Habarini wadau!
Hakuna kitu nachokipenda dunia hii kama ukweli na haki, hata uwe unaniumiza kiasi gani lakini ukiwa ukweli tu basi roho yangu inabaki kuwa kwatu kabisa!
Kuanzia muda fulani jana jioni, masaa machache baada ya matokeo ya kidato cha nne kutoka, habari iliyoenea na kusambaa kwa kasi ni kuhusu matokeo fulani ya shule kumi (10) dhaifu zaidi katika matokeo hayo ya jana ya kidato cha nne ambapo katika hizo tisa (9) zimetoka mkoa wa Mtwara. kwakuwa taarifa hiyo ilitolewa muda huhuo wa matokeo basi moja kwa moja ikahusishwa na matokeo ya 2020 na kama kawaida, 'wachambuzi' wakaibuka na chambuzi kedekede kuhusu mtwara na watu wake.
Kama utani nilianza kuona hilo kwenye group la rafiki yangu fulani ambae ni mkuu wa shule huko lindi (wana group lao wa wakuu kanda ya kusini) tulipokuwa tunajadili hayo matokeo. alinionyesha mjadala wao mule na jinsi gani wakuu wa mtwara wa shule tajwa walivyokuwa wanashangaa na kubishia hizo taarifa kwa kuyarusha matokeo yao ya mwaka 2020 (ikumbukwe kuwa mtwara na lindi ni ndugu wenye utani na ushindani kiasi flani hivyo hoja hii iliibua u-mtwara na u-lindi fulani baina yao) .
Nakumbuka mkuu mmoja mle akasema hayo matokeo ni ya 2016 na kuwataka wakuu wajiridhishe kwa kuyaangali matokeo ya shule tajwa ya mwaka 2016 wajionee wenyewe. yule rafiki akadowload matokeo ya shule mojawapo ya 2016 na kweli yalikuwa kama yanavyoonekana haya yanayotembea..... nikaachana nalo kwakuwa haikuwa interest yangu na wala siyo mnufaika na wa kwanza au mwisho lkn pia nikajua kwakuwa iko hivyo basi taarifa hii itakuwa imeshapuuzwa kitambo tu. tukahamia kwenye mada zingine.
Ilipofika usiku nikaingia zangu JF kuperuzi (kama kawaida yangu ya kila siku....ndo starehe yangu kuu). nilistuka kukuta threads za kutosha huko za habari hiyo...kama kawaida, watu wa mtwara walishambuliwa mno kwenye treads hizo na michango; malaya, wavivu, hawana akili n.k. Lindi pia haikubaki salama hapo, watu wake nao waliambulia matusi kibao. hiyo ni JF; kwenye wasomi, wachunguzi na wachambuzi mahili tu.
Leo tena, humu JF, mjadala huo umeendelea kwa kasi.....kila mmoja anasema anavyoweza. wapo waliojitokeza na kutoa taarifa kuwa hiyo habari siyo sahihi bila mafanikio; wakajitahidi hadi kutoa matokeo ya mwaka 2020 ya shule hizo bila mafanikio. mashambulizi ya kusini yakazidi. nilibaki kinywa wazi kwakweli, nilibaki kinywa wazi kwa sababu humu ni JF na siyo kitu kingine.
Mshangao wangu haukuegemea dhihaka na dharau za watu wa kusini, hapana! hilo lipo kila siku humu na ni nadra kupita mwezi usione thread ya kupondea kusini. mshangao ulikuwa kwenye kuvuma na kuaminika kwa hiyo habari hadi humu JF na jinsi wadau walivyokuwa wanajitahidi, kwa umakini mkubwa, kutoangalia au kusikiliza wale waliokuwa wanatoa taarifa sahihi.
Habari ikavuma mno na mkuu wa mkoa akaona isiwe tabu (maana alikuwa anaulizwa sana, bila shaka) akaamua, kitendo ambacho kwangu (labda kwakuwa elimu yangu ndogo) niliona ni cha busara mno, kuwaeleza waandishi wa habari waliofika ofisini kwake kuwa ameamua KUMUOMBA katibu mtendaji wa baraza la mitihani, KWAKUWA TAASISI YAKE NDIYO ILIYOTANGAZA NA NDIYO YENYE MAMLAKA YA KUKANUSHA KUTANGAZWA KWA ISICHOKITANGAZA. sijajua kama kuna protokali iliyonyooka zaidi ya hiii!
Mkuu wa mkoa huyu, baada ya kutoa taarifa hiyo, ametukanwa vya kutosha tu.....kilaza kama wananchi wake (eti 'anamuamrisha katibu wa baraza' ye kama nani? (ingawa mi nilichokisikia ni kuwa AMEMUOMBA)), nonsensical, anatumbuliwa huyu sasa hivi n.k. ikumbukwe kuwa kuna watu waliyarusha matokeo ya 2020 ya shule hizo tangu jana masaa kadhaa kabla ya mkuu wa mkoa kusema chochote.
Baraza lilipokanusha uvumi huo baadae leo; wachangiaji, kwa makusudi nafikiri, wanasema kuwa 'baraza limefuta na kupanga tena'......dah, HII DUNIA HII, acha tu!
Poleni wana Mtwara na kusini kwa ujumla, mna gundu hampendeki wala hamna sifa ya kusifiwa. kwangu JF naiheshimu sana na ni kipimo kizuri tu cha yanayoendelea. kushadadiwa huku kwa habari fake kama hii na KUTOTAKA KABISA KUGEUZA, ANGALAU KIDOGO, KWA SHINGO ZAO KUUTAKA UKWELI ULIO WAZI KABISA ni ushahidi tosha kwa nikisemacho kwa watu wa kusini,,,,mna gundu. gundu sugu! hebu oneni:-
1. Hakuna yeyote anayezungumza kuhusu kupanda kwa ufaulu wa halmashauri ya Manispaa ya Mtwara.
2. Hakuna yeyote anayezungumzia kushika nafasi ya pili kwa mkoa wa lindi katika matokeo ya darasa la nne 2020.
3. Hakuna yeyote anayezungumza chochote kuhusu kupanda kwa ufaulu wa kidato cha pili kwa mkoa wa lindi kwa miaka mitatu mfululizo.
4. Hakuna yeyote anayezungumza chochote kuhusu kupanda kwa ufaulu wa kidato cha nne kwa miaka mitatu mfululizo kwa mkoa wa Lindi.
5. Hakuna yeyote anaesema chochote kuhusu mafanikio haya yaliyoanza kuonekana yanachagizwa na R.E.O ambaye pia ni mtu wa kusini huko huko.....hakuna!
Poleni wanu Mtwara, poleni wanakusini!
Hakuna kitu nachokipenda dunia hii kama ukweli na haki, hata uwe unaniumiza kiasi gani lakini ukiwa ukweli tu basi roho yangu inabaki kuwa kwatu kabisa!
Kuanzia muda fulani jana jioni, masaa machache baada ya matokeo ya kidato cha nne kutoka, habari iliyoenea na kusambaa kwa kasi ni kuhusu matokeo fulani ya shule kumi (10) dhaifu zaidi katika matokeo hayo ya jana ya kidato cha nne ambapo katika hizo tisa (9) zimetoka mkoa wa Mtwara. kwakuwa taarifa hiyo ilitolewa muda huhuo wa matokeo basi moja kwa moja ikahusishwa na matokeo ya 2020 na kama kawaida, 'wachambuzi' wakaibuka na chambuzi kedekede kuhusu mtwara na watu wake.
Kama utani nilianza kuona hilo kwenye group la rafiki yangu fulani ambae ni mkuu wa shule huko lindi (wana group lao wa wakuu kanda ya kusini) tulipokuwa tunajadili hayo matokeo. alinionyesha mjadala wao mule na jinsi gani wakuu wa mtwara wa shule tajwa walivyokuwa wanashangaa na kubishia hizo taarifa kwa kuyarusha matokeo yao ya mwaka 2020 (ikumbukwe kuwa mtwara na lindi ni ndugu wenye utani na ushindani kiasi flani hivyo hoja hii iliibua u-mtwara na u-lindi fulani baina yao) .
Nakumbuka mkuu mmoja mle akasema hayo matokeo ni ya 2016 na kuwataka wakuu wajiridhishe kwa kuyaangali matokeo ya shule tajwa ya mwaka 2016 wajionee wenyewe. yule rafiki akadowload matokeo ya shule mojawapo ya 2016 na kweli yalikuwa kama yanavyoonekana haya yanayotembea..... nikaachana nalo kwakuwa haikuwa interest yangu na wala siyo mnufaika na wa kwanza au mwisho lkn pia nikajua kwakuwa iko hivyo basi taarifa hii itakuwa imeshapuuzwa kitambo tu. tukahamia kwenye mada zingine.
