Chaimaharagwe
Senior Member
- Oct 15, 2014
- 177
- 27
Viko viashiria kuwa huenda Mizengo Pinda akawa Rais wa tano wa jamuhuri ya Muungano wa Tanzania. Pinda ambaye hakuwa na nia hiyo hapo awali, Inasemekana kuwa ameombwa na wazee na vigogo wastaafu waliowahi kushika nyadhifa za juu nchini. Hii inatokana na utulivu wake katika kupanga na kuamua mambo kwa hekima na busara, jambo ambalo linahitajika sana katika kipindi hiki ambacho siasa za dunia na hasa Afrika zinapitia katika wakati mgumu wa vuguvugu la mageuzi. "Hauhitaji mtu anayekurupuka katika kupanga na kuamua mambo wakati huu, Africa imekuwa na maadui wengi sana kutoka nje na ndani ambao wanatumia nafasi ya kuleta machafuko ili kupora rasilimali zetu . Hivyo unahitaji viongozi wenye busara na utulivu katika kuamua mambo. "Alinukuliwa mjumbe mmoja wa halmashauri kuu ya CCM taifa kutoka Mkoa mmoja ulioko kusini.
Kugunduliwa kwa gesi asilia huko Mtwara na tetesi za mafuta katika ukanda wa bahari ya hind kunatajwa kuwa ni moja ya sababu ya taifa kuhitaji mtu wa aina ya Pinda, mkomavu , anayejua vema misingi ya taifa, usalama wa nchi na makini katika kuamua mambo hasa nchi inapokuwa katika changamoto. Mabeberu wanatajwa kunyemelea rasilimali hii ya gesi na mafuta.
Uwezo aliouonesh waziri mkuu Pinda katika kukabiliana na joto la wabunge katika vipindi tofauti umezidi kumjengea sifa na heshima kubwa. Sakata la ESCROW, Operesheni TOKOMEZA na mengineyo ni mifano tosha ya uwezo wa Pinda katika kuhimili mambo mazito. Rais Jakaya Kikwete anatajwa kuridhishwa sana na uwezo wa Pinda kusimamia na kuivusha nchi katika kipindi kizito. Hii imesababishwa na umahiri aliouonesha waziri mkuu nyakati zote za masakata mazito kama TOKOMEZA na hata ESCROW ambapo wakati wote Rais hakuwepo nchini na mambo yalikwenda vema.
Pinda ametumikia ikulu kwa miaka 22, miaka 6 akifanya kazi kama msaidizi wa karibu wa hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere. Hivyo anaijua vizuri nchi. Pinda amejifunza uongozi kwa Mwalimu, Mwinyi na Mkapa akiwa ikulu. Hivyo anaelewa kwa upana uongozi ni nini. Ameanza kulitumikia baraza la mawaziri kabla hajawa waziri. Mwaka 1996 baada ya Rais Benjamin Mkapa kuingia madarakani, Pinda aliteuliwa kuwa afisa msaidi wa baraza la mawaziri, chombo kinachojadili mambo yote mazito ya nchi. Inasemekana mwalimu ndiye aliyeshauri Rais Mkapa afanye kazi kwa karibu na Pinda.
Rais mstaafu Benjamin William Mkapa anatajwa kumuunga mkono waziri Mkuu Mizengo Pinda katika mchakato wa mwakani 2015. Rais mstaafu Mkapa ambaye anatoka sehemu moja (Lindi) na waziri wa mambo ya nje Bernard Membe, anatajwa kutomkubali Membe kwa nafasi ya Urais . Mzee Mkapa aliwahi kusimama hadharani katika harambee kumsifu Pinda kuwa ni mtu makini na kiongozi anayefaa kupewa majukumu makubwa zaidi. Habari zisizo rasmizinasema waziri Membe anatajwa kwenda kuzungumza na Rais Mkapa na kumuomba amuunge mkono katika ndoto yake ya Urais, lakini mzee Mkapa alimwambia wazi kuwa haoni kama anafaa kwa nafasi hiyo. Mkapa alikwenda mbali zaidi kumwambia Membe kuwa yeye Mkapa akiwalinganisha Membe na Pinda kutokana na jinsi anavyowafahamu, anaona Pinda ana sifa kumzidi Membe.
Suala la Ukanda. Ukanda wa Pwani unaojumuisha mikoa ya Tanga, Pwani, Dar es salaam, Lindi na Mtwara inatajwa kutoa Rais mara tatu. RAIS Ali Hassan Mwinyi licha ya kutokea Zanzibar, upande ni mtu wa Mkuranga. Rais Mkapa alitokea Lindi, Rais Jakaya Kikwete kadhalika anatokea Pwani . Hivyo ili kuleta umoja wa kitaifa ni lazima Rais ajaye atoke maeneo mengine ya nchi mbali na Pwani. Hili ni kaa la moto kwa Membe.
Kila nikitafakari kwa kina, simpuuzi Pinda. Namtazama kama mtu ambaye anaweza kufika mbali ya alipo sasa.
Rudisha pesa bhana.......hujaandika ki2 apo!!!