POCHI LA MAMA KUJENGA ZAHANATI KILA KIJIJI:
Waziri wa Nchi ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na serikali za Mitaa Mheshimiwa Ummy Mwalimu amesema Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan anakusudia kujenga zahanati kila kijiji Nchi nzima ili kuongeza huduma za Afya jirani na wananchi Zaidi.
Akizungumza Kwenye kikao cha Ndani kilichowakutanisha wakuuu wa Idara na Baraza la madiwani Wa Halmashauri ya Chalinze wilayani Bagamoyo Waziri Ummy amewataka madiwani wawahakikishie wananchi wao Kupitia mikutano ya Hadhara kwamba serikali ya awamu ya Sita Chini ya Rais Samia inayo dhamira ya dhati ya kuondoa changamoto za huduma za Jamii ikiwemo Afya, Elimu na Barabara
"Nataka niwahakikishie ndugu zangu madiwani, Rais Samia amekusudia kujenga zahanati Kwenye kila kijiji Nchini na kama alivyosema yeye ni mtu wa matendo Zaidi kuliko maneno hivyo Nendeni mkawaambie wananchi Kwenye mikutano ya Hadhara dhamira hii njema ya Rais wetu" alisema Ummy Mwalimu
Waziri wa Nchi ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na serikali za Mitaa Mheshimiwa Ummy Mwalimu amesema Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan anakusudia kujenga zahanati kila kijiji Nchi nzima ili kuongeza huduma za Afya jirani na wananchi Zaidi.
Akizungumza Kwenye kikao cha Ndani kilichowakutanisha wakuuu wa Idara na Baraza la madiwani Wa Halmashauri ya Chalinze wilayani Bagamoyo Waziri Ummy amewataka madiwani wawahakikishie wananchi wao Kupitia mikutano ya Hadhara kwamba serikali ya awamu ya Sita Chini ya Rais Samia inayo dhamira ya dhati ya kuondoa changamoto za huduma za Jamii ikiwemo Afya, Elimu na Barabara
"Nataka niwahakikishie ndugu zangu madiwani, Rais Samia amekusudia kujenga zahanati Kwenye kila kijiji Nchini na kama alivyosema yeye ni mtu wa matendo Zaidi kuliko maneno hivyo Nendeni mkawaambie wananchi Kwenye mikutano ya Hadhara dhamira hii njema ya Rais wetu" alisema Ummy Mwalimu
Waziri Ummy anaendelea na ziara za kukagua Utekelezaji wa miradi ya maendeleo iliyo Chini ya Ofisi ya Rais TAMISEMI Kwenye Halmashauri mbalimbali Nchini.