Pinda: Serikali kuunda jopo kuchunguza madai ya katiba mpya

Niliandika hapa kwamba moto kuhusu katiba mpya uliowashwa na CHADEMA hakuna wa kuuzima. Sasa ni kuendelea kuishinikiza Serikali kwamba hatutaki kuongeza viraka kwenye katiba mpya ambavyo vinavyoulizana mwenzangu umekuja lini, bali tunataka katiba mpya ambayo itaendana na hali halisi ya siasa za vyama vingi nchini na pia kuhakikisha katiba hiyo inapatikana kabla ya uchaguzi ujao 2015. Hongera sana CHADEMA juhudi zenu taratibu zinazaa matunda.

Mkuu,

Samahani sana mkuu kama kwa kauli yangu nitakuudhi lakini usifanye issue ya katiba mpya kama issue ya kichama, ni issue ya kila mlalahoi, ya kila mwananchi na kila chama isipokuwa CCM. CHADEMA kama Chadema pekee hawatofika mbali na issue hii.

Wala usiuchukulie ujumbe huu kuamini kuwa nina beef na chadema,, no,no..
Katiba mpya ni kwa manufaa ya umma, si kwa manufaa ya chama kama ilivyo sasa.Na kila anayeipendelea mema nchi hii awe-on board.
 
Lets get down to work, tupendekeze marekibisho!
1. Muundo wa Muungano, Serikali moja au tatu au tuvunje muungano? Serikali mbili ndio ishafeli! haya na tupige kula!
 
Thanks Pinda, umewapatia kweli, ngoja sasa uone watavyoigeuza hiyo.

Mkuu,

Unaelewa kuwa ninyi hamko serious. *trickery!!
Unaelewa kuwa anaturushia changa la macho! Well put, though ila wengi watang’amua,wataelewa hilo.
 
Niliandika hapa kwamba moto kuhusu katiba mpya uliowashwa na CHADEMA hakuna wa kuuzima. Sasa ni kuendelea kuishinikiza Serikali kwamba hatutaki kuongeza viraka kwenye katiba mpya ambavyo vinavyoulizana mwenzangu umekuja lini, bali tunataka katiba mpya ambayo itaendana na hali halisi ya siasa za vyama vingi nchini na pia kuhakikisha katiba hiyo inapatikana kabla ya uchaguzi ujao 2015. Hongera sana CHADEMA juhudi zenu taratibu zinazaa matunda.

BAK,

Masahihisho kidogo, Chadema hawajawasha moto, moto ulishawashwa zamani sana! Walichofanya Chadema ni kununua kidum cha mafuta na kuyamwaga kwenye moto na hivyo kuongeza nguvu ya moto.
 
Ccm wanaweza kuunda mchakato wa kupata katiba mpya wakati , katiba mpya ni kisu cha kuchinja ccm??
Tunaweza kupata katiba mpya yenye haki na huru kupitia serikali ya ccm?
Kwa nini jopo hilo lisihusishe wapinzani au wanataka kupoteza mda kama tume ya nyarali
 
Jamani, CCM inaiteka hoja ya Katiba ambayo kina Mtikila wamekuwa wakiipigia kelele kwa miaka karibu 20 sasa... mtasikia CCM wakiwa mstari wa mbele na kisha Katiba itaundwa au kurekebishwa ili kukidhi matakwa ya Chama tawala na kisingizio kitakuwa matokeo ya kupiga kura!
 
Kama ccm wameng'oa meno ya pccb na kuchakachua matokeo , je wataruhusu katiba mpya ili wang'oke??
 
Sasa yule aliyekurupuka na kusema serikali kwa sasa fedha za kufanya mabadiliko alisema kwa niaba ya nani? ya kwake au ya serikali? kwa maana maelezo yake yalimaanisha hakuna kitu kama hicho kitaendelea, na kwa maelezo haya ina maana serikali is indecisive, na huyu hajatamka kama ana preempt yale maelezo ya awali.


Kwani Pinda kasema fedha ipo?

Pinda simply kawanyamazisha. Kwani mkiambiwa hamsikii, suala la katiba si maslahi ya Chadema ni la waTanzania wote, sasa unataka Serikali wakurupuke tu, kama unavyokurupuka wewe humu?
 
Kumekucha!!! CCM ishaanza dandia hoja ya Katiba baada ya kuhisi fukuto. Wajanja hawa wanamtumia Mtoto wa Mkulima kujaribu kuzima au kupooza move iliyoanzishwa na wapinzani tangu miaka mingi iliyopita na kuhamasishwa na CHADEMA baada ya wizi wa kura uliomweka Madarakani Kikwete. Si kweli serikali haijui ni mabadiliko yepi yafanyike; makubwa au madogo! Ukweli ni kwamba CCM wanabuni mbinu za kujivutavuta hadi 2015 ili waingie uchaguzini na Katiba hii waliyoitunga wao kwa faida yao. Juhudi za kudai Katiba mpya na si "Marekebisho" ya iliyopo ziongezwe vinginevyo tutaishia kuundwa kwa Tume kama ileee ya Mkapa iliyotufanyia kiini macho cha kuongeza mzigo juu ya mzigo.
Wapinzani wa kweli sasa wajipambanue kudai Katiba Mpya, itakayojadiliwa na watanzania wote bila kujali itikadi na napendekeza; ili haki itendeke na ionekane imetendeka vyama pinzani vilivyosajiliwa vyote vitoe wajumbe wawili wawili na vyenye wabunge zaidi ya kumi vichangie wajumbe watano watano na Rasimu ya Katiba hiyo iwekwe wazi kusomwa na watanzania wote kwa kipindi cha mweziau zaidi ili baadae ipigiwe kura ya kuikubali au kuikataa endapo itaonekana kuchakachuliwa. Vinginevyo "Uhuni" uliotendeka wakati wa uchaguzi uliopita utajirudia na matokeo yake yataitesa nchi kwa miaka mingi ijayo. Kama CCM iliweza kutumia "Tume" na vyombo vya Dola ikiwemo Usalama wa Taifa kuchakachua matokeo ya uchaguzi uliopita itashindwaje kufanya hivyo kwa Rasimu ya Katiba Mpya? A Luta Continua
 
Haya tena, mlitaka Serikali iseme nini? Mnafikiri katiba mpya ni kwa maslahi ya Chadema? Kama wazo lenu ni hilo mtakuwa highly disappointed, katiba mpya ni kwa ajili ya Taifa la Tanzania na ni lazima Serikali iwe makini kwa hilo. Wacha jopo liundwe, ikibidi, katiba ianze kuundwa, by the time ikiwa tayari na Chadema itakuwa kama NCCR mageuzi au TLP. Kama unabisha tazama mambo yanavyokwenda.

Kwanza hii ya Pinda leo ni kuwaambia "shut-up"!
 
..........wanajamvini wenzangu, kuna janja ambayo CCM daima wamekuwa wakiitumia kunyakua hoja motomoto kama kilaza Dar-es-salaam alivyomalizia comment yako hapo juu (hii ni 'shut-up'). Nime-note kwamba whenever kuna big issue inayowashika pabaya, utasikia tumeunda tume so nyamazeni subirini matokeo (Mengi Vs Nzoa et al., Richmond, mabomu mbagala etc).

Maadam wao walishasema hawaoni umuhimu wa katiba mpya, waache wanaoona umuhimu wa katiba mpya watengeneze au wa-propose mchakato uende vipi. Kimsingi katiba mpya sio ishu ya kujadili ni lazima....sio ishu ya kufanywa na viongozi wenye mapenzi na uchama bali wenye mapenzi na nchi......
 
Kuna uchaguzi hapa:

a) Serikali kuamua yafanyike mabadiriko makubwa ama madogo
b) Kutumia bunge kushona viraka kwenye katiba (hasa kuichana zaidi na wala siyo viraka)
b) Suala lirudishwe kwa wananchi

Chagua jibu lililo sahihi!

Mheshimiwa Pinda asitupindishe, sisi wananchi ndiyo tuwe chanzo cha katiba hii. Itakuwa ni katiba yetu siyo ya serikali wala bunge. Hilo halina mjadala. Wala suala si kurudisha kwa wananchi ni kuwapa wananchi haki yao ya mda mrefu:

- Serikali ya Tanganyika
- Serikali ya shirikisho (Zanzibar na Tanganyika)
- Kupunguza madaraka ya raisi - leo anaweza kuamua watanzania Bara wote wachapwe viboko, ni kichekesho lakini anaweza kuamua hivo.
- Kuimarisha mfumo wa secular state zaidi kwenye katiba
- Matumizi ya mali asili
- Haki za uraia - raia asipewe haki kwa mkono huu kisha kunyang'anywa kwa mkono mwingine na katiba hiyo hiyo kwa visingizio vya sentensi kama ''ili mradi havunji sheria''
- Uondoaji wa uhai wa mtu
- Mfumo wa kubadilisha serikari (uchaguzi)
- Maeneo ya nchi

na kadhalika
 
Naomba nirudie maneno yangu tena. Chini ya utawala wa CCM hakutakuwa na katiba mpya hiyo ya pinda ni danganya toto tu. watakachofanya ni kuiwekea viraka tu, ili kuwatuliza wananchi. CCM will never dig is own grave.
 
katiba ijumuishe maoni ya watanzania wote si ccm tu plse ccm nawaonya juu la hilo mmetunyima haki yetu muda mrefu sanaaaaaaaaa.
 
Tehe tehe tehehehe....!
Pinda nadhani anajaribu kupindisha wananchi. Sidhani kama tuna haja ama ya kuweka viraka vichache au vingi katika vazi kuukuu. Tunahitaji nguo mpya yenye mtindo utakaodumu kwa muda mrefu. Umakini ni muhimu katika hili. Tusikubali hii iwe hadithi au namna nyingine ya kuwahadaa wananchi. Mapendekezo mengi yalikwishatolewa na wahusika wanayajua vizuri kwa kuwa ni wao waliowatuma kukusanya hayo mapendekezo.
Katiba yetu imekuwa haidumu kwa muda mrefu kwa vile hakuna umakini wa uundwaji wake. Mf tangu uhuru nadhani kuna marekebisho zaidi ya matano na yote hayo hayaleti muafaka zaidi ni migogoro kila kukicha.
Serikali isicheze na akili za watu. Wakati umebadilika sasa. Msiwe watata kwa kusema hamjui marekebisho yanayohitajika kwa sasa e.i makubwa au madogo.
Sidhani Pinda kama amekuja kuchokoza mjadala kama alivyofanya Kombani!
Wananchi mwendo wetu usitulizwe kwa maneno bali matendo.
Ee Mungu bariki fikra zetu nchi yetu kwa maendeleo yakinifu.
 
Ccm wanaweza kuunda mchakato wa kupata katiba mpya wakati , katiba mpya ni kisu cha kuchinja ccm??
Tunaweza kupata katiba mpya yenye haki na huru kupitia serikali ya ccm?
Kwa nini jopo hilo lisihusishe wapinzani au wanataka kupoteza mda kama tume ya nyarali

Katiba ni ya wananchi wote sio ya ccm pekee. Ni ya vyama vyote ni ya watu wote wasiokuwa na vyama na wenye vyama, wafungwa, machangudoa, makaka poa, na majambazi pia.

ccm haina uhalali wa kukaa na kujadili na kuamua kwa niaba ya wananchi 44,000,000 wa Tanzania swala la kama tuwe na katiba mpya au la.
 
Pinda hakuna hoja ya mabadiliko makubwa au madogo, inatakiwa katiba shirikishi ya wananchi na mchakato ufuate mkondo wa wadau wote au sivyo NGUVU YA WATU
 
Hii ni empty promise,
1. hakuna time frame
2.composition ya jopo la wataalam haijulikani itakuwa na watu gani
3. Haijulikani nani atateua kuunda hilo jopo

Hata kama 1-3 vitakuwa kama wananchi wanavyotaka, bado kuna neno limetumika hapo " hata hivyo". Hii inaashiria kuwa , wameshakuwa na doubt hata kabla hata ya jopo hilo kuteuliwa. Ukisoma vizuri utagundua kuwa mabadiliko ya katiba bado ni ndoto serikali bado ina kigugumizi
 
Mkuu,

Samahani sana mkuu kama kwa kauli yangu nitakuudhi lakini usifanye issue ya katiba mpya kama issue ya kichama, ni issue ya kila mlalahoi, ya kila mwananchi na kila chama isipokuwa CCM. CHADEMA kama Chadema pekee hawatofika mbali na issue hii.

Wala usiuchukulie ujumbe huu kuamini kuwa nina beef na chadema,, no,no..
Katiba mpya ni kwa manufaa ya umma, si kwa manufaa ya chama kama ilivyo sasa.Na kila anayeipendelea mema nchi hii awe-on board.

Bila samahani Mkuu. Ni kweli kabisa hili la katiba mpya ni swala linalohusu umma wote wa Watanzania ambao wana mapenzi ya kweli na nchi yetu na si la CHADEMA au CCM tu. na sikutaka kumaanisha kwamba issue hii inaihusu CHADEMA tu. Pamoja na Watanzania wengi kuipigia kelele katina iliyopo na kutaka iundwe katiba hii, safari hii chokochoko hizi za kuishinikiza Serikali kuhusu katiba mpya zilianzishwa rasmi na CHADEMA mara tu baada ya matokeo ya uchaguzi kutangazwa. Hivyo sioni ubaya wowote wa kuipongeza CHADEMA kama waanzilishi wa chokochoko hizi ambazo taratibu zinaanza kuzaa matunda.
 
Back
Top Bottom