Pinda futa kauli yako kuhusu kuwashughulikia mafisadi

BAK

JF-Expert Member
Feb 11, 2007
124,790
288,007
Posted Date::4/23/2008
Waziri Mkuu Pinda atakiwa kufuta kauli yake kuhusu mafisadi
Na James Magai
Mwananchi

KITUO cha Seria na Haki za Binadamu (LHRC) kimemtaka Waziri Mkuu Mizengo Pinda kufuta kauli yake ya kuwa Serikali inashindwa kuwachukulia hatua za kisheria watuhumiwa wa ufisadi waliojichotea mabilioni ya shiling katika Ankauti ya Malipo ya Madeni ya Nje (EPA), kutokana na utajiri mkubwa walio nao.

Pinda alitoa kauli hiyo hivi karibuni katika mkutano wake ma waandishi wa habari mjini Dodoma, ambapo alisema watuhumiwa hao lazima watakuwa ni matajiri wakubwa na kwamba iwapo watapelekwa mahakamani bila umakini, wanaweza kuitia hasara zaidi serikali kutokanana uwezekano mkubwa wa kuweza kushinda kesi na fedha zisirudi.

Alliongeza kuwa kutokana na hali hiyo njia inayotumiwa na Kamati ya Rais ya kushughulikia suala hilo kuwabana watuhumiwa hao, ili wazirejeshe fedha hizo na zitumike kama ushahidi mahakamani.

Akizungumza na waandishi wa habari jana juu ya ushughukiajia wa masuala ya ufisadi nchini, Mkurugenzi Mtendaji wa LHRC Helen Kijo Bisimba alisema kauli ya Waziri Mkuu, ni aibu kwa taifa kutolewa na kiongozi kama huyo.

Bisimba alisema LHRC na wananchi wote kwa ujumla walikuwa na matumainai makubwa na waziri mkuu huyo kuwa angeweza kushikilia bango kama alivyoahidi katika Mkutano wa Kumi wa Bunge kuwa angeyaafanyia kazi kikamilifu masuala ya ufisadi yanayowahusu watuhumiwa wa kashfa ya Richomond.

"Kauli hii ni aibu kubwa kwa taifa letu na hatukutegemea itoke kwa Waziri Mkuu ambaye ndiye mwenye mamlaka ya juu kiutendaji serikalini," alisema.

Aliongeza kuwa kauli hiyo inakatisha tamaa na inaweza kutafsiriwa kuwa na mwelekeo wa kuweka matabaka ya watu wanaoweza kushitakiwa kirahisi na wasioweza kushtakiwa kutokana na utofauti wa kipato.

Akielezea zaidi athari za kauli hiyo Bisimba alisema serikali inaelekea kuvunja Ibara ya (13) , na ibara ndogo ya (1) ya Katiba ya nchi.

"Kwa mtu yeyote makini akilinganisha maneno ya ibara hii na kauli ya waziri mkuu kuhusun watuhumiwa wafedha za EPA, ataona kuwa Waziri Mkuu anaelekea tusikokutarajia maana anakinzana na katiba yetu," alisema Bisimba.

Alitahadharisha kuwa kauli hiyo isipofutwa, kuna hatari ya kuleta mgawanyiko mkubwa kwa watanzania na hivyo kupoteza dira ya umoja wa kitaifa.
 
Posted Date::4/23/2008
Waziri Mkuu Pinda atakiwa kufuta kauli yake kuhusu mafisadi
Na James Magai
Mwananchi

KITUO cha Seria na Haki za Binadamu (LHRC) kimemtaka Waziri Mkuu Mizengo Pinda kufuta kauli yake ya kuwa Serikali inashindwa kuwachukulia hatua za kisheria watuhumiwa wa ufisadi waliojichotea mabilioni ya shiling katika Ankauti ya Malipo ya Madeni ya Nje (EPA), kutokana na utajiri mkubwa walio nao.

Pinda alitoa kauli hiyo hivi karibuni katika mkutano wake ma waandishi wa habari mjini Dodoma, ambapo alisema watuhumiwa hao lazima watakuwa ni matajiri wakubwa na kwamba iwapo watapelekwa mahakamani bila umakini, wanaweza kuitia hasara zaidi serikali kutokanana uwezekano mkubwa wa kuweza kushinda kesi na fedha zisirudi.

Alliongeza kuwa kutokana na hali hiyo njia inayotumiwa na Kamati ya Rais ya kushughulikia suala hilo kuwabana watuhumiwa hao, ili wazirejeshe fedha hizo na zitumike kama ushahidi mahakamani.

Akizungumza na waandishi wa habari jana juu ya ushughukiajia wa masuala ya ufisadi nchini, Mkurugenzi Mtendaji wa LHRC Helen Kijo Bisimba alisema kauli ya Waziri Mkuu, ni aibu kwa taifa kutolewa na kiongozi kama huyo.

Bisimba alisema LHRC na wananchi wote kwa ujumla walikuwa na matumainai makubwa na waziri mkuu huyo kuwa angeweza kushikilia bango kama alivyoahidi katika Mkutano wa Kumi wa Bunge kuwa angeyaafanyia kazi kikamilifu masuala ya ufisadi yanayowahusu watuhumiwa wa kashfa ya Richomond.

"Kauli hii ni aibu kubwa kwa taifa letu na hatukutegemea itoke kwa Waziri Mkuu ambaye ndiye mwenye mamlaka ya juu kiutendaji serikalini," alisema.

Aliongeza kuwa kauli hiyo inakatisha tamaa na inaweza kutafsiriwa kuwa na mwelekeo wa kuweka matabaka ya watu wanaoweza kushitakiwa kirahisi na wasioweza kushtakiwa kutokana na utofauti wa kipato.

