Pingamizi la Dr Slaa dhidi ya Rose Kamili lakataliwa mahakamani

Ritz

JF-Expert Member
Jan 1, 2011
46,903
32,312
Wanabodi,



Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam, imetupilia mbali kwa gharama pingamizi lilowasilishwa mbele yake na Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dkt. Willbrod Slaa lililokuwa likiomba mahakama hiyo ifute kesi ya madai iliyofunguliwa na ‘mkewe’ Rose Kamili Slaa nee Sukum, akiomba mahakama hiyo imzuie ‘mumewe’ Dkt. Slaa asifunge ndoa na mchumba wake Josephine Mushumbusi.

Uamuzi huo ulitolewa na Jaji Laurnce Kaduri ambaye alisema amepitia kwa kina pingamizi lilowasilishwa na Dkt. Slaa na majibu yaliyojibiwa na mlalamikaji Rose anayetetewa na wakili wa kujitegemea Joseph Thadayo na amefikia uamuzi wa kuona hoja zilizowasilishwa mbele yake na Dkt. Slaa zikiomba mahakama hiyo iifute kesi ya msingi iliyofunguliwa na Rose, ni dhahifu na hivyo amezitupilia mbali.

Jaji Kaduri alisema Dkt. Slaa alikosea kudai kuwa Rose hakuwa na haki ya kufungua kesi hiyo ya kumzuia asifunge ndoa na mchumba wake Josephine kwa taratibu za kisheria kwa sababu Slaa na Rose hawakuwai kufunga ndoa ila kulikuwa na dhana ya ndoa.

“Mahakama hii inaitupilia mbali, tena kwa gharama, pingamizi hilo la Dkt. Slaa linalosema kuwa Rose hakuwa na haki ya kupinga ndoa yake kwa sababu hakuwa mke wake na wala hawajawai kufunga ndoa, kwa sababu sheria ya ndoa inasema mtu ambaye umeishawahi kuishi kama mke na mume kwa zaidi ya miaka miwili, sheria inawahesabu kama ni wanandoa, hivyo Mahakama hii inasema Rose ana haki ya kufungua kesi ya kuzuia ndoa ya wadaiwa, yaani Slaa na Josephine na mahakama inatupilia mbali pingamizi la Slaa,” alisema Jaji Kaduri.

Kesi ya msingi itatajwa mahakamani hapo Novemba 6 mwaka huu.


  1. Kesi hiyo ya madai ya ndoa Na.4/2012 ilifunguliwa mahakamani hapo na Rose dhidi ya Dkt. Slaa na Josephine kwa mara ya kwanza mapema Julai mwaka huu, akiiomba mahakama isikubali shauri hilo lipelekwe kwenye Bodi ya Maridhiano ya Masuala ya Ndoa ya kwa ajili ya kupatanishwa.
  2. Dai la pili, Rose anaiomba mahakama itanganze yeye na Dkt. Slaa bado ni wanandoa.
  3. Dai la tatu, anaiomba mahakama itamke kuwa ndoa baina yake na Dkt. Slaa bado ni halali kisheria na kwamba ndoa nyingine itakayofungwa kinyume na sasa ndoa hiyo itakuwa ni batili.
  4. Katika dai lake nne, mlalamikaji ambaye ni Mbunge wa Viti Maalum (CHADEMA) anadai mdaiwa wa pili (Josephine) alimshawishi mumewe (Dkt. Slaa) kuivuruga ndoa yake na mumewe ambaye ni mdaiwa wa kwanza.

“Pia, nia ya wadaiwa hao wawili ya kutaka kufunga waliyopanga ifungwe Julai 21 mwaka huu katika eneo lolote lile, ndoa hiyo ihesabike kuwa ni batili”

Aidha anaiomba mahakama iwaamuru wadaiwa wamlipe fidia ya shilingi 50,000,000 kama gharama za matunzo ya watoto watoto wawili ambao Emiliana Slaa na Linus Slaa aliyezaliwa mwaka 1987 na kwamba walianza kuishi pamoja na Dkt. Slaa kama mume na mke, ambao amekuwa akiwahudumia kwa tangu mwaka 2009 baada ya mume wake kumkimbia.

