Pinda alisema mamlaka ya usitawishaji makao makuu dodoma haina wasomi,amechukua hatua gani?

misoza Gete

Member
Sep 28, 2012
57
20
Wakuu jana nimeona kwenye tv watu wamevunjiwa nyumba maeneo fulani dodoma,tatizo ni nini?najua inasadikiwa wamevamia maeneo,lakini je cda imefanya nini toka 1973 ilipoundwa?ukifika hapo dodoma ndani ya km 10 tu ni mapori,hivi tukiivunja mamlaka kuna shida?pinda nadhani june au july alipiga mkwala kuwa 70% ya watumishi wa pale hawana sifa ya kuwa hapo,amechukua hatua gani mpaka sasa?duuu babu wa kigogo kalia sana jana tbc hadi aibu nyumba imevunjwa !hebu nipeni mwongozo tuwafanyaje hawa jamaa japo tupime hata eneo la km 40 ifikapo 2015?wanakomaa kuuza viwanja vya rushwa tu katikati ya mji nasikia!mikono inatetemeka kuandika nina hasira sana,nakomea hapo!
 
Kama kuna janga katika mji huo basi ni hao the so called CDA...........from my heart sioni nini wanafanya hao jamaa kuna siku nilikuwa huko nikashuhudia walivyosababisha wananchi kupigwa mabomu ya machozi!!!!!!

Cha ajabu na bunge kukaa Dodoma all these years nao sijwahi wasikia wakikomaa na hili dubwasha au kwa sababu wao wanapewa priority kila vinapogawiwa viwanja??????

Huu mji adui yake mkubwa ni mbunge, meya, RC, mkurugenzi na kwa kiasi fulani bunge linahusika kama huwa wanakaa pale kwa miezi takribani minne kila mwaka na hali ndo kama vile then majibu ni kuwa mji huu hauna mwenyewe.......unatumika kisiasa bhaaaaas!!!!!!

Hawa CDA sijawahi wasikia wamekopa Bank na kuwa na miradi kama ya NHC atleast waweke miuondombinu halafu wauze viwanja kama tatizo ni pesa......ubunifu hakuna na wanaendesha kwa mazoea......ingekuwa amri yangu wakurugenzi pale nafasi zitangazwe upya watu waombe na interview juu ili kupata watu wanaoweza kufanya kazi kwa tija.....as of now hakuna kitu pale............!!!!!!
 
Tatizo rushwa!Sijui tatukuru hawajui green areas za kupata waharifu?Mi naaamini ukienda pale nusu saa tu unakamata watuhumiwa kumi kwa rushwa!TAKUKURU TOENI MFANO BASI PALE WATU TUFURAHI?IPO SIKU NITAENDA KUTAFUTA KIWANJA KULE THEN NIKAMATE MTU HATA KWA KUMNASA KOFI INATOSHA!KIUJUMLA NASIKIA HAKUNA WAKURUGENZI PALE NI MAZOEA TU,NIMEANGALIA KWENYE TOVUTI YAO NAONA VIDUDU TU!NIMEGUNDUA KUWA TANZANIA BILA MAKAO MAKUU INAWEZEKANA!
 
kuna ndugu yangu alifariki 2010 alikuwa na kiwanja kisasa nae alikuwa anakaa kisasa ya wanajeshi,wakati tunaenda kuzika kurudi mke wake kafuatilia kiwanja chao ambacho kilikuwa na matofali na mchanga lakini akakuta kinajengwa hata mwezi bado baada ya mume wake kufariki,alipofuatilia cda akaambiwa mbona kiwanja si mali yake?
amefuatilia mpaka kwa mkurugenzi alichoamriwa ni kwenda kuondoa mchanga na matofali na mpaka leo mjane wa marehemu bado analia.
sina hamu na hilo jina cda.
 
Hii kitu sijui hata inafanya nini maana hakuna progress yoyote ya kuhamia dodoma zaidi ya CDA kuendelea kula hela za walipa kodi.
 
Inabidi tupate updates wamefanya nini hadi sasa toka waundwe na wana muda gani,ila pia tuangalie manispaa ya dodoma wanafanya nini otherwise dodoma kushney!Wakurugenzi wake sijui huwa wakitoka pale wanafanikiwa walipo au ndio vilaza wote.Wana JF inabidi tuweke hoja ya kuwaondoa katika usimamizi wa makao makuu,tutoe contract hata kwa wachiina watengeneze muda kwa 2 years dom iwe kama ulaya!
 
Back
Top Bottom