bwegebwege
JF-Expert Member
- Jul 30, 2010
- 1,071
- 185
Miaka kadhaa iliyopita serikali ya CCM iliaamua kuhamishia Makao Makuu ya Serikali Kutoka DAR ES SALAAM na kuhamia DODOMA! Uamuzi huo ulifuatwa na hataua za utekelezaji, ikiwemo kujenga Ofisi za Bunge (mhimili mmoja wapo wa Serikali) na pia kuamuru baadhi ya Wizara kuhamishia shughuli zake mjini Dodoma.Kati ya ofsi nyeti zilizohamishiwa kule ni OFISI YA WAZIRI MKUU!!
PM, ambaye kwa sasa ni PINDA (sijawahi kumsikia akilizungumzia hili hata kidogo) alijengewa Nyumba ya kuishi pamoja na Ofisi. Serikali ya Awamu ya Tatu na hii ya Mh. J Kikwete ziliahidi kwamba zitahaklikisha Serikali inahamia DODOMA!!
Leo bado Waziri Mkuu yupo Oyster Bay, ofisi yake ipo pale Magogoni jirani na president! Kule Dodoma kuna Makazi na ofisi, na nina hakika kuna watendaji/watumishi wako kule na serikali inawalipa mshahara, posho, achilia mbali magari na kadhalika!! Naamini pia baadhi ya Wizara zina watendaji kule .
Swali: Kama tumeshindwa kwenda Dodoma, kuna haja gani serikali kupoteza fedha nyingi kuendesha hizi ofisi na makazi kule?? Kuna haja gani kwa PM kuwa na ofisi na makazi katika sehemu mbili tofauti wakati zaidi ya 90% ya muda wake anakuwa Dar es Salaam?? Serikali haioni kwamba mpango wa kuhamia Dodoma UMESHINDIKANA?
Siku za karibuni watu wengi wamechangia threads za ukosefu wa uwezo wa ndugu yetu PINDA. Leo nimelikumbuka hili, Nawasilisha na nitawashukuru wabunge wenye mapenzi ya kweli ya nchii hii kuishinikiza serikali kuamua kusuka ama kunyoa. KAMA TUNAKWENDA DODOMA BASI TWENDE MARA MOJA, KAMA HAIWEZEKANI BASI TUENDELEE KULA UPEPO WA PWANI DAR, LAKINI TUISELEKEZE HELA KULE DODOMA AMBAKO HATUNA MUDA NAPO, HUU NI UFUJAJI WA FEDHA ZA SERIKALI!!
PM, ambaye kwa sasa ni PINDA (sijawahi kumsikia akilizungumzia hili hata kidogo) alijengewa Nyumba ya kuishi pamoja na Ofisi. Serikali ya Awamu ya Tatu na hii ya Mh. J Kikwete ziliahidi kwamba zitahaklikisha Serikali inahamia DODOMA!!
Leo bado Waziri Mkuu yupo Oyster Bay, ofisi yake ipo pale Magogoni jirani na president! Kule Dodoma kuna Makazi na ofisi, na nina hakika kuna watendaji/watumishi wako kule na serikali inawalipa mshahara, posho, achilia mbali magari na kadhalika!! Naamini pia baadhi ya Wizara zina watendaji kule .
Swali: Kama tumeshindwa kwenda Dodoma, kuna haja gani serikali kupoteza fedha nyingi kuendesha hizi ofisi na makazi kule?? Kuna haja gani kwa PM kuwa na ofisi na makazi katika sehemu mbili tofauti wakati zaidi ya 90% ya muda wake anakuwa Dar es Salaam?? Serikali haioni kwamba mpango wa kuhamia Dodoma UMESHINDIKANA?
Siku za karibuni watu wengi wamechangia threads za ukosefu wa uwezo wa ndugu yetu PINDA. Leo nimelikumbuka hili, Nawasilisha na nitawashukuru wabunge wenye mapenzi ya kweli ya nchii hii kuishinikiza serikali kuamua kusuka ama kunyoa. KAMA TUNAKWENDA DODOMA BASI TWENDE MARA MOJA, KAMA HAIWEZEKANI BASI TUENDELEE KULA UPEPO WA PWANI DAR, LAKINI TUISELEKEZE HELA KULE DODOMA AMBAKO HATUNA MUDA NAPO, HUU NI UFUJAJI WA FEDHA ZA SERIKALI!!