokolewa na majirani kwenye mafuriko Dar cha ajabu hakuna kikosi cha zimamoto wala watu kutoka idara yoyote ya serikali imeenda kumsaidia kumuangalia wala nini.

Sasa tujiulize hizi idara zinafanya kazi gani. Ni kwamba hazijapewa pesa, hatuna vifaa au ni kwamba wana kila kitu lakini hawajui kazi yao?

Serikali wamekuwa wakaguzi tu lakini sio waokoaji. Tatizo lingine kila mapungufu tulionayo kuna watu watatetea badala ya kulalamika.

Zile namba zilizofunguliwa za ukipata tatizo unapiga zinafanya kazi gani?
Huyu mtu anapaswa kumshukru mheshimiwa rais wa awamu ya tano kwa juhudi zake maana amewapa majirani zake roho nzuri na moyo wa upe do otherwise alikuwa asombwe
 
Wataendelea kulaumu na kufa pia kama hawataki kutoka sehemu hatarishi,kila siku serikali inasisitiza watu wahame ila hawataki sa serikali ifanyaje?
NB: Wanaweza kuendelea kuishi maana hata serikali yenyewe imejenga kituo Jangwani wakati wanajua hapafai.

macson
Uko sahihi,huu ujenzi maeneo hatarishi kama mabondeni au karibu na mikondo ya maji bila kusahau ujenzi holela bila kufuata utaratibu unakwamisha uokoaji.
 
5 Reactions
Reply
Back
Top Bottom