Pia anaiomba mahakama imwamuru mdaiwa wa pili (Josephine) amlipe fidia ya Shilingi 500,000,000 kwasababu alimsababishia usumbufu mkubwa na kumharibia ndoa yake.

Akaongeza kuiomba mahakama hiyo impatie nafuu nyingine ambazo itaona inafaa.

Source: wavuti.com - wavuti
 
minyoo.jpg

mkuu unawazaga vitu viwili tu.........Dr.Slaa na Ukiristo
 
Ndoa kati ya Dr Slaa na Rose Kamili ilifungwa wapi, na lini?
 
Ndoa kati ya Dr Slaa na Rose Kamili ilifungwa wapi, na lini?

Sheria inahesabu kuwa mwanaume akiishi na mwanamke kwa miaka miwili au zaidi hao ni wanandoa regardless wana watoto au laa.... Mbaya zaidi Dr. Slaa kazaa ma Rose watoto 2, kaazi kweli.... yaani patamu hapo..
 
  • Thanks
Reactions: FJM
Mungu yupo pamoja na Mama yetu Rose Kamili.
 
Wanabodi,



Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam, imetupilia mbali kwa gharama pingamizi lilowasilishwa mbele yake na Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dkt. Willbrod Slaa lililokuwa likiomba mahakama hiyo ifute kesi ya madai iliyofunguliwa na ‘mkewe' Rose Kamili Slaa nee Sukum, akiomba mahakama hiyo imzuie ‘mumewe' Dkt. Slaa asifunge ndoa na mchumba wake Josephine Mushumbusi.

hahaha ... huyu jamaa alafu anataka kuja kuongoza nchi!.. while ku control hao wanawake wawili wakakaa wakayamaliza hawezi...

slaa ni more than mchekeshaji ..
 
Here we go again, tuko busy na fujo za ndugu zako wanazoendelea kuzifanya katika taifa letu hili la amani na hasa waloyafanya leo Dar na Zanzibar we uko busy na ndoa za watu? "Harusi siyo yako we waishonea suti?". Well miafrica ndivyo tulivyo Ritz
 
Last edited by a moderator:
Wanabodi,



Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam, imetupilia mbali kwa gharama pingamizi lilowasilishwa mbele yake na Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dkt. Willbrod Slaa lililokuwa likiomba mahakama hiyo ifute kesi ya madai iliyofunguliwa na ‘mkewe’ Rose Kamili Slaa nee Sukum, akiomba mahakama hiyo imzuie ‘mumewe’ Dkt. Slaa asifunge ndoa na mchumba wake Josephine Mushumbusi.

Uamuzi huo ulitolewa na Jaji Laurnce Kaduri ambaye alisema amepitia kwa kina pingamizi lilowasilishwa na Dkt. Slaa na majibu yaliyojibiwa na mlalamikaji Rose anayetetewa na wakili wa kujitegemea Joseph Thadayo na amefikia uamuzi wa kuona hoja zilizowasilishwa mbele yake na Dkt. Slaa zikiomba mahakama hiyo iifute kesi ya msingi iliyofunguliwa na Rose, ni dhahifu na hivyo amezitupilia mbali.

Jaji Kaduri alisema Dkt. Slaa alikosea kudai kuwa Rose hakuwa na haki ya kufungua kesi hiyo ya kumzuia asifunge ndoa na mchumba wake Josephine kwa taratibu za kisheria kwa sababu Slaa na Rose hawakuwai kufunga ndoa ila kulikuwa na dhana ya ndoa.

“Mahakama hii inaitupilia mbali, tena kwa gharama, pingamizi hilo la Dkt. Slaa linalosema kuwa Rose hakuwa na haki ya kupinga ndoa yake kwa sababu hakuwa mke wake na wala hawajawai kufunga ndoa, kwa sababu sheria ya ndoa inasema mtu ambaye umeishawahi kuishi kama mke na mume kwa zaidi ya miaka miwili, sheria inawahesabu kama ni wanandoa, hivyo Mahakama hii inasema Rose ana haki ya kufungua kesi ya kuzuia ndoa ya wadaiwa, yaani Slaa na Josephine na mahakama inatupilia mbali pingamizi la Slaa,” alisema Jaji Kaduri.

