SautiYaMnyonge
JF-Expert Member
- May 13, 2018
- 439
- 742
Miezi 8 si haba. Lakini wako UAMSHO walikaa miaka 9. Kwa hiyo kama kuumia mtani hujawafikia UAMSHO.
Ningefurahi ukawaiga UAMSHO. Hakika wameonesha hekima kubwa toka waachiwe huru. Wamejirudi.
La muhimu ni namna walivyo "behave" walipoachiliwa. Hatukuwasikia wakituambia unayotuambia mtani. Unafikia hata kumuudhi aliyekusamehe! Kwamba hakuna aliyekuhurumia bali umetoka kwa nguvu ya umma? Really? Ipi? Ni nguvu ipi ya umma unafanya kazi kwenye kutoa watu jela lakini inashindwa kuzuia watu wasiende jela? Mtaniii?
Mtani ushakuwa mtu mzima na uzee ushabisha hodi. Haipendezi kila siku uwe wa vituo vya polisi, jela na mahakamani ! Mtani kuna marafiki wa kweli na kuna wapambe! Hebu tusikilize marafiki wa kweli.
Achana na siasa fanya biashara. Na kama siasa ndio biashara yako basi acha siasa za kibabe. Hazilipi kwa kuwa sifa ya ubabe ni sifa ya serikali zoote duniani. Hakuna chombo au mtu anaweza kuwa mbabe kuliko serikali.
Dai chochote kwa kistaarabu utaeleweka. Serikali kuiambia hupoi, mpaka kieleweke, una kiberiti, utafanya nchi iwe Libya, n. k. haifai. Serikali ina uwezo wa kufanya hicho kibiriti kikuchome mwenyewe! Serikali ina uwezo wa kufanya wéwé peke yako uishi kama uko Libya!
Mtani hakuna sifa ya mtu kutembelewa na watu wengi gerezani, Sawa na mgonjwa ajisifie kutembelewa na watu wengi kitandani akiwa wodini It's an illusion! Haimfanyi awe mgonjwa bora kuliko wagonjwa wengine!
Mtani miaka inasonga hairudi nyuma. Na ukweli ni kuwa bado hauna hiyo "nguvu ya umma". Wenye nguvu ya umma hawakamatwi usiku, wakasafirishwa usiku, wakakaa ndani miezi 8 Huku wenzake wanachomudu ni kuvaa t-shirt zenye hukumu!
Sikupenda walichofanya UAMSHO lakini nimependa busara zao baada ya kuachiwa. Ukiziiga utakuwa salama. Ukifuata wapambe basi utatembelewa tena jela. Na hao wapambe watalala na kula makwao wewe ukilia njaa. Jela hakujawahi kuwa kuzuri hivyo sio mahali pakupenda kwenda.
Wenzako wanaokupa moyo Mtani kina Godbless Lema na Tundu Lissu wapo ughaibuni wanakula maisha na kuendesha shughuli zao huku wakilipwa madola kila mwezi. Usiwe mjinga, jua limezama shtuka!
Umelia kwa uchungu sana Mtani kila uliposimulia miezi yako 8 jela, itoshe kusema imekufunza. Ogopa mwanaume kulia kwa kiwango kile tena mbele ya umati akiwa na mke wake kando yake.
Anyway, akili ni nywele!
Ningefurahi ukawaiga UAMSHO. Hakika wameonesha hekima kubwa toka waachiwe huru. Wamejirudi.
La muhimu ni namna walivyo "behave" walipoachiliwa. Hatukuwasikia wakituambia unayotuambia mtani. Unafikia hata kumuudhi aliyekusamehe! Kwamba hakuna aliyekuhurumia bali umetoka kwa nguvu ya umma? Really? Ipi? Ni nguvu ipi ya umma unafanya kazi kwenye kutoa watu jela lakini inashindwa kuzuia watu wasiende jela? Mtaniii?
Mtani ushakuwa mtu mzima na uzee ushabisha hodi. Haipendezi kila siku uwe wa vituo vya polisi, jela na mahakamani ! Mtani kuna marafiki wa kweli na kuna wapambe! Hebu tusikilize marafiki wa kweli.
Achana na siasa fanya biashara. Na kama siasa ndio biashara yako basi acha siasa za kibabe. Hazilipi kwa kuwa sifa ya ubabe ni sifa ya serikali zoote duniani. Hakuna chombo au mtu anaweza kuwa mbabe kuliko serikali.
Dai chochote kwa kistaarabu utaeleweka. Serikali kuiambia hupoi, mpaka kieleweke, una kiberiti, utafanya nchi iwe Libya, n. k. haifai. Serikali ina uwezo wa kufanya hicho kibiriti kikuchome mwenyewe! Serikali ina uwezo wa kufanya wéwé peke yako uishi kama uko Libya!
Mtani hakuna sifa ya mtu kutembelewa na watu wengi gerezani, Sawa na mgonjwa ajisifie kutembelewa na watu wengi kitandani akiwa wodini It's an illusion! Haimfanyi awe mgonjwa bora kuliko wagonjwa wengine!
Mtani miaka inasonga hairudi nyuma. Na ukweli ni kuwa bado hauna hiyo "nguvu ya umma". Wenye nguvu ya umma hawakamatwi usiku, wakasafirishwa usiku, wakakaa ndani miezi 8 Huku wenzake wanachomudu ni kuvaa t-shirt zenye hukumu!
Sikupenda walichofanya UAMSHO lakini nimependa busara zao baada ya kuachiwa. Ukiziiga utakuwa salama. Ukifuata wapambe basi utatembelewa tena jela. Na hao wapambe watalala na kula makwao wewe ukilia njaa. Jela hakujawahi kuwa kuzuri hivyo sio mahali pakupenda kwenda.
Wenzako wanaokupa moyo Mtani kina Godbless Lema na Tundu Lissu wapo ughaibuni wanakula maisha na kuendesha shughuli zao huku wakilipwa madola kila mwezi. Usiwe mjinga, jua limezama shtuka!
Umelia kwa uchungu sana Mtani kila uliposimulia miezi yako 8 jela, itoshe kusema imekufunza. Ogopa mwanaume kulia kwa kiwango kile tena mbele ya umati akiwa na mke wake kando yake.
Anyway, akili ni nywele!