Ilipofika usiku nikaingia zangu JF kuperuzi (kama kawaida yangu ya kila siku....ndo starehe yangu kuu). nilistuka kukuta threads za kutosha huko za habari hiyo...kama kawaida, watu wa mtwara walishambuliwa mno kwenye treads hizo na michango; malaya, wavivu, hawana akili n.k. Lindi pia haikubaki salama hapo, watu wake nao waliambulia matusi kibao. hiyo ni JF; kwenye wasomi, wachunguzi na wachambuzi mahili tu.
Leo tena, humu JF, mjadala huo umeendelea kwa kasi.....kila mmoja anasema anavyoweza. wapo waliojitokeza na kutoa taarifa kuwa hiyo habari siyo sahihi bila mafanikio; wakajitahidi hadi kutoa matokeo ya mwaka 2020 ya shule hizo bila mafanikio. mashambulizi ya kusini yakazidi. nilibaki kinywa wazi kwakweli, nilibaki kinywa wazi kwa sababu humu ni JF na siyo kitu kingine.
Mshangao wangu haukuegemea dhihaka na dharau za watu wa kusini, hapana! hilo lipo kila siku humu na ni nadra kupita mwezi usione thread ya kupondea kusini. mshangao ulikuwa kwenye kuvuma na kuaminika kwa hiyo habari hadi humu JF na jinsi wadau walivyokuwa wanajitahidi, kwa umakini mkubwa, kutoangalia au kusikiliza wale waliokuwa wanatoa taarifa sahihi.
Habari ikavuma mno na mkuu wa mkoa akaona isiwe tabu (maana alikuwa anaulizwa sana, bila shaka) akaamua, kitendo ambacho kwangu (labda kwakuwa elimu yangu ndogo) niliona ni cha busara mno, kuwaeleza waandishi wa habari waliofika ofisini kwake kuwa ameamua KUMUOMBA katibu mtendaji wa baraza la mitihani, KWAKUWA TAASISI YAKE NDIYO ILIYOTANGAZA NA NDIYO YENYE MAMLAKA YA KUKANUSHA KUTANGAZWA KWA ISICHOKITANGAZA. sijajua kama kuna protokali iliyonyooka zaidi ya hiii!
Mkuu wa mkoa huyu, baada ya kutoa taarifa hiyo, ametukanwa vya kutosha tu.....kilaza kama wananchi wake (eti 'anamuamrisha katibu wa baraza' ye kama nani? (ingawa mi nilichokisikia ni kuwa AMEMUOMBA)), nonsensical, anatumbuliwa huyu sasa hivi n.k. ikumbukwe kuwa kuna watu waliyarusha matokeo ya 2020 ya shule hizo tangu jana masaa kadhaa kabla ya mkuu wa mkoa kusema chochote.
Baraza lilipokanusha uvumi huo baadae leo; wachangiaji, kwa makusudi nafikiri, wanasema kuwa 'baraza limefuta na kupanga tena'......dah, HII DUNIA HII, acha tu!
Poleni wana Mtwara na kusini kwa ujumla, mna gundu hampendeki wala hamna sifa ya kusifiwa. kwangu JF naiheshimu sana na ni kipimo kizuri tu cha yanayoendelea. kushadadiwa huku kwa habari fake kama hii na KUTOTAKA KABISA KUGEUZA, ANGALAU KIDOGO, KWA SHINGO ZAO KUUTAKA UKWELI ULIO WAZI KABISA ni ushahidi tosha kwa nikisemacho kwa watu wa kusini,,,,mna gundu. gundu sugu! hebu oneni:-
1. Hakuna yeyote anayezungumza kuhusu kupanda kwa ufaulu wa halmashauri ya Manispaa ya Mtwara.
2. Hakuna yeyote anayezungumzia kushika nafasi ya pili kwa mkoa wa lindi katika matokeo ya darasa la nne 2020.
3. Hakuna yeyote anayezungumza chochote kuhusu kupanda kwa ufaulu wa kidato cha pili kwa mkoa wa lindi kwa miaka mitatu mfululizo.
4. Hakuna yeyote anayezungumza chochote kuhusu kupanda kwa ufaulu wa kidato cha nne kwa miaka mitatu mfululizo kwa mkoa wa Lindi.
5. Hakuna yeyote anaesema chochote kuhusu mafanikio haya yaliyoanza kuonekana yanachagizwa na R.E.O ambaye pia ni mtu wa kusini huko huko.....hakuna!
Poleni wanu Mtwara, poleni wanakusini!