Pitia hapa kama wewe ni graduate

Bess

JF-Expert Member
Oct 4, 2016
542
649
Kijana mmoja,Graduate ana hekari kadhaa za shamba pale Morogoro, analima na kupeleka mazao yake moja kwa moja sokoni.

Ana supply chakula kwa vijana wanaolalamika kila kukicha CCM imesababisha umaskini wao., amesikia pia fursa za kupanda miti na Ufugaji anataka kuzijaribu. Simu yake anatumia kibiashara kutafuta masoko mitandaoni. E-business imeimarisha sana biashara yake.

Somo: Usomi sio kujua siasa, tuwaachie wale wenye traits za siasa wapige siasa; sisi tusiozijua tukapige kaz. Tuwe tunabishana soko lipi bora kwa bidhaa tulizotengeneza au kuzalisha
 
kila msomi au kijana akiikimbilia siasa nchi itajengwa na nani??(serious)
Sikumaanisha wajiingize kwenye siasa ila waangalie fursa zingine.
Tatizo watu wamekomalia kilimo kama fursa pekee kila mtu kilimo kilimo sasa mnataka watanzania karibia wawe wakulima?
 
Hii nchi yangu bhana,hivi hawa vijana wamekosea nini?
Maana kila wakiuliza kuhusu ajira wanaambiwa wajiajiri tena kwenye kilimo cha jembe la mkono!!

Wamesoma mpaka vyuoni ili waajiriwe,wangetaka kujiajiri si mngewaambia wakomee kidato cha 4 tu.

Wapeni ajira bhana
 
Mbaya zaidi sio graduate wote wamesomea biashara ndio maana aliyebuni hii JF akaweka forums mbalimbali mfano siasa, mahusiano, biashara nk.
 
Hii nchi yangu bhana,hivi hawa vijana wamekosea nini?
Maana kila wakiuliza kuhusu ajira wanaambiwa wajiajiri tena kwenye kilimo cha jembe la mkono!!

Wamesoma mpaka vyuoni ili waajiriwe,wangetaka kujiajiri si mngewaambia wakomee kidato cha 4 tu.

Wapeni ajira bhana

Hapo kwenye red tuwekane sawa kidogo!

Hivi unadhani kila anayesoma mpaka Chuo kikuu anasoma ili aje kuajiriwa?.

Na pia kila anayekomea kidato cha nne kazi yao ni kujiajiri?.
 
Back
Top Bottom