mbingunikwetu
JF-Expert Member
- Feb 17, 2015
- 13,651
- 18,021
Kulikuwa na suala la kupata ndege za kivita ili kupeleka Ukraine zikasaidie kupambana na Urusi. Nchi zote zikaingia baridi, halafu Marekani ikasema inafanya majadiliano na Poland ili ikubali kupeleka ndege zake Ukraine. Poland hakutaka kumkatisha tamaa Marekani, ila ikamwambia kuwa haiwezi kuzipeleka moja kwa moja Ukraine kutokea Poland isije ijikuta kwenye midomo ya Putin.
Ila Poland ikasema nitazipeleka hizo ndege na kuzikabidhi kwa Marekani kwenye kambi ya Marekani iliyoko Ujerumani TENA BILA GHARAMA! Halafu Marekani kama ina ubavu huo ndio izipeleke hizo ndege huko Ukraine!
Marekani kuona hivyo ikaruka kimanga!! Tuambizane ukweli, hakuna mwenye ubavu wa kujitumbukiza kwenye midomo ya Putin. Ikasema SIWEZI KUFANYA HIVYO!!
Sasa najiuliza, wakati Marekani inaiambia Poland (mwanachama wa NATO) kuwa ipeleke ndege zake Ukraine haikuwa inajua kuwa itaziingia nchi za NATO kwenye vita na Urusi? Ila kwa sasa Marekani ilipoambiwa yenyewe ndiyo izipeleke ndo inajua kuwa itaziingiza NATO vitani na Urusi??
Mchezo uko hivi: Putin aliipigia simu Poland kuitonya kuwa usijaribu kuleta ndege zako Ukraine, iambie Marekani kama ina ubavu izilete yenyewe!! Ona hapa!
A plan under which the US would transfer Polish-owned planes to Ukraine risks dragging NATO directly into a military conflict between Kiev and Moscow, the Pentagon said, as it seemingly rejected a deal earlier proposed by Warsaw.
On Tuesday, Poland announced that it was ready to deploy “immediately and free of charge” its fleet of MiG-29 jets to a NATO base in Germany and hand them over to the US military.
Marekani kwa suala hili imepata aibu sana!! Ni sawa na baba mtu aliposikia kuna sauti ya hatua za mtu akitembea kuzunguka nyumba yake usiku halafu akamtuma mtoto atoke nje kwenda kuangalia ni kitu gani. Mtoto akamjibu baba kuwa hawezi maana anaogopa, ila ataenda kufungua mlango ili baba mwenyewe atoke nje!!
Baba kuambiwa hivyo akasema, "mwanangu kutoka nje usiku ni hatari sana kwa maisha yetu wote hapa nyumbani". Sasa mtoto atabaki akijiuliza hii hatari ameijua saa ngapi? Wakati ananiambia mimi nitoke hakuwa anajua hatari hiyo?
Kumtegemea baba wa hivyo yatakukuta yaliyomkuta Rais Zelensky wa Ukraine, alivimbishwa kichwa kwa kuahidiwa kujiunga na NATO na kupewa vimsaada vya kijeshi ambavyo mpaka sasa vimeshasambaratishwa!
Ila Poland ikasema nitazipeleka hizo ndege na kuzikabidhi kwa Marekani kwenye kambi ya Marekani iliyoko Ujerumani TENA BILA GHARAMA! Halafu Marekani kama ina ubavu huo ndio izipeleke hizo ndege huko Ukraine!
Marekani kuona hivyo ikaruka kimanga!! Tuambizane ukweli, hakuna mwenye ubavu wa kujitumbukiza kwenye midomo ya Putin. Ikasema SIWEZI KUFANYA HIVYO!!
Sasa najiuliza, wakati Marekani inaiambia Poland (mwanachama wa NATO) kuwa ipeleke ndege zake Ukraine haikuwa inajua kuwa itaziingia nchi za NATO kwenye vita na Urusi? Ila kwa sasa Marekani ilipoambiwa yenyewe ndiyo izipeleke ndo inajua kuwa itaziingiza NATO vitani na Urusi??
Mchezo uko hivi: Putin aliipigia simu Poland kuitonya kuwa usijaribu kuleta ndege zako Ukraine, iambie Marekani kama ina ubavu izilete yenyewe!! Ona hapa!
A plan under which the US would transfer Polish-owned planes to Ukraine risks dragging NATO directly into a military conflict between Kiev and Moscow, the Pentagon said, as it seemingly rejected a deal earlier proposed by Warsaw.
On Tuesday, Poland announced that it was ready to deploy “immediately and free of charge” its fleet of MiG-29 jets to a NATO base in Germany and hand them over to the US military.
Marekani kwa suala hili imepata aibu sana!! Ni sawa na baba mtu aliposikia kuna sauti ya hatua za mtu akitembea kuzunguka nyumba yake usiku halafu akamtuma mtoto atoke nje kwenda kuangalia ni kitu gani. Mtoto akamjibu baba kuwa hawezi maana anaogopa, ila ataenda kufungua mlango ili baba mwenyewe atoke nje!!
Baba kuambiwa hivyo akasema, "mwanangu kutoka nje usiku ni hatari sana kwa maisha yetu wote hapa nyumbani". Sasa mtoto atabaki akijiuliza hii hatari ameijua saa ngapi? Wakati ananiambia mimi nitoke hakuwa anajua hatari hiyo?
Kumtegemea baba wa hivyo yatakukuta yaliyomkuta Rais Zelensky wa Ukraine, alivimbishwa kichwa kwa kuahidiwa kujiunga na NATO na kupewa vimsaada vya kijeshi ambavyo mpaka sasa vimeshasambaratishwa!