Pinda aomba msaada kukabili mafisadi

BAK

JF-Expert Member
Feb 11, 2007
124,792
287,994
Washughulikie kwanza waliokwishajulikana badala ya kudai wakikamatwa nchi italipuka

Posted Date::5/28/2008
Pinda aomba msaada kukabili mafisadi

Na Kizitto Noya
Mwananchi

SERIKALI imeiomba jamii kuipa ushirikiano kuwabaini wala rushwa na wahujumu uchumi, kwa kuwa wamekuwa kikwazo cha maendeleo nchini.

Waziri Mkuu Mizengo Pinda alisema jana jijini Dar es Salaam kuwa pamoja na uchumi wa nchi kukua kwa kiwango kikubwa katika miaka ya hivi karibuni, ufisadi umekuwa ukihujumu uchumi na kuongeza kiwango cha umaskini nchini.

Pinda alisema hayo wakati akifungua Jukwaa la Nne la Sekta ya Nishati, lililoandaliwa na Shirikisho la Wenye Viwanda Nchini (CTI) kwa kushirikiana na Taasisi ya Sekta Binafsi (TPSF) na kufanyika jijini Dar es Salaam.

Alisema tangu kuanzishwa kwa sera ya Urekebishaji na Ubinafsishaji wa Mashirika ya Umma na Mageuzi ya Kiuchumi yaliyoruhusu mfumo wa soko huria, mapato ya serikali yameongezeka kutoka Sh25bilioni kwa mwezi mwaka 1995 hadi Sh280 bilioni kwa mwezi mwaka huu.

Alisema pia thamani ya uuzaji wa bidhaa nchi za nje imeongezeka kutoka dola za Marekani 851.3milioni mwaka 2001, hadi dola 3.5 bilioni mwaka jana. Kwa mujibu wa Pinda pamoja na ongezeko hilo uchumi wa Tanzania unahujumiwa rushwa na wizi wa rasilimali za umma vinavyofanywa na baadhi ya watendaji wa serikali na wananchi wa kawaida.

Wito wangu kwa wananchi wote wakiwemo wafanyakazi wa Shirika la Umeme Nchini (tanesco), ni kushirikiana na serikali kubaini wahalifu ambao wamekuwa wakisababisha hasara kubwa.

Serikali itachukua hatua kali za kisheria kupambana na wote wataopatikanma wakihujumu miundombinu muhimu,?alisema Pinda. Waziri Pinda aliwataka wafanyabiashara nchini kuwekeza katika uzalishaji wa umeme ili kukabiliana na tatizo la upatikana wa nishati hiyo kwa kuwa na vyanzo mbadala.

Alisema kwa upande wake, serikali inayafanyia kazi mapendekezo ya wadau, kuhusu kuigawa Tanesco ili liwe na kampuni tatu zitakazojitegemea, pamoja na kuanzisha mamlaka za kusimamia biashara katika sekta ya nisahti na maji mijini na vijijni.
 
Hatua ya kwanza mwambieni awe anakuja hapa kupata issues kama hajajua bado.

Wananchi wapo na wanakata issues hapa.
 
Hivi ukimtukana PM si unaweza kupelekwa Keko? Huyu jamaa naye anaweza kuishia kutukanwa. Wamepewa majina na Dr. Slaa, wameshindwa kuchukua hatua mpaka wengine wanakufa/wanatoroka bila kuhojiwa.

Anataka wananchi tumsaidie nini tena?
 
Huyu PM hajui kuwa yeye si mwanasiasa ni mtendaji. Mkuu wa SIRIKALI..tena kwa action tupu si longo longo...ila navyomuona taratibu anakuwa mwanasiasa kabisa wa kuomba kura zetu kw ahadi kila kijiji..............ahahaha...kwa "ANGUKA"na ukute anavimba kichwa sababu ameshaambiwa......ni chaguo la JK kumrithi...ukute nae anachekelea chinix2
 
Hivi ukimtukana PM si unaweza kupelekwa Keko? Huyu jamaa naye anaweza kuishia kutukanwa. Wamepewa majina na Dr. Slaa, wameshindwa kuchukua hatua mpaka wengine wanakufa/wanatoroka bila kuhojiwa.

Anataka wananchi tumsaidie nini tena?

Mtukane kimoyo moyo tu, ila kusema kweli hapo amechemsha na hiyo kauli yake.
 
Kama Pinda anakubali kwamba kuna ufisadi, mbona Kikwete na mouthpieces wake Rweyemamu na Simba wanaongea kama vile ni sisi hatuna dogo?

Kikwete kasema Viongozi wasiogope kuitwa Mafisadi. Rweyemamu jana ka imply waandishi wameikomalia ishu ya Ballali, ishu ya kifisadi.

Kwa hiyo kwanza watuambie kwa sauti moja. Wanakubali nchi inanuka ufisadi au ni sisi hatuna dogo?
 
