PINDA: Serikali yaanda Mkakati, Mafisadi Sasa Kiama

The Khoisan

JF-Expert Member
Jun 5, 2007
15,330
12,898
Mafisadi sasa kiama

2008-07-18 10:02:58
Na Mashaka Mgeta, Dodoma


Serikali inaandaa muswada wa marekebisho ya sheria, ili kuongeza nguvu ya kudhibiti ufisadi unaoshamiri nchini.

Waziri Mkuu, Bw. Mizengo Pinda, alisema hayo jana bungeni mjini hapa, wakati akijibu swali la Mbunge wa Kishapu (CCM), Bw. Fred Mpendazoe, wakati wa maswali ya papo kwa hapo, kutoka kwa wabunge.

Bw. Mpendazoe, alitaka kujua kama serikali haioni umuhimu wa kuchukua hatua za dharura, kuipitia Katiba na sheria ili kuukabili ufisadi, kwa vile unaathiri ustawi wa jamii.

Mbunge huyo, aliuliza swali hilo, huku akirejea katika ibara ya 8(i)(b) inayoelezea lengo la serikali katika ustawi wa wananchi.

Bw. Pinda, alisema suala hilo linafanyiwa kazi, ambapo sheria husika zitapitiwa upya, ili kufikia maamuzi yatakayojenga na kuimarisha misingi ya utawala bora nchini.

Hata hivyo, Bw. Pinda, alisema kuwa na sheria nzuri haitoshi, bali kunahitajika ushiriki wa watu binafsi, hasa viongozi wa umma, kuwa waadilifu.

Alisema ufisadi siyo dhana inayowahusisha matajiri pekee, na kutoa mfano wa kuwepo taarifa za vitendo hivyo katika ngazi ya halmashauri za wilaya nchini.
Awali, Bw. Mpendazoe, alielezea kuwepo wimbi la wafanyabiashara, wanaotumia fedha kuingia katika siasa na baadaye katika uongozi wa serikali.

Bw. Mpendazoe, alikariri sehemu ya hotuba iliyotolewa na Rais Jakaya Kikwete, alipolihutubia Bunge Desemba 30, 2005 na kuzungumzia athari za uongozi unaopatikana kwa njia ya `kununuliwa`.

Pia, Bw. Mpendazoe, alitaka kujua ikiwa serikali ipo tayari kuleta mswada wa sheria ili kuliwezesha Bunge kuteua watendaji wakuu serikalini, ambao hivi sasa wanateuliwa na Rais.

Alisema ushiriki wa Bunge katika uteuzi huo, utakidhi ibara ya 4(2) ya Katiba na kazi ya Serikali ya Muungano na ya Zanzibar itakuwa utekelezaji, wakati Bunge na Baraza la Wawakilishi vitasimamia utekelezaji huo.

Aidha, Bw. Mpendazoe, alisema kwa kuwa Bunge linawajumuisha wawakilishi wa wananchi, kushiriki kwake katika uteuzi huo, kutakidhi ibara ya 8(i)(c) inayozungumzia serikali kuwajibika kwa wananchi.

Bw. Mpendazoe, alitaja baadhi ya watendaji wakuu wanaostahili kuteuliwa na Bunge kuwa ni Wakurugenzi wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), Usalama wa Taifa, Tume ya Haki za Binadamu, Tume ya Maadili ya Viongozi wa Umma na mabalozi.

Akijibu swali hilo, Bw. Pinda, alisema mageuzi hayo yatafanyika ikiwa kutakuwa na mfumo wa kikatiba uliopo sasa.

Hata hivyo, Bw. Pinda alisema kuwa kwa mujibu wa Katiba, Rais ni sehemu ya Bunge, aliyepewa mamlaka ya kusimamia shughuli za Serikali ikiwemo uteuzi wa watendaji hao.

Alisema Bunge linajumuisha wabunge kwa upande mmoja na Rais kwa upande mwingine, hivyo fursa na wajibu wa chombo hicho (Bunge) ni kusimamia utekelezaji wa watendaji wanaoteuliwa na Rais.

Naye Mbunge wa Musoma Mjini (CCM), Vedastus Manyinyi, alitaka kujua msimamo wa Serikali kuhusu madai ya fedha zilizotolewa, maarufu kama `mabilioni ya Kikwete`, kutowafikia walengwa.

Kwa mujibu wa Bw. Manyinyi, fedha hizo zilitolewa katika mpango wa Serikali, kupitia benki za CRDB na NMB, ziliwafikia matajiri na watu wenye uwezo mkubwa kiuchumi badala ya wajasiriamali wadogo waliokuwa walengwa wake.

Akijibu swali hilo, Bw. Pinda, alisema serikali imewaagiza viongozi wa mikoa yote nchini, kuwasilisha taarifa yenye majina ya watu na kiasi walichokopa, ili yachapishwe kwenye kitabu maalum.

Bw. Pinda, alisema kitabu hicho kitasambazwa kwa wabunge ili kuwarahisishia kazi ya kubaini kasoro zilizojitokeza.

Aidha, Bw. Pinda, alisema kiasi cha fedha zilizotengwa katika mpango huo, kilikuwa kidogo ikilinganishwa na mahitaji halisi, hali inayoweza kuwa miongoni mwa sababu za kuibuka kwa malalamiko.

Pia, Bw. Pinda, alisema kuna changamoto inayoikabili Serikali, kuwawezesha wananchi wa Kihadzabe, kuishi kwa kufuata mabadiliko yanayotokea duniani.

Alikuwa akijibu swali la Mbunge wa Iramba Mashariki (CCM), Bw. Mgana Msindai, ambaye pamoja na mambo mengine, alitaka kujua mpango wa serikali kuwapelekea Wahadzabe mahitaji muhimu kama wataalamu wa masuala ya maendeleo.

SOURCE: Nipashe
 
Sheria wakati hawachukui hatua? Wanahitaji sheria gani mpya kuwashughulikia mafisadi wa RICHMOND, EPA, mzee wa vijisenti na wengine?

Pinda naye afadhali akae kimya tu.

Mimi sikutegemea kitu toka kwa Pinda kwa kuangalia utendaji wake kule serikali za mitaa.
 
Hamna jipya tutakaloliona au lisikia hizo zitaendelea kuwa ndoto za alinacha.
 
Yaani Tanzania ni nchi ya ajabu sana

Thats why we have a song to celebrate this...just sing....


Tanzaniaaa Tanzaniaaaa!!
Nakupenda kwa moyo woooteee
Nchi yangu Tanzaniaaaa
Stori zako ni tamuu saanaaa!!
Nilalapo namwaza Vijisentiiii
Niamkapo Mkapa baba weee!
Tanzania Tanzaniaaaa
Nakupenda na EPA zakoooooo
TANZANIA!!!
TANZA NIA


Nchi pekee ambayo Makanisa yanafisha mafisadi kwa shs million 7.6
The only country were footballers plays BUT they dont win!!
The only country with a laboratory to measure witchcraft.
The only country were mzungu comes with one dollars and leaves with millions of dollars!!
The only country were engineers builds but House falls down!!
The only country with Politicians who believes in voo doo!!!
Attorney General!!
The only country were ufisadi is Prestige!!!
The only country with many TUMEz!!
The only country were development is in Figure!!Not visible!!
The only country were politicians are richest men!!
The only country were Language iz a problem!!
AND THE ONLY COUNTRY were PRESIDENT keep on SMILING despite of national difficulties! !!

THE ONLY COUNTRY WITH HANDSOME PREZZIDAAA!! !
I LAV THIS COUNTRY!!
 
Unahitaji kuwa na moyo mgumu kuwaamini hawa watu. Sheria zilizopo zinatosha sana kuwashughulikia wezi wa fedha za umma, tatizo sio kutokuwepo kwa sheria tatizo ni kuwa wanaotakiwa kusimamia utekelezaji wa sheria ndio wakiukaji wakubwa wa sheria. Na serikali kama ya kina Pinda inawaogopa mafisadi, so what do you expect. Huku ni kudanganyana tu.
 
Ni pumba,upupu na kichefu chefu.
Halafu hata hayo wanaosema ni mambo ya serikali ya ccm ambayo utekelezaji wake watakwambia ni baada ya uchaguzi wa 2010.
Usanii tu! Inaonyesha ni kwa kiasi gani hawa viongozi wetu wako out of touch na hata hawajisumbuwi kujaribu kufikiri ni nini hasa mawazo na malalamiko ya wananchi.
Ni maneno amabayo bado yanazidi kumshushia hadhi Pinda moja kwa moja kwani ndiye yeye alisema kuwa Mungu atowe roho yake kama akishindwa kuwashugulikia mafisadi...Lakini ni huyo huyo aliyekuja na suala la Meremeta kuwa la usalama wa Taifa na wala si mafisadi.
Sana sana mafisadi kwao hao wanga ni kina Kubenea na si kina Chenge na RA.
Hatuna viongozi na ni lazima tufanye mageuzi makubwa sana Tanzania la sivyo maendeleo yatakuwa ndoto.
 
Walipokuja na sheria mpya ya Rushwa mwaka jana, The Prevention and Combating of Corrption Act, walisema:

“In terms of updating its corruption law, Tanzania is further down the line than the UK and may be one of the pioneer countries that have gone a long way to domesticate their international obligations under the UN Convention against Corruption.” Edward Hosea, Feb, 2007.

Sasa hizo sheria hazitoshi? Sheria ya PCCA kulikoni tena?
 
Ni msanii mwingine huyu. Hivi mnamsikiliza? Mnamuamini huyu? Mwongo mwingine aliyezaliwa na Kikwete. Ni hawa hawa wameishia kumkamata Kubenea badala ya kukamata Lowasa, Chenge na RA
 
Blaaa blaa blaaa za kila siku izi tushazizoea.............. huu ndio upumbavu wa kufanya kazi kwa mazoea...unaulizwa swali unajibu..miaka inapita hakitelezwi kilichojibiwa na kupigiwa makofi kwenye mabenchi...tofauti na wengine huyu yeye anajibu papo kwa hapo..anaonyesha umahiri zaidi wa porojo..........kwenye ku implementation ni uozo ule ule....hamna kiongozi mwenye uchu wakutaka changes..wanafikiria watajibu nini..sio watafanya nini...useless''!!
 
Mafisadi sasa kiama

2008-07-18 10:02:58
Na Mashaka Mgeta, Dodoma


Serikali inaandaa muswada wa marekebisho ya sheria, ili kuongeza nguvu ya kudhibiti ufisadi unaoshamiri nchini.

Waziri Mkuu, Bw. Mizengo Pinda, alisema hayo jana bungeni mjini hapa, wakati akijibu swali la Mbunge wa Kishapu (CCM), Bw. Fred Mpendazoe, wakati wa maswali ya papo kwa hapo, kutoka kwa wabunge.

Bw. Mpendazoe, alitaka kujua kama serikali haioni umuhimu wa kuchukua hatua za dharura, kuipitia Katiba na sheria ili kuukabili ufisadi, kwa vile unaathiri ustawi wa jamii.

Mbunge huyo, aliuliza swali hilo, huku akirejea katika ibara ya 8(i)(b) inayoelezea lengo la serikali katika ustawi wa wananchi.

Bw. Pinda, alisema suala hilo linafanyiwa kazi, ambapo sheria husika zitapitiwa upya, ili kufikia maamuzi yatakayojenga na kuimarisha misingi ya utawala bora nchini.

Hata hivyo, Bw. Pinda, alisema kuwa na sheria nzuri haitoshi, bali kunahitajika ushiriki wa watu binafsi, hasa viongozi wa umma, kuwa waadilifu.

Alisema ufisadi siyo dhana inayowahusisha matajiri pekee, na kutoa mfano wa kuwepo taarifa za vitendo hivyo katika ngazi ya halmashauri za wilaya nchini.
Awali, Bw. Mpendazoe, alielezea kuwepo wimbi la wafanyabiashara, wanaotumia fedha kuingia katika siasa na baadaye katika uongozi wa serikali.

Bw. Mpendazoe, alikariri sehemu ya hotuba iliyotolewa na Rais Jakaya Kikwete, alipolihutubia Bunge Desemba 30, 2005 na kuzungumzia athari za uongozi unaopatikana kwa njia ya `kununuliwa`.

Pia, Bw. Mpendazoe, alitaka kujua ikiwa serikali ipo tayari kuleta mswada wa sheria ili kuliwezesha Bunge kuteua watendaji wakuu serikalini, ambao hivi sasa wanateuliwa na Rais.

Alisema ushiriki wa Bunge katika uteuzi huo, utakidhi ibara ya 4(2) ya Katiba na kazi ya Serikali ya Muungano na ya Zanzibar itakuwa utekelezaji, wakati Bunge na Baraza la Wawakilishi vitasimamia utekelezaji huo.

Aidha, Bw. Mpendazoe, alisema kwa kuwa Bunge linawajumuisha wawakilishi wa wananchi, kushiriki kwake katika uteuzi huo, kutakidhi ibara ya 8(i)(c) inayozungumzia serikali kuwajibika kwa wananchi.

Bw. Mpendazoe, alitaja baadhi ya watendaji wakuu wanaostahili kuteuliwa na Bunge kuwa ni Wakurugenzi wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), Usalama wa Taifa, Tume ya Haki za Binadamu, Tume ya Maadili ya Viongozi wa Umma na mabalozi.

Akijibu swali hilo, Bw. Pinda, alisema mageuzi hayo yatafanyika ikiwa kutakuwa na mfumo wa kikatiba uliopo sasa.

Hata hivyo, Bw. Pinda alisema kuwa kwa mujibu wa Katiba, Rais ni sehemu ya Bunge, aliyepewa mamlaka ya kusimamia shughuli za Serikali ikiwemo uteuzi wa watendaji hao.

Alisema Bunge linajumuisha wabunge kwa upande mmoja na Rais kwa upande mwingine, hivyo fursa na wajibu wa chombo hicho (Bunge) ni kusimamia utekelezaji wa watendaji wanaoteuliwa na Rais.

Naye Mbunge wa Musoma Mjini (CCM), Vedastus Manyinyi, alitaka kujua msimamo wa Serikali kuhusu madai ya fedha zilizotolewa, maarufu kama `mabilioni ya Kikwete`, kutowafikia walengwa.

Kwa mujibu wa Bw. Manyinyi, fedha hizo zilitolewa katika mpango wa Serikali, kupitia benki za CRDB na NMB, ziliwafikia matajiri na watu wenye uwezo mkubwa kiuchumi badala ya wajasiriamali wadogo waliokuwa walengwa wake.

Akijibu swali hilo, Bw. Pinda, alisema serikali imewaagiza viongozi wa mikoa yote nchini, kuwasilisha taarifa yenye majina ya watu na kiasi walichokopa, ili yachapishwe kwenye kitabu maalum.

Bw. Pinda, alisema kitabu hicho kitasambazwa kwa wabunge ili kuwarahisishia kazi ya kubaini kasoro zilizojitokeza.

Aidha, Bw. Pinda, alisema kiasi cha fedha zilizotengwa katika mpango huo, kilikuwa kidogo ikilinganishwa na mahitaji halisi, hali inayoweza kuwa miongoni mwa sababu za kuibuka kwa malalamiko.

Pia, Bw. Pinda, alisema kuna changamoto inayoikabili Serikali, kuwawezesha wananchi wa Kihadzabe, kuishi kwa kufuata mabadiliko yanayotokea duniani.

Alikuwa akijibu swali la Mbunge wa Iramba Mashariki (CCM), Bw. Mgana Msindai, ambaye pamoja na mambo mengine, alitaka kujua mpango wa serikali kuwapelekea Wahadzabe mahitaji muhimu kama wataalamu wa masuala ya maendeleo.

SOURCE: Nipashe

Labda kama sijaelewa vizuri, yaaani huu mkakati ni kwaaajili ya UFISADI unaoshamiri au na ule ambao ulishakuwepo? Waungwana naomba mwenye kuelewa anielekeze sawa, mimi naona bado haijaka sawa, isije ikawa ndio wanawawekea watu ukuta na kutaka kufunika yaliyokuwepo.
 
Swali la msingi ni je? sheria zilizopo hazina uwezo wa kuwabana mafisadi? let say hao walioiba BOT kupitia EPA sasa wanarudisha fedha walizoiba ni upungufu upi unaotaka kurekebishwa?

Haya masuala ya kila siku TUNAPANGA MKAKATI utekelezaji utakuwa lini? mbona mikakati iliyopo haitekelezwi?
 
huko kujiandaa kunachukua miaka 40? Nyerere na wahujumu uchumi, Alhaji na ufagio wa Chuma, Mkapa na Uwazi, bado tu hawa shiki mtu?
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom