amakyasya
JF-Expert Member
- Jun 26, 2013
- 3,480
- 907
Wana JF:
Leo bungeni akijibu swali la papo kwa papo la mheshimiwa Mnyaa aliyeuliza '' Ni lini bunge lilikaa kujadili na kupitisha mshahara na posho za rais kama katiba inavyotaka? Waziri mkuu Pinda alishindwa kujibu na aliishia kusema hajui ni kwa nini hajawahi kuona pia suala hilo likiletwa bungeni japo katiba inataka iwe hivyo. Na pia akasema labda kuna sheria nyingine inayoruhusu lisijadilwe bungeni japo pia hakujua ni sheria gani. Kiujumla majibu yake katika hili yalikuwa ni ya kubahatisha ama kukisia tu bila uhakika wowote.
Je, kama waziri mkuu ambaye ni kiongozi mkuu wa shughuli za serikali bungeni hajui suala nyeti kama hili, inatoa tafsiri gani kwa wananchi wa kawaida?
Leo bungeni akijibu swali la papo kwa papo la mheshimiwa Mnyaa aliyeuliza '' Ni lini bunge lilikaa kujadili na kupitisha mshahara na posho za rais kama katiba inavyotaka? Waziri mkuu Pinda alishindwa kujibu na aliishia kusema hajui ni kwa nini hajawahi kuona pia suala hilo likiletwa bungeni japo katiba inataka iwe hivyo. Na pia akasema labda kuna sheria nyingine inayoruhusu lisijadilwe bungeni japo pia hakujua ni sheria gani. Kiujumla majibu yake katika hili yalikuwa ni ya kubahatisha ama kukisia tu bila uhakika wowote.
Je, kama waziri mkuu ambaye ni kiongozi mkuu wa shughuli za serikali bungeni hajui suala nyeti kama hili, inatoa tafsiri gani kwa wananchi wa kawaida?