Ni kweli wengi wetu tunashauri Pinda ajiuzulu,lkn pia tunashindwa kutafakari gharama za yeye kuachia hayo madaraka.....kama alivyosema mchangiaji mmoja kuwa tayari Serikali hii ina waziri Mkuu mstaafu sada ikitokea na Pinda naye anaachia hiyo nafasi basi ni aibu kwa hii Serikali,binafsi nadhani Pinda anataka kweli kuachia hayo madaraka kutokana na vigingi anavyokutana navyo anapotaka kufanya kazi yake,lkn kuachia madaraka ya uwaziri Mkuu si jambo dogo na rahisi hasa kama Mh Rais hayupo tayari kukubali hilo jambo.
Pinda amekuwa akiongea kiutu uzima akionyesha kutoridhishwa na wateule wa Rais,lkn afanye nini? tukumbukeni ishu ya Jairo,Pinda alitamani sana kumuondoa yule jamaa madarakani lkn akaishia kulalama tu maana anajua ni mteule wa Rais,sasa hata hili la operation tokomeza majangili naamini angetanani kuwatoa kina Said Mwema na wenzake waliokuwa wanasimamia hiyo zoezi,lkn angeanzia wapi......ni mpk Rais apende......Pamoja na udhaifu wa Pinda lkn udhaifu na uswahiba wa aliye juu na wateule wake unatesa sana,Pinda hataondoka kuficha aibu ya JK,udhaifu Pinda ndio umaarufu wa JK.
Kwa nini usijiuzulu tu tujue moja??viongozi wa kiafrika mbona mnapenda sana kun'gang'ania madaraka??kwanini usitoke hapo madarakani ukabaki kuheshimiwa??huoni kuwa wewe pinda ndio chanzo cha mambo yote yaliyotokea bungeni?????????Nenda mwalimu
Shut up your mouth locust.
Kama vile fisi anavyofuatilia mkono wa binadamu udondoke!