Pinda: ehe tee ha hiyo ni gelesha tu ..

Mwanamayu

JF-Expert Member
May 7, 2010
11,349
6,476
Kama wabunge wa Chadema wamegelesha kwa kutoka kwao nje ya Bunge kwa nini yafuatayo yalimkuta JK:

1. Kupigwa na butwaa na kubaki mdomo wazi,

2. hotuba nzima imejaa kukosea maneno ambayo ni ishara ya ku-panic,

3. JK kujikuta akihutubia bila wawakilishi wa sehemu kubwa ya jiji la Mbeya, Mwanza, DSM, pia miji mikubwa kama Arusha na Kilimanjaro - Hotuba kwa CCM, CCM B, CCM C na CCM D bila wapinzani,

4. JK: watatoka watarudi - maana yake ni kuwa hawatakaa pamoja na ndio lengo la Chadema,

5. JK: watafuta tu huduma serikalini - Chadema watafuata kodi inayotolewa na mimi na wewe tunaolipa kodi ili kuendesha pia vyama vya siasa

Pia inakuwaje gelesha wakati ni mwendelezo wa matukio ya Chadema kutokuudhuria hafla zenu kuanzia kutangazwa matokeo, kuapishwa kwa JK, kuapishwa kwa Pinda mwenyewe, hafla fupi ya jana jioni Ikulu ndogo pale Chamwino.

Kwa kifupi: kama waliotoka nje wamegelesha basi hata waliobaki ndani walikuwa wanagelesha kwamba haijawa-touch!!!!!!!!!
 
Dr. Slaa alisema atakwenda mahakamani, mboni kimyaa, tunataka tuone sheria zikimiminwa kute kwenye jengo la haki, asichelewe sana keki inapoa atiii!!:yield:
 
Back
Top Bottom