Kesi ya msingi itatajwa mahakamani hapo Novemba 6 mwaka huu.


  1. Kesi hiyo ya madai ya ndoa Na.4/2012 ilifunguliwa mahakamani hapo na Rose dhidi ya Dkt. Slaa na Josephine kwa mara ya kwanza mapema Julai mwaka huu, akiiomba mahakama isikubali shauri hilo lipelekwe kwenye Bodi ya Maridhiano ya Masuala ya Ndoa ya kwa ajili ya kupatanishwa.
  2. Dai la pili, Rose anaiomba mahakama itanganze yeye na Dkt. Slaa bado ni wanandoa.
  3. Dai la tatu, anaiomba mahakama itamke kuwa ndoa baina yake na Dkt. Slaa bado ni halali kisheria na kwamba ndoa nyingine itakayofungwa kinyume na sasa ndoa hiyo itakuwa ni batili.
  4. Katika dai lake nne, mlalamikaji ambaye ni Mbunge wa Viti Maalum (CHADEMA) anadai mdaiwa wa pili (Josephine) alimshawishi mumewe (Dkt. Slaa) kuivuruga ndoa yake na mumewe ambaye ni mdaiwa wa kwanza.

“Pia, nia ya wadaiwa hao wawili ya kutaka kufunga waliyopanga ifungwe Julai 21 mwaka huu katika eneo lolote lile, ndoa hiyo ihesabike kuwa ni batili”

Aidha anaiomba mahakama iwaamuru wadaiwa wamlipe fidia ya shilingi 50,000,000 kama gharama za matunzo ya watoto watoto wawili ambao Emiliana Slaa na Linus Slaa aliyezaliwa mwaka 1987 na kwamba walianza kuishi pamoja na Dkt. Slaa kama mume na mke, ambao amekuwa akiwahudumia kwa tangu mwaka 2009 baada ya mume wake kumkimbia.

Pia anaiomba mahakama imwamuru mdaiwa wa pili (Josephine) amlipe fidia ya Shilingi 500,000,000 kwasababu alimsababishia usumbufu mkubwa na kumharibia ndoa yake.

Akaongeza kuiomba mahakama hiyo impatie nafuu nyingine ambazo itaona inafaa.

Source: wavuti.com - wavuti

Dah!!! Nimeshangaa kuona JF Leo iko silent. juu ya tukio hili. Haya yetu macho ngoma inogile.
 
Rose Kamili anatumiwa. Hana shida kwa sasa; ni mbunge na ameshajijenga. Angemwacha kibabu atengeneze first lady wake bila matatizo. Ina maana Rose....kama Willy akikuomba nanhii utampa? unaona! achana nae bhana
 
Ndoa kati ya Dr Slaa na Rose Kamili ilifungwa wapi, na lini?

Mkuu haya ni masuala ya kisheria hayataki kulazimisha sheria ni taaluma Jaji Laurnce Kaduri ni msomi aliyebobea hawezi kukurupuka kutoa hukumu.
 
Kumbe Mheshimiwa alikuwa akizini miaka yote hiyo. kwani dhehEbu la Mh Dr Slaa linahalalisha uzinzi? hatari hii.
 
Ndio kipaumbele cha Chama Chako, yaani unrest inayoletwa na waislam we haikuusu, ni nani ya kumleta ku-disscus huu ujinga
 
Mmeona mmerikoroga la udini mnataka mponee kwa dk, malizen kwanza hilo mlilolianzisha la udini la sivo hakuna mtu atakae waelewa
 
Dah!!! Nimeshangaa kuona JF Leo iko silent. juu ya tukio hili. Haya yetu macho ngoma inogile.
Mkuu kwani hii habari ni ya uongo? usitake kuziba watu midomo kwa mapenzi yako mkuu.
 
Shehe wa mkoa wa DSM Sheikh Alladi Mussa amesema waislam wanaoandamana ni wahuni na vibaka
 
Back
Top Bottom