Waziri Mkuu Pinda asitisha utekelezaji wa agizo la Magufuli la Bomoa bomoa

Jatropha nimekuelewa vizuri lakini kama na wewe umenielewa ugomvi wangu ni kwa waziri mkuu kutamka hivyo hadharani, haoni kwamba hata wale ambao walisitisha ujenzi maeneo husika wataendelea kwa kuwa wameruhusiwa kufanya hivyo.

Na kitu kiinge angemwita ofisini amweleze bwana hili unalofanya litatugharimu, ili wananchi tubaki tunajua kwamba kujenga kwenye hifadhi ya barabara ni kosa, lakini walojenga kwa hizo sheria za zamani wasibomolewe.

Halafu naamini Magufuli sio mbumbumbu wa sheria kiasi hiki, nadhani anafahamu anachokifanya, incidencies za makosa zipo unapotekeleza majukumu yako. Mimi nadhani Magufuli aendelee kusimamia sheria hata kama waathirika wa usimamizi wake wataendelea kumpinga akiwemo PM Pinda.

Ugomvi wangu siyo kusitisha ubomoaji bali ni nani alistahili kutoa tamko la kusitisha. Na kama ilikuwa ni lazima kwa yeye kutoa tamko, basi alipaswa kutumia lugha ya kistaarabu kulinda heshima waziri wake Pombe Magufuli. Kuna mchangiaji anasema Pinda angeweza hata kutumia maneno kama 'nitakaa niongee na waziri magufuli ili tuone namna bora ya kutekeleza zoezi hili'. Lakini tatizo la viongozi wa nchi hii kila mtu anataka ajitutumue mbele ya wananchi kwamba ana mamlaka. Kazi kwelikweli!
 
Huku kusitishwa hakuna uhusiano na hali ya sasa ya siasa kweli?
Isitoshe alivyotoa hiyo kauli alikusudia kumaanisha nini?
Kwamba hawatabomoa tena au wanadanganya wananchi, wakishatulia waje kubomoa anyway?
Kwa nini kauli ya usitishwaji imetolewa na Pinda wakati ya utekelezaji ilitolewa na Magufuli?
Hapa hakuna kuingilia majukumu ya watu kweli?
Ila kama Magufuli anahisi kudhalilishwa namshauri ajiuzulu, atajijengea heshima zaidi... Aachane na siasa za Kinafki za akina Pinda.
 
Wazee nimesikia kwenye taarifa ya habari usiku huu kupitia RFA kwamba Waziri Mkuu Mizengo Pinda amesitisha ubomoaji wa majengo yaliyojengwa ndani ya hifadhi ya barabara nchini kote. Najua ubomoaji huo ulikuwa unafanywa kwa amri ya Mhe. Pombe Magufuli. Hii amri ya Pinda, imekaaje wazee? Au ndiyo mwendelezo wa tabia ile ile ya serikali yetu ya sasa ambapo kila kiongozi anafanya kazi na kutoa statements kadri anavyojisikia? Mhe. Magufuli atajisikiaje?
Kamuulize ngeleja alijickiaje aliposema kuwa selikali itailipa dowans, ndo zao ccm kucgana kupingana kila m2 anaongea jinsi anvojua/ona they have no one setting :blah::blah::blah::blah::blah::blah:
 
Kweli kabisa mkuuu inatia uchungu eti viongozi wanaona suluhisho ni kudhibiti cdm na wa2 wanaunga mkono, hovyoooooooooooooooooooooooooooooooooo!
 
Wadau juzi tarehe 5/3/2011 mbunge wa jimbo la Ubungo John Mnyika alifanya ziara jimboni kwake na kuzungumza na wananchi waishio kandokando ya Barabara ya Morogoro,kuhusu kuvunjiwa nyumba zao na hatma ya malipo yao.Walikubaliana na wakazi waishio pembezoni mwa barabara ya morogoro kuwa mapema siku hiyohiyo kumpelekea azma Waziri mkuu Pinda amwamuru Waziri wa Ujenzi Magufuli asitishe zoezi la bomoa bomoa,Nimetahamaki Leo Asubuhi Nasikia kuwa Magufuli Kaamrishwa asimamishe Zoezi la bomoa bomoa.Jamani Hv Nyie Chadema Kwani Nyie ndo wenye Nchi?Mbona kila kulicha matamko yenu ndo yanafuatwa kila siku?

ni chama kikuu cha upinzani kinachomjali mwananchi wa kawaida, chama ambacho kinatishia uwepo na ustawi wa mafisani nchini, chama kinachoungwa mkono na kila kundi. PEOPLE'S POWER

 
Hapo sikubaliani na mnyika! na PINDA wake wangemwaacha Magufuli afanye kazi yake but kwa hivyo wanaailisha matatizo tuuu!
 