SERIKALI imeiomba jamii kuipa ushirikiano kuwabaini wala rushwa na wahujumu uchumi, kwa kuwa wamekuwa kikwazo cha maendeleo nchini.
Huyu pinda anataka ushirikiano gani tena? Pinda anza na ripoti ya EPA. majina unayo. mnasubiri nini kuwakamata hawa jamaa? ripoti ya mkaguzi na mdhibiti mkuu wa mahesabu ya serikali imejaa madudu. unasubiri nini kushughulika? what are you waiting for mr Prime Minister? mnasubiri hadi wote waliotajwa kwenye kashfa ya EPA wafe? Stop making these empty slogans which are not directed at anybody ' eti unaiomba jamii'?
 

Alisema kwa upande wake, serikali inayafanyia kazi mapendekezo ya wadau, kuhusu kuigawa Tanesco ili liwe na kampuni tatu zitakazojitegemea, pamoja na kuanzisha mamlaka za kusimamia biashara katika sekta ya nisahti na maji mijini na vijijni.[/size][/color]

Nadhani Pinda alikusudia kusema haya sasa alikuwa anatafuta gear ya kupandia kufikia hapa. Jamani Tanesco mbona imekuwa kama mpira wa kona kwenda golini? kila mmoja anajaribu kuupiga ili aone kama atafunga goli.
 
Kwanza atusaidie kuwapeleka keko EL na wenzie ambao tuna ushahidi wao mkononi. Naye siku hizi naona kapinda na anaturudisha kwenye enzi zilezile za maneno bila matendo. Kila leo wananchi tunaombwa tusaidie bila hatua kuchukuliwa sasa wacha sisi tushughulike kivyetu na tuone jinsi tunavyoweza kuwashughulikia hawa mafisadi. Subiri tu ilo siku watajua kuwa Umma wa watizedi umekasirika.
 
Washughulikie kwanza waliokwishajulikana badala ya kudai wakikamatwa nchi italipuka

Posted Date::5/28/2008
Pinda aomba msaada kukabili mafisadi

Na Kizitto Noya
Mwananchi

SERIKALI imeiomba jamii kuipa ushirikiano kuwabaini wala rushwa na wahujumu uchumi, kwa kuwa wamekuwa kikwazo cha maendeleo nchini.

Waziri Mkuu Mizengo Pinda alisema jana jijini Dar es Salaam kuwa pamoja na uchumi wa nchi kukua kwa kiwango kikubwa katika miaka ya hivi karibuni, ufisadi umekuwa ukihujumu uchumi na kuongeza kiwango cha umaskini nchini.

Wito wangu kwa wananchi wote wakiwemo wafanyakazi wa Shirika la Umeme Nchini (tanesco), ni kushirikiana na serikali kubaini wahalifu ambao wamekuwa wakisababisha hasara kubwa.

Serikali itachukua hatua kali za kisheria kupambana na wote wataopatikanma wakihujumu miundombinu muhimu,?alisema Pinda.

Hivi nikuulize Pinda.....Unaongea hayo kuwadhihaka wananchi?

Hivi unajiangalia kwenye kioo na kuangalia maneno unayokwenda kuongea mbele ya kadamnasi ya watu?

Yaani jamani kweli nchi hii inaenda wapi ikiwa mawaziri wanaongea utumbo na sasa mpaka hata Mzee Pinda tulitegemea utakuja Nyooka kumbe umeng'ang'ana ku Pinda kama wenzio....sasa tukimbilie wapi sisi wanyonge?...hio hotuba yako naelewa kuwa una uchungu tu na wale petty fisadis lakini wale big EL Fisadi ni immune kwa sheria yetu ya CCM....Mungu Ibariki Tanzania
 
Dahh, yaani sina hamu,..............

Mi nilifikiri Pinda ungetakiwa utushukuru wananchi kwa ushirikiano tuliouonyesha (atleast that acknowledgement.....), then ungetuomba TUENDELEE KUTOA USHIRIKIANO.......however, tunataka kuona matokeo ya ushirikiano wetu kwanza tokea kwa Dr.Slaa hadi kwa Dr.Mwakyembe........hatutaki kusubiri mpaka watu wafe!!
 
Hivi karibuni kuna kiongozi wetu mmoja mzito, aliniomba nimpe mawazo yangu kuhusu PM wetu, nikamwambia kuwa mkuu mbona anaongea sana, akasema kijana kama vile ulikuwa kichwani mwangu, nitamuomba mkuu mmoja wa nchi zaidi yangu amuambie hilo kwa siri na busara sana ili asikasirike,

I hope atamfikishia hilo soon, I mean it about time mkuu akanyamaza sasa!
 
Cha muhimu ni kumuambia kuwa Wananchi tumezila, Kama anataka majina atayajua tutakapo wazomea na wale tutakao watosa 2010
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom