please!ujuaji wako ni muhimu sana kwa hili.

x - mas

JF-Expert Member
Oct 5, 2012
914
597
Amani
iwe nanyi,tafadhali kwa yeyote anaye jua baada ya mwalimu kuandika
barua ya kuomba kuhama mkoa ni hatua zipi zinafuata hadi kufanikiwa
kupata uhamisho huo?na nisababu zipi zinafanya mwalimu anyimwe
uhamisho?je,ni muda gani muhafaka wa mwalimu kuomba uhamisho?ASANTE KWA
KUSOMA NI MATUMAINI YANGU UTATHAMINI SHIDA YANGU NITAPATA MAJIBU MAZURI.
 
Natumaini Waalimu watakuja kukufahamisha, ila binafsi naomba rekebisha kichwa cha habari kwa kuondoa neno ujuaji. Tumia neno mbadala wa hilo .
 
Amani
iwe nanyi,tafadhali kwa yeyote anaye jua baada ya mwalimu kuandika
barua ya kuomba kuhama mkoa ni hatua zipi zinafuata hadi kufanikiwa
kupata uhamisho huo?na nisababu zipi zinafanya mwalimu anyimwe
uhamisho?je,ni muda gani muhafaka wa mwalimu kuomba uhamisho?ASANTE KWA
KUSOMA NI MATUMAINI YANGU UTATHAMINI SHIDA YANGU NITAPATA MAJIBU MAZURI.

Baada ya kuandika barua ya uhamisho na kuiwasilisha sehemu husika,hakuna muda maalum wa ombi lako kukubaliwa!!!ila inapaswa ujibiwe mara tu baada ya kuwasilisha barua yako!

Kisheria unaweza kuomba kuhama kituo cha kazi endapo umeshatumikia eneo husika kwa kipindi kisichopungua miaka mitano na kuendelea!

Kinachofanya mtumishi wa umma anyimwe uhamisho ni kuzingatia ikama ya ofisi husika!mfano,shule unayofundisha ina walimu 17 na inahitaji walimu 20,ww ukihama basi ikama ya shule hiyo itazidi kupungua ,hivyo mwajiri anaruhusiwa kukunyima uhamisho ili kulinda ikama ya ofisi husika!!!lkn km shule inahitaji walimu 25 halafu ina walimu 30,hapo ukiomba uhamisho utapewa fasta kwani hata ukihama hutoharibu ikama ya shule hiyo!

Ila kumbuka,uhamisho wa kuuomba mwenyewe hauna malipo,hutopewa disturbance allowance wala pesa ya mizigo,utajigharamia mwenyewe kila kitu!!

Kwa maelezo zaidi waone watumishi wa TSD na pia onana na DEO ili akupe uchambuz yakinifu wa maswala ya uhamisho kwa mujib wa standing order ya mwaka 2009!

Nawasilisha!!
 
asanteni kwa maelezo yenu mazuri lakini samahanini naomba niulize tena je,kunahaja ya kusuburia miaka mitano ndio uhamisho uombe hata kwa mwl anaye sumbuliwa na maladh au mwl.aliyepata mwenzake wa kubadilisha vitio vya kazi?
 
Nataraji sina ujuaji, si kwa hili tu bali hata kwenye mengine
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom