Kuna habari nilizozisikia kwenye vyombo vya habari Kuhusiana na mtoto wa mkulima kukataa gari ambalo tayari amenunuliwa! Sitaki kuamini kuwa tokea mchakato wa manunuzi ambao kwa serikalini huchukua muda uanze huyu jamaa hakuwa aware, but ni yeye ambaye kwa kipindi chake kilichopita aliondoa semina na makongamano yote yasiyo na tija, aidha alikataza manunuzi ya magari kwa mwaka wa fedha uliopita isipokuwa magari ya wagonjwa na matreta. Je kama wasaidizi wake ndivyo wanavyomuelewa wanaweza kumnunulia gari kama hilo? Je kama yeye mwenyewe kanunuliwa, hao wasidizi wake wakiwemo mawaziri,makatibu wakuu na wakurugenzi wa wizara hawajanunuliwa? Gari ngapi amezikataa? Hii ni staili ya kiongozi makini au ni kutafuta sifa binafsi? Nani akemee yasinunuliwe kama yeye mwenyewe kaishia kuzira? Wangapi watazira kama alivyofanya yeye kwenye serikali yake? Ni Uzaifu katika uongozi au WOGA? Ni kutokujiamini?