Pole sana Mh.ZITTO kumbe na wewe hutumii chandarau!

Nachukua nafasi hii kumpa pole MPIGANAJI MACHACHARI WA MASLAHI YA TAIFA HILI....Mh. ZITTO, POLE SANA! Pamoja na hayo,uchunguzi wa kitabibu umeonyesha anasumbuliwa na malaria (vidudu 120)! Ni mara nyingi viongozi wetu wamekuwa wakisisitiza suala la utumiaji wa vyandarua tena vyenye dawa na kwa nia thabiti ya kukomesha malaria nchini,mkuu wa nchi aliwahi kupokea TAKRIMA ya vyandarua alipotembelewa na swahiba wake, George BUSH! Hoja yangu, watu wengi wanasumbuliwa na malaria hadi sasa japo vyandarua vimejaa kila kona na kuna uhamasishaji wa kutosha,tuamini havina uwezo wa kutukinga na malaria au watu tumepuuza kuvitumia!!!?

Mbu wanashambulia sehemu yoyote si wakati wa kulala tuu. Hata ukiwa kwenye mkusanyiko wa vikao vya misiba, harusi vinavyofanyika maeneo ya wazi kama bustanini uwezekano wa kuumwa na mbu ni mkubwa sana. Tuombe tu ipatikane chanjo lakini chandarua inazuia wakati umelala tuu
 
Acha kukurupukia hoja kwa kuandika vitu usivyovijua wala kuwa na ushahidi navyo.Basi hao wataalamu kama wangekuwa wanajua hilo wasingekuwa wanatoa ushauri wa kutumia net kama kinga madhubuti dhidi ya malaria.Wamefanya utafiti ndio wakaja na hiyo suluhu.
Kwenye hiyo statement yako leta chanzo cha hiyo tafiti yako.Wewe kwa kuwa ni mshabiki wa Zitto unachangia hoja kishabikikwani

hawajui sasa...mimi ndo nakwambia.
 
Serikali ya CCM imejipanga vema kuakikisha kila mwananchi anapata chandarua cha bure kwaiyo mh. Zitto asisite kupokea. zamu kigoma ikifika. kweli malaria haichagui POLE MH. ZITTO.

Zitto hana chandalua wakati zinagawiwa yeye alikua Bungeni.
Pole kamanda.
 
Nadhani AZA una matatizo ya kimombo! Document alio download bwana Karata ni valid kabisa. Ndio maana hapa Tanzania juzi tumezindua dawa ya chanjo ya malaria ili kusaidiana na njia nyingine za kujikinga na ugonjwa wa malaria. Jamani someni magazeti basi kama hamuwezi kwenda wizarani! Kwasasa hivi, kuna tafiti nyingi ambazo zinafanyika kuhusu hao mbu na resistance ya insecticides.
Kuhusu vyandarua vidogo hapo uko sahihi, lakini huenda wewe sio mlengwa kabisa. Kwanza una uwezo wa kuburuza hapa mtandao which means una uwezo wa kifedha. Una kitanda cha futi sita kwa sita, na godolo lake! Vyote hivyo thamani yake ni Tsh.. Laki Nne na Ushee (kama anavyosema Waziri Mkuu wetu!) Sasa unashindwa kununua chandarua cha elfu nane? Acha kulalamika chukua hatua! Watanzania tumekua na tabia mbovu sana tena hatuna aibu kulalamika lalamika huku!
 
KAGOSAKI...
sijivunii eti kujua au kutokujua kimombo,si lugha yangu ni lugha za kigeni tu
ata kama una ubia nao uo ndo ukweli na vyandarua vyenu vya "bush"havina maana na mnapotosha wanainchi
ndo mana nakwambia kwamba ata km nna uwezo wa kununua nini alikwambia sina neti ni nani?ss izo neti ndo zinaua mazalia ya mbu?zinazuia malaria???wacha maneno yako bwana,neti si suluhisho na uo mpango wenu wa kunyunyiza dawa haujafikia mamilioni ya watu,mnachofanya labda mmechagua sensa ya mahali fulani-fulani tu afu mtatulia...
tunasema ivi leteni hapa iyo mipango yenu ya njia zingine mbadala ya kutokomeza malaria kbs na sio izi neti zenu za bure,sizizo na faida
 
Mwenzetu unavaa nguo za chandarua nini?

naona uyu mtu anazo labda...anatembea nazo asubuhi to usiku na kuamka nazo...
halafu izo neti zinatolewa kwa kuhesabu vitanda???na kama kuna watoto???
kama una watoto 10 wanatoa neti 10????uyu kagosaki atembee aone sio kukaa ofisini akipunga kiyoyozi
 
AZA....
Nakushukuru ila mimi siwezi kukuletea mipango kwakuwa ipo kwenye ilani ya chama changu cha CCM. Ninachofanya ni kufuatilia utelekelezaji wa Ilani ya Chama changu ndio maana nafahamu sana kuhusu utekelezaji wa sera za wizara ya afya. CCM hoyeee!

Nawasilisha..
 
vyandarua vya BUSH ni fut 4 na vitanda vya waheshimiwa ni fut 6,hii si issue sana fact ni kuwa mtu kama zito hulala too late akiwa amechoka mno na kwa vile hana mke(labda kaoa kimya kimya)kung'atwa mbu ni rahisi sana,akijitupa tu usingizi hakumbuki kushusha net wadudu 120 ni wengi sana,pole mh.nyepesi,jifunze kutokana na makosa

Nachukua nafasi hii kumpa pole MPIGANAJI MACHACHARI WA MASLAHI YA TAIFA HILI....Mh. ZITTO, POLE SANA! Pamoja na hayo,uchunguzi wa kitabibu umeonyesha anasumbuliwa na malaria (vidudu 120)! Ni mara nyingi viongozi wetu wamekuwa wakisisitiza suala la utumiaji wa vyandarua tena vyenye dawa na kwa nia thabiti ya kukomesha malaria nchini,mkuu wa nchi aliwahi kupokea TAKRIMA ya vyandarua alipotembelewa na swahiba wake, George BUSH! Hoja yangu, watu wengi wanasumbuliwa na malaria hadi sasa japo vyandarua vimejaa kila kona na kuna uhamasishaji wa kutosha,tuamini havina uwezo wa kutukinga na malaria au watu tumepuuza kuvitumia!!!?
 
nilikuwa cjui kumbe ukitumia chandarua ndo hupati malaria??!!!!
mbona mie ctumii net na malaria kwangu ni hadithi?????
 
mkuu,nadhani hujafuatilia maelezo ya kitaalamu kuhusu malaria inavyo ambukizwa; tunaambiwa mbu aambukizaye malaria anaogopa mwanga hivyo ukiwa mezani au sebuleni unaangalia AlJAZERA au unafanya ibada na watoto,hapo hakuna malaria kwani kuna taa hivyo hao mbu waenezao malaria hawasogei! Wao hupatikana zaidi kukiwa na giza tena usiku wa manane! Ndio maana tunasisitizwa tutumie net usiku kwa kinga madhubuti dhidi ya malaria! Au chenga tu, tuamini ni biashara au!

Mkuu hili nalo neno la uzima!!
 
Inahitajika kampeni ya uhakika ya kutokomeza mbu waletao malaria na si kuwa na kauli mbiu zisizokwisha bila utekelezaji, Mbona Zanzibar wameweza?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom