Pinda na mnaoitwa mawaziri mizigo kumbe ukweli huu hapa.

Mwanamume

JF-Expert Member
Jan 3, 2013
262
190
Kwa mfumo wa uundwaji serikali ulivyo sasa, ambapo Rais anateua Waziri mkuu na "kuthibitishwa" na bunge lkn pia anateua mawaziri wengine wote, wakuu wa mikoa na wilaya, wakurugenzi, makatibu wakuu wa wizara, wakuu wa mashirika, wakuu wa vyombo vya ulinzi na usalama, n.k ni vigumu waziri kumuwajibisha mtendaji aliye chini yake. Mfano bungeni Hawa Ghasia katajawa na kamanda Sugu kuwa ana majibu ya jeuri kwa kuwa tu anaelewana na mama Salma. Hii ina tafsiri nyingi sana. Moja ni kwamba Ghasia anajua kwa kuwa karibu na mke wa rais kibarua chake kiko salama zaidi. Hawezi kuwajibishwa hata na Waziri mkuu. Mifano kama hii iko mingi kwa ngazi zote. Ndiyo maana Pinda akasema uwaziri mkuu ni msalaba. Kwa sababu anaongoza mawaziri ambao yy hana mamlaka ya kuwafuta kazi. Waziri naye chini kuna tatizo kama hilo. Kwahiyo tatizo lipo kwenye mfumo.
Kinachofanywa na CC ya CCM ni kucheza karata ya uchaguzi mkuu ujao. Kwa kuwachafua mawaziri na hatimaye kuwavua madaraka ionekane ati CCM nayo inawajibisha. Ni mpango mkakati wa CCM KUJISAFISHA KWA DAMU YA AKINA PINDA. Kwa kusema hivi c kwamba nawaunga mkono mawaziri. Laa! Hasha. Ninachokisema tatizo ni serikali nzima tukianza na rais kwa kuteua mtu eti kisa ni rafiki wa mwanaye, mkwewe, mkewe, n.k
 
Kwa kawaida nchi ikiwa na mfumo wa uraisi (presidential system) kuna kuwa na makamo wa raisi tu hakuna waziri mkuu. Nchi zenye mawaziri wakuu ambao ni heads of government kunakua na raisi au mfalme ceremonial. Sasa huku kwetu raisi ni head of state amd government lakini bado tuna waziri mkuu.
 
Hapa naona umelenga sana serikali ya kishikaji ambalo ni suala lisilowezekana kuizuia kwa sababu kila kitu ndivyo kinavyokwenda kama mm sijulikani na Mh.Rais ,First Lady na au Mwanae au Mkuu wangu wa kazi basi sitaweza kuonekana utendaji wangu na wala sitapewa nafasi .
Kama ni mborongaji basi sitapewa nafasi
 
Wanaume wengine mnatia shaka uanaume wenu, sasa mwanaume na udaku wapi na wapi tena.
Mwaga nondo wanaume wenzio wajue kuna kidume kina data, fact na habari.Bora kukausha some times.
 
Kwa mfumo wa uundwaji serikali ulivyo sasa, ambapo Rais anateua Waziri mkuu na "kuthibitishwa" na bunge lkn pia anateua mawaziri wengine wote, wakuu wa mikoa na wilaya, wakurugenzi, makatibu wakuu wa wizara, wakuu wa mashirika, wakuu wa vyombo vya ulinzi na usalama, n.k ni vigumu waziri kumuwajibisha mtendaji aliye chini yake. Mfano bungeni Hawa Ghasia katajawa na kamanda Sugu kuwa ana majibu ya jeuri kwa kuwa tu anaelewana na mama Salma. Hii ina tafsiri nyingi sana. Moja ni kwamba Ghasia anajua kwa kuwa karibu na mke wa rais kibarua chake kiko salama zaidi. Hawezi kuwajibishwa hata na Waziri mkuu. Mifano kama hii iko mingi kwa ngazi zote. Ndiyo maana Pinda akasema uwaziri mkuu ni msalaba. Kwa sababu anaongoza mawaziri ambao yy hana mamlaka ya kuwafuta kazi. Waziri naye chini kuna tatizo kama hilo. Kwahiyo tatizo lipo kwenye mfumo.
Kinachofanywa na CC ya CCM ni kucheza karata ya uchaguzi mkuu ujao. Kwa kuwachafua mawaziri na hatimaye kuwavua madaraka ionekane ati CCM nayo inawajibisha. Ni mpango mkakati wa CCM KUJISAFISHA KWA DAMU YA AKINA PINDA. Kwa kusema hivi c kwamba nawaunga mkono mawaziri. Laa! Hasha. Ninachokisema tatizo ni serikali nzima tukianza na rais kwa kuteua mtu eti kisa ni rafiki wa mwanaye, mkwewe, mkewe, n.k

Wanachofanya kina Kinana ni kudhoofisha wasiokuwa kwenye mtandao wa uraisi wa Migiro...
 
Hadi Kikwete anatoka IKULU, kila mbunge wa CCM atakuwa amepitia uwaziri/unaibu
 
Back
Top Bottom