Akielezea zaidi athari za kauli hiyo Bisimba alisema serikali inaelekea kuvunja Ibara ya (13) , na ibara ndogo ya (1) ya Katiba ya nchi.

"Kwa mtu yeyote makini akilinganisha maneno ya ibara hii na kauli ya waziri mkuu kuhusun watuhumiwa wafedha za EPA, ataona kuwa Waziri Mkuu anaelekea tusikokutarajia maana anakinzana na katiba yetu," alisema Bisimba.

Alitahadharisha kuwa kauli hiyo isipofutwa, kuna hatari ya kuleta mgawanyiko mkubwa kwa watanzania na hivyo kupoteza dira ya umoja wa kitaifa.

Huyu Pinda masikini hadi anatia huruma sasa
 
Huyu ameanza kupinda mapema sana naona ataichukia JF mapema zaidi kwani akopeshwi mtu hapa.
 
Huyu Pinda alikuw akaribu sana na Mwl JKN.....namkumbuka bwana Kasori alisema kuwa katika mambo aliyojifunza ni mtu usikurupuke kusema kitu bila kuwa na reference (mamlaka) ya kusupport unachokisema (hakuna cha personnal feelings)...........i.e. kutokana na kifungu x cha mwaka y ...................sheria itachukua mkondo wake.......blah blah

..........lakini huu ujinga wa kusema jamaa hawa ni matajiri sana......oooh mara tutaingia hasara ni ufinyu na uvivu/uzembe wa kutekeleza majukumu uliyoaminiwa kuyatekeleza
 
suala lililopo sio kufuta yale aliyo yasema. kwani hata kama akisema ameyafuta, na utekelezaji utakuwa ni ule ule.wanawaogopa mafisadi na utajiri wao wa dhuluma. sisi tulie tu!!!
macinkus
 
Kama handlers wake mpo hapa mwambieni aje maana kuna darasa kubwa sana anaweza kulitumia.
 
Akizungumza na waandishi wa habari jana juu ya ushughukiajia wa masuala ya ufisadi nchini, Mkurugenzi Mtendaji wa LHRC Helen Kijo Bisimba alisema kauli ya Waziri Mkuu, ni aibu kwa taifa kutolewa na kiongozi kama huyo.

Bisimba alisema LHRC na wananchi wote kwa ujumla walikuwa na matumainai makubwa na waziri mkuu huyo kuwa angeweza kushikilia bango kama alivyoahidi katika Mkutano wa Kumi wa Bunge kuwa angeyaafanyia kazi kikamilifu masuala ya ufisadi yanayowahusu watuhumiwa wa kashfa ya Richomond.

"Kauli hii ni aibu kubwa kwa taifa letu na hatukutegemea itoke kwa Waziri Mkuu ambaye ndiye mwenye mamlaka ya juu kiutendaji serikalini," alisema.

Aliongeza kuwa kauli hiyo inakatisha tamaa na inaweza kutafsiriwa kuwa na mwelekeo wa kuweka matabaka ya watu wanaoweza kushitakiwa kirahisi na wasioweza kushtakiwa kutokana na utofauti wa kipato.

Akielezea zaidi athari za kauli hiyo Bisimba alisema serikali inaelekea kuvunja Ibara ya (13) , na ibara ndogo ya (1) ya Katiba ya nchi.

"Kwa mtu yeyote makini akilinganisha maneno ya ibara hii na kauli ya waziri mkuu kuhusun watuhumiwa wafedha za EPA, ataona kuwa Waziri Mkuu anaelekea tusikokutarajia maana anakinzana na katiba yetu," alisema Bisimba.

Alitahadharisha kuwa kauli hiyo isipofutwa, kuna hatari ya kuleta mgawanyiko mkubwa kwa watanzania na hivyo kupoteza dira ya umoja wa kitaifa.

Huyu mama yuko juu!
I really admire the way she express herself and especially what she choose to speak or not to speak about.
I envy you Bi Helen Kijo Bisimba.
 
Nina wasiwasi kwamba Kikwete aidha yuko peke yake au naye ni fisi mdogo na anonekana kama mbwa kumbe sivyo. Hawa watu wanatuchezea niwazi kwamba utafika wakati wabongo tukatae kuwa kama watoto kudanganywa kwa pipi ili tunyamaze kulia.

Hivi kweli JK ana nia anayosema? napata wasiwasi mwanzenu, nisaidieni maana nakata tamaa

Hiyo ni geresha tu na danganya toto ya akina 'Ze Comedy'. Nani kakuambia hawakujua yote yanayoonekana kuibuliwa sasa, walijua shukuru Mungu walau JK ametupa uhuru wa kujieleza siyo kama alivyokuwa Chinga.

Wakati ukifika tutachukua nchi kwa maandamano,wanadhani wameumbwa ili kutwala kumbe Mungu kawapa dhamana ambayo wanashindwa kuitumia na kuwa mawakili wema.
MUNGU SAIDIA TANZANIA NA WOTE WENYE NIA NJEMA.
 
nayo hiyo tume ya haki ya binaadamu ilikuwa imelala muda mrefu acha iamke.
haki za binaadamu zinavunjwa kila dakika tanzania, wao wamelala tu
na waende UDSM, Kwenye Migodi, kote kunasubiri input yao
 
Sijui tumelaaniwa... Yaani watuibie halafu tuwaogope kwa sababu wametuibia...ama kweli wajinga ndio waliwao..ndio maana wanatuchimba mikwara kuwa hata mahakamani tuwapeleke (DY) tupambane huko huko ????
 
Back
Top Bottom