Mnyika safi kizuri kula na nduguzo kwa hiyo wanaubungo ni ndunguzo watetee unavyoweza kaka. Then kama utapata ujumbe huu utusikilize.
 
Hapo sikubaliani na mnyika! na PINDA wake wangemwaacha Magufuli afanye kazi yake but kwa hivyo wanaailisha matatizo tuuu!

Tatizo mkuu ni kwamba hata haao wanaobomolewa hawalipwi pesa za kutosha, hapo ndio kwenye tatizo.
Maana mtu unapata pesa huwezi hata ukajenga nyumba kama uliyobomolewa.
Ndio maana wananchi wanakuwa na chuki.
 
ugomvi wangu siyo kusitisha ubomoaji bali ni nani alistahili kutoa tamko la kusitisha. Na kama ilikuwa ni lazima kwa yeye kutoa tamko, basi alipaswa kutumia lugha ya kistaarabu kulinda heshima waziri wake pombe magufuli. Kuna mchangiaji anasema pinda angeweza hata kutumia maneno kama 'nitakaa niongee na waziri magufuli ili tuone namna bora ya kutekeleza zoezi hili'. Lakini tatizo la viongozi wa nchi hii kila mtu anataka ajitutumue mbele ya wananchi kwamba ana mamlaka. Kazi kwelikweli!
hvi ulimuona kwenye magufuli tv wakati akisema kuwa "kama halamshauri zinataka kuweka mabango katika barabara zao waweke hata katikati ya barabara" alikuwa akifoaka kama mbogo usingeweza kujua kama huyu ni kiongozi mwanadamizi wa serikali. Angetumia maneno kama unayoshauri kutumika akina nani wiki hii huyu chizi angebomoa nyumba za watu halafu serikali ije kuamualiwa na mahakama kulipa fidia. Ilitakiwa kutumia strong worded statement kwa kuwa magufuli alionyesha dharau kutokea mwanzo kwa kutoshirikisha wizara, moa. Wilaya, manspaa n.k
 
Pinda asitisha bomoabomoa

Monday, 07 March 2011 07:54 newsroom


*Asema kasi ya Magufuli inatisha
* Muafaka sasa kupatikana bungeni
NA Angela Sebastian,Chato
WAZIRI Mkuu Mizengo Pinda, amemwagiza Waziri wa Ujenzi, Dk.John Magufuli, kusitisha mara moja operesheni bomoabomoa inayoendelea nchini hadi serikali itakapotafakari upya suala hilo. Alitoa agizo hilo jana katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika viwanja vya shule ya msingi Chato, mkoani Kagera.
pinda.jpg

Waziri Mkuu alisema uamuzi huo unatokana na malalamiko mengi yanayotolewa na wananchi ikiwemo kutopewa elimu ya kutosha juu ya operesheni hiyo.
Kutokana na hilo, alisema iwapo operesheni itaendelea, ni wazi itaibua migogoro isiyokuwa ya lazima.
Operesheni hiyo imekuwa ikiendelea katika maeneo mbalimbali nchini, kwa ajili ya kupisha ujenzi wa miundombinu ikiwemo ya barabara.
Katika utekelezaji wa operesheni hiyo, nyumba na maendeleo mengine ikiwemo vibanda vya biashara ambavyo vimejengwa ndani ya hifadhi ya barabara vimekuwa vikibomolewa.
"Magufuli akishaagiza, meneja wa TANROADS jasho linamtoka na kuanza kubomoa... hatuendi hivyo. Ukitizama X wanalolibandika linakera," alisema Waziri Mkuu
Alisema kasi ya waziri Magufuli katika kutekeleza operesheni hiyo ni kali, na husababisha watendaji wa TANROADS wakilalamikiwa na wenyewe kushindwa kuweka bayana kwa waziri husika.
Kutokana na hilo, alisema suala hilo linarudishwa serikalini ili Baraza la Mawaziri likae na kulitafutia ufumbuzi na baadaye liwasilishwe bungeni kujadiliwa na muafaka kufikiwa.

Baadhi ya wananchi waliokuwa kwenye mkutano huo, waliipokea kauli hiyo kwa furaha huku wakisema serikali imesikia kilio chao.
Ayoub Musa, ambaye ni mkazi wa Chato, alisema serikali imekuwa ikisemamaeneo fulani ni hifadhi ya barabara, lakini katika maeneo hayo hakuna alama inayoonyesha ni hifadhi, jambo ambalo limekuwa likiwachanganya.
Mbali na hilo, alisema wananchi wengi hawajawahi kupewa elimu juu ya hifadhi za barabara, bali husikia kwenye vyombo vya habari operesheni bomoabomoa inapofika eneo lao.
Mkazi mwingine ambaye hakutaka jina lake liandikwe gazetini, alisema serikali imesikia kilio chao na kwamba elimu itolewe kwa watendaji na wenyeviti wa mitaa na vijiji, ili waweze kuwaelimisha wananchi.
My take
Juzi juzi tulishuudia minyukano katika baraza la mawaziri, wateule wa jk wakitoa matamko kila moja kivyake na mbaya zaidi misimamo ikiwa imetofautiana. Mawaziri hawo ni Ngeleja (ufisadi), sitta na mwakyembe walitoa misimamo yao ambayo ilitikisa serikali juu ya hujuma za dowans kwa wananchi. Kabala ya hata miezi miwili kupita tunasikia mtoto wa mkulima aka Pinda akimvua nguo Makufuli kuwa ana spidi kali na anaweza kuwamwangia unga. Je hii ni serikali au kundi la wabaka uchumi?
 
Hii serkali bwana!!!!!!!!!! mmmmmh haya. Maagizo yanatolewa barabarani. Kwanini asimuite ofisini kwake akampa maagizo ya kusitisha zoezi hilo? Halafu amwachie yeye mwenyewe atangaze? Anataka kuonekana anawapenda sana wananchi? HAWADANGANYIKI SIKU HIZI
 
Hii serkali bwana!!!!!!!!!! mmmmmh haya. Maagizo yanatolewa barabarani. Kwanini asimuite ofisini kwake akampa maagizo ya kusitisha zoezi hilo? Halafu amwachie yeye mwenyewe atangaze? Anataka kuonekana anawapenda sana wananchi? HAWADANGANYIKI SIKU HIZI

Watu wana roho mbaya sana na wanafurahi wakiona wenzao wanateseka kwa kukosa hata chakula. Lakini mara wapatapo mwanya wa kusafisha jina wako tayari kuwatoa wenzao kafara
 
Hapo Magufuli kesha vunjwa moyo na kwa kifupi amedhalilishwa mbele ya Tanroads na mbele ya wapiga kura wake. Unadhani hata mbeleni atakapotoa maagizo, si watamwambia subiri kwanza waziri mkuu akubali. Politics bana!!!!
 
serikali inaposhindwa kufuata sheria zake iliyojiwekea ni hatari sana.
 
hii serkali bwana!!!!!!!!!! Mmmmmh haya. Maagizo yanatolewa barabarani. Kwanini asimuite ofisini kwake akampa maagizo ya kusitisha zoezi hilo? Halafu amwachie yeye mwenyewe atangaze? Anataka kuonekana anawapenda sana wananchi? hawadanganyiki siku hizi

ametoa maagizo kwa staili ile ile magufuli aliyotoa maagizo yake kwa mameneja wa tanroads. La sivyo nyumba za waannchi zingebomolewa bure
 
Hapo Magufuli kesha vunjwa moyo na kwa kifupi amedhalilishwa mbele ya Tanroads na mbele ya wapiga kura wake. Unadhani hata mbeleni atakapotoa maagizo, si watamwambia subiri kwanza waziri mkuu akubali. Politics bana!!!!


Makufuli akili zake bwana, sijui hana darubini za kuona kesho..

Yeye hajioni ni targeti ya wajanja kumwondolea imani ya wananchi juu yake ili wabaki wao. teh teh teh.

Magufuli ni kama Raila tu wa Kenya.
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom