Ukweli ni kwamba huwezi kuuza muda ukawa tajiri, mwenye nafasi ya kuwa matajiri au mafanikio makubwa kiuchumi ni yule tu, anae nunua muda. maana yake kuuza muda ni kuajiriwa na kununua muda ni kujiajiri au kuajiri. Hivyo hakikisha unakuwa salama kuwa mnunuzi wa muda wako kabla haujanunuliwa na mtu mwingine.Mkuu huu ndo ukweli unaotutesa. Binafsi nimeamua mwaka huu wa 2017 kuanzia January ya leo naingia mtaani kwa asilimia 100. Nimekuwa muajiriwa kwa miaka 3 sasa ila nimeona huko niendako ni giza zaidi. Nitakuja hapa December kwa neema ya Mungu kushuhudia yale nitakayokuwa nimekutana nayo.