Pita hapa kama unataka kujua chochote kuhusu biashara Kampala

Ni wazo tu jamani hivi kwanini mtu asianzishe uzi ambao utamuwezesha mtu kuchangia kuuhu jinsi alivyopata mafanikio yake ili wengine wapate kitu ila yawe ya njia halali
ANGALIZO: Huu ni ushauri tu
Vizuri Sana. Itatusaidia wengi
 
Wakuu nashukuru kwa hii mada.
Mfano mzigo milion 3 kamili naweza pata faida kiasi gani.
Asante
 
kingine kinachosaidia ni thamani ya hela tz na ug...ya kwetu ipo juu hivyo gharama zinakua sio kubwa sn ukilinganisha na nchi nyingine km Rwanda
 
Ndiyo, chukua ya mwaka mmoja (10,000/=)

east and central African unaweza tumia hio ya mwaka mmoja bila shida yoyote...ila km unafanya sana biashara chukua hio ya elfu 10 wkt huo una fanya application ya ile kubwa ya elfu 50 ili usihangaike kila mwaka kufuatilia hilo karatasi
 
Kingine hiyo biashara uchanganye nguo za kike na kiume, za kike ziwe nyingi kuliko za wanaume ambao si wavaaji kama wanawake pia wakopaji wazuri. Usisahau kununua chupi za kisasa hasa cotton, soma mazigira unayouzia kama kuna wadada wanapenda nguo za kimamtoni then waletee hizo. Ngoja nikipata muda takutumia business card za maduka ya nguo Kampala.
Mkuu nimevutiwa na maelezo yako naomba unitumie biz cards za hao dealers wa nguo kama hutojali whatsap no 0688939892
 
Maduka ya nguo ama bidhaa huwa yako sehemu moja lakini katika style ya Malls. Ukishuka kwenye basi na kufikia Hotel (Tanzania mnaita Guest house) waambie pale reception wakupatie kijana wa kukupeleka mjini (kukutembeza). Utamlipa shilling 15,000/=ya Uganda sawa na 9,000/= ya Tanzania. Siku nzima. Huyo mtu unayepewa lolote atakalokufanyiwa amedhaminiwa na hiyo Hotel, epuka wale wa mitaani ni wezi kuliko hata Watanzania. Baada ya safari mbili utakuwa mwenyeji. Sasa sijui mwezangu unaongea lugha gani lkn kama wewe ni Mhaya hakuna shida maana mnasikilizana na Waganda.
Mkuu unafaa sana maana unatupa maujanja kibao
 
Mie nilikuwa nafikia Rock Classic ni salama hata ukiacha mlango wazi na hivi majuzi wameongeza huduma nyingine ya tungi hivyo ukiwa mpenzi wa maji na watoto mbona utabadiri uraia huko huko.
Mkuu hiyo rock clasic vip gharama zake
 
Watu wenye roho za hivi ndo mlikuwa mnafaa hata kupewa uongozi hata kutawala nchi kwani unaonyesha kuwajali watu lakn tatizo nchi yetu kupata uongozi mpaka uwe na roho mbaya..!
Hii inatukumbusha stori ya Bwana yule aliye ukwaa uongozi kwa bahati nasibu.
 
Kampala ni hatari sana,,nlisoma hizi nyuzi zimenisaidia sana,,nimemaliza kufunga mzigo kesho narudi Tz,,ndani ya week nne ntarudi,,nimeona fursa nyiiingi,,naenda kujipanga nirudi na nguvu ya hatari
Long live Jf
 
Baada ya kusoma nyuzi nyingi za biashara na kampala nikaamua kuja kujionea,,nimepanda bus la friends mpaka kampala,,through research nikawa najua where to go kupata vitu navohitaji,,nafanya biashara ya nguo,,vitu ni vingi na vizuri,,bei sio kubwa kama dar nahisi sababu ya thamani ya pesa yao,,watu wa hotel niliyofikia wako very friendly pia,,nguo,viatu,vyombo ,,mashuka etc,,nauli sio gharama,,so kwa ufupi naona ukikazana unatoka
 
Ni wazo tu jamani hivi kwanini mtu asianzishe uzi ambao utamuwezesha mtu kuchangia kuuhu jinsi alivyopata mafanikio yake ili wengine wapate kitu ila yawe ya njia halali
ANGALIZO: Huu ni ushauri tu
Lakini pia kumbuka maisha ni siri
 
Huko naskia ni balaa... Eti dar haikamati hata kidogo kwenye biashara..kuna mtu nilikua namshangaa anatoka dar kwenda kuchkua mzigo kampala...yeye ndo akanishangaa zaid..ipo cku ntaenda kujionea... Naskia hawana mabidhaa feki kama bongo..halafu fashion mpya znaanzia kule eti
Kweli kabisa fashion mpya zinaanzia huko
 
Back
Top Bottom