Pinda akiri polisi wameshindwa kazi!

nimie

JF-Expert Member
Sep 9, 2011
525
104
"Mtoto wa mkulima" kawapiga chini polisi kusimamia zoezi la kuzuia utoroshaji wa sukari nje ya nchi, kisa WANAHUSIKA kufanya escort ya "mzigo".

Rungu wamepewa wanajeshi.

Hapa nina mawazo mawili

1. Kwa hiyo polisi wameshindwa kazi na wakuu wanajua!
2. Hawa wanajeshi nahisi nao wataangukia kwenye rushwa jamani, na wakipotea hawa ndo tumekwisha.
 
Kumbe sukari imekuwa lulu Tanzania kushinda madini yetu. Huyu pm ni mwhehu kweli.
 
It is unfortunate that what we only have in our government system is reactionary leadership. They do not plan, analyse issues and make viable decisions. It is as if they work without technical advisers. Even thought leaders are capable of gathering information they can't correctly act upon it. They are failing to act against their clients because they depend on them to cling on power. The major crises of governance in Africa to date is Neo-patrimonialism. Mr. Pinda's action depicts how patrons react on their clients' actions. Poor Tanzania!

Tanzania Needs a Third Liberation and this is a duty of me and you
 
Ukiona hivyo ujue nchi imekwisha, chukua chako mapema.

Tunaposema state apparatus, tunamaanisha jeshi, mahakama, polisi. Sasa kama vyote hivyo vimeshindwa, unasubiri nini? Mii nadhani tuingie barabarani tuu, kieleweke, au tufanye opposite yake, tupaki mabegi yetu tujiondokee zetu, bora kuwa mkimbizi kuliko kuishi tanzania
 
There is a need to make evaluation on our armed forces are treated.
 
There is a need to make evaluation on how members of armed forces are treated, insteady of blaming them.Eg.How much are they paid?How is their working conditions?How long do they work per day?How is their dwelling areas?e.t.c
 
Hongo ya mfanyabiashara wa sukari ni sawa na mshahara wa polisi kwa miezi hata mitatu. Polisi hawezi kukataa hongo hiyo na pia hawapewi wote anapewa mkuu wao tu wengine wanapewa amri kusindikiza na baadaye wanaambulia posho ya kusindikiza sukari.


Hivi kwa nini sukari inataka kuwa issue? Nadhani sababu za uhaba zinzfahamika ila serikali hii isiyojua inachofanya ina jaribu kupambana na matokeo yake badala ya kupambana na kinachosababisha.

Hivi PM akijiudhuru kuna shida gani anang'ang'ana kwenye cheo ambacho hawezi kutoa matokeo hata kidogo tu.
Shame on you PM!
 
Pole polis kwa kutumiwa na nyie kukubali kutumiwa hasa wakati wa uchaguzi , sasa mtaliipwa nini kama si kuihujumu nchi yenu. Pinda umekuwa mpiga kelele tu maana wewe na mkuu wa kaya siyo kitu kimoja
 
Taarifa za habari leo zimesheheni Tamko la Waziri Mkuu akiwa Bunda: kuwa Jeshi la Wananchi (JW) watumike kudhibiti utoroshaji wa sukari kwenda nchi za jirani kwani kuna taarifa kuwa sasa polisi wanasaidia utoroshaji huo.

Majuzi tu tulimsikia JK akihimiza Wizara ya Maliasili na utalii watumie JW kupambana na majangili sitashangaa na Magufuli akianza kutumia JW kusimamia ubomoaji na Mathayo akawatumia kudhibiti uvuvi haramu na Nundu akawatumia kudhibiti utoroshaji wanyama pori airpoti na Mkulo akawatumia kukusanya kodi na ... Orodha inaweza kuwa ndefu sana ila moja ni hakika haya ni majibu mepesi kwa maswali mazito na uvivu wa kufikiri na kutafakari.

Hivi matamko kama haya yanapotolewa na kiongozi wa ngazi inatuambia nini ikiwa tunajua na wizara ya mambo ya ndani na jeshi la polisi ni sehemu uongozi wake?

Hivi kama somo la uwajibikaji siyo sehemu ya semina elekezi zinazotolewa kila uchao ni kipi kingine kiko huko?

Inanikumbusha kituko kingine cha Sumatra walipoona askari wa usalama barabarani wanazembea wakaajiri Majembe Auction kushika magari mabovu huku wakisindikizwa na askari wa usalama barabarani

Si ingekuwa vema Pinda badala ya kukwepesha wajibu akwataka Waziri Nahodha na IGP wajibu tuhuma za polisi kusindikiza magendo na wakishindwa wawajibike?
 
Nakubaliana na mtoto wa mkulima. mm ninaushaidi kule Tarakea hiyo shuhuli hufanyika sana na polisi.
 
Nakubaliana na mtoto wa mkulima. mm ninaushaidi kule Tarakea hiyo shuhuli hufanyika sana na polisi.

Kwa hiyo kashindwa nani sasa polisi au Pinda? Kwani wakumwajibisha Polisi ni nani siyo Mwema akiwajibishwa na Nahondah akiwajibishwa na Pinda. ili Kalumekenge(Polisi) aende shule tunahitaji tumwajibishe aliye juu yao ili mlolongo uanzae kufanya kazi
 
Hivi hao Wanajeshi na njaa zao za sasa watavimudu vishawishi vya wanamagendo hawa? Nchi imeoza hii. Turuhusu wananchi wayazuie malori haya. Ndani ya siku mbili tu biashara hii itakuwa imekwisha.
 
Nakubaliana na mtoto wa mkulima. mm ninaushaidi kule Tarakea hiyo shuhuli hufanyika sana na polisi.
Haki ya mungu we unastahili kuchapwa viboko matakoni,yaani badala waziri mkuu kutumia mamlaka aliyopewa awawajibishe hao polisi,we unadhani yuko sahihi kusema atatumia wanajeshi,je hao wanajeshi wakipokea rushwa itakuwaje,sukari itaendelea kutoroshwa tu,hapa dawa ni kuwawajibisha wahusika..Mi huwa simkubali Pinda kwa kuwa ni mwoga na hajitambui.
 
Nchi imeoza hii, eti anasema ameletewa taarifa wanaosindikiza sukari ni polisi, sasa kwann asimuulize huyo anayemletea taarifa majina ya hao polisi na kuwawajibisha na sio kuja kupiga kelele kwenye majukwaa?
 
PM anatakiwa kufanya maamuzi sasa anamwagiza RPC asimamie ambaye yuko kwenye pay roll ya hili "deal". Alitakiwa kufanya maamuzi palepale polisi wote border toa kama ushahidi upo peleka mahakamani, kama hakuna tafuta simamisha kazi then watakao kuja hawafanyi tena ujinga sasa utakuta hakuna hatua iliyochukuliwa maneno matupu tu
 
huo ni uvivu wa kufikiri! kwani Nahodha anafanya nini mpaka sukari inaenda nje ya nchi kama hawezi aachie office wengine wafanye kazi! hapo kuna tatizo la kiuongozi na wakuwajibishwa ni mkubwa wao!
 
Taarifa za habari leo zimesheheni Tamko la Waziri Mkuu akiwa Bunda: kuwa Jeshi la Wananchi (JW) watumike kudhibiti utoroshaji wa sukari kwenda nchi za jirani kwani kuna taarifa kuwa sasa polisi wanasaidia utoroshaji huo.

Majuzi tu tulimsikia JK akihimiza Wizara ya Maliasili na utalii watumie JW kupambana na majangili sitashangaa na Magufuli akianza kutumia JW kusimamia ubomoaji na Mathayo akawatumia kudhibiti uvuvi haramu na Nundu akawatumia kudhibiti utoroshaji wanyama pori airpoti na Mkulo akawatumia kukusanya kodi na ... Orodha inaweza kuwa ndefu sana ila moja ni hakika haya ni majibu mepesi kwa maswali mazito na uvivu wa kufikiri na kutafakari.

Hivi matamko kama haya yanapotolewa na kiongozi wa ngazi inatuambia nini ikiwa tunajua na wizara ya mambo ya ndani na jeshi la polisi ni sehemu uongozi wake?

Hivi kama somo la uwajibikaji siyo sehemu ya semina elekezi zinazotolewa kila uchao ni kipi kingine kiko huko?

Inanikumbusha kituko kingine cha Sumatra walipoona askari wa usalama barabarani wanazembea wakaajiri Majembe Auction kushika magari mabovu huku wakisindikizwa na askari wa usalama barabarani

Si ingekuwa vema Pinda badala ya kukwepesha wajibu akwataka Waziri Nahodha na IGP wajibu tuhuma za polisi kusindikiza magendo na wakishindwa wawajibike?


Kumbe JW ndio hawanaga tamaa ya fedha, heri yao.
 
Basi wote wafukuzwe kazi halafu tukodishe askari toka nchi za nje na kuwalipa mishahara na marupurupu manono labda mara 100 ya wanayopata sasa askari wetu.
 
Back
Top Bottom