nadiriki kusema huyu pinda akapimwe akili..hatuwezi tukawa na pm anaropoka ropoka tu mambo yasiyo na mantiki,yaani yeye kipimo cha matumizi ya pesa na anasa ni kuvaa suti??hivi huyu ana nini?mi ananitia mapka kichefuchefu jamani
PM lazima afikirie umakini unaotakiwa kuzungumzia mambo muhimu katika nchi yetu...muda wa kusema bila ya kutenda umekwisha. ameshasema vitu vingi lakini hakuna utekelezaji maana labda alikuwa anafurahisha baraza tu. kwa mfano tunataka tumwone sasa anayatekeleza yeye mwenyewe kwana...nakumbuka sokoine alikuwa anavaa safari buti na kutembelea landrover 109...hakutowa kauli ila kesho ameamka na kuitekeleza. tatizo wakubwa wetu sasa wanasema mambo kama wanashauri vile kumbe wao ndo wanatakiwa kuyatekeleza kwanz...posho za vikao alizikataza pinda lakini mpaka leo watu wanalipana maboresho...juzi tanesco wamenunua mashangingi...wizara inasema inachunguza...huyu pm kweli anahitaji ushari nasaha.
Breaking news
tafadhali wana jf wa morogoro tupeni habari zilizojiri siku mbili hizi. Kuna taarifa kuwa moto umechoma bweni la shule na kuteketeza wanafunzi watatu. Inaelezwa kuwa ni shule ya walemavu. Miezi miwili haijapita tangu tukio la idodi.
tumeaandika na kusema mara nyingi. Huyu ni pm dhaifu kabisa tanzania kuwa naye. Sasa akibanwa tu. Atalia na kutafuta visingizio chungunzima. Aha! Wakati mwingine tunawaza hivi hawa wazee wakienda asia wanapewa nini? Mwingine alikwenda thailand akarejea na mvua ya mabomu. Kabla hajamkufuru mungu akaondolewa. Huyu naye kaja na kukomesha vazi la suti. Tunakwenda wapi?
tumeaandika na kusema mara nyingi. Huyu ni pm dhaifu kabisa tanzania kuwa naye. Sasa akibanwa tu. Atalia na kutafuta visingizio chungunzima. Aha! Wakati mwingine tunawaza hivi hawa wazee wakienda asia wanapewa nini? Mwingine alikwenda thailand akarejea na mvua ya mabomu. Kabla hajamkufuru mungu akaondolewa. Huyu naye kaja na kukomesha vazi la suti. Tunakwenda wapi?
Mbona wao ndio wa kwanza kuagiza suti toka ulaya na America??Nadhani hapa kila mtu kaja na translation yake kuhusu alichokizungumza PM. Kwa kusema suti ni gharama kubwa mimi nakubaliana nalo kimsingi suti moja inagharimu sio chini ya Tshs 200,000/= sasa kwa maana hiyohiyo kuna viongozi wengi na maafisa wengi waandamizi ambao wanapata allowances kwa ajili ya mavazi na kwa mavazi huwa wanamaanisha suti hizi hela ndio zinaonekana ni gharama kubwa sana na hivyo basi PM anajaribu kuhimiza au kuzuia matumizi makubwa kama haya kwa ajili ya mavazi ambayo hayaleti maendeleo yoyote kwa watanzania.
Mkuu kama ni suti kila mtu ajinunulie kwa kipato chake lakini sio hela za wananchi zitumike kuwapa suti hawa viongozi. Nadhani umefika wakati kila mtu na hasa great thinkers kuwa na uwezo angalau wa kujaribu kutafakari kabla ya kuanza kubonyeza buttons za keyboard. PM mimi nakuunga mkono 100% lakini pia nakuhimza uwaonyeshe Watz mfano na tuone kama hao walio chini yako hawatafuata.... Kudos Pinda!