- Gari alilolikataa ni gari la ubunge ambalo kila Mbunge anatakiwa kupewa anapoanza ubunge, hizo hela za hayo magari zimo kwenye bajeti tayari kwa mujibu wa katiba ya Jamhuri, sasa Mbunge anaweza kukataa gari lakini hawezi kusimamisha katiba eti kwa sababu yeye ni Waziri Mkuu na kuzuia wabunge wengine wasipewe magari.
changanya akili zako, na za mbayuwayu. utapata jibu.
kwamba 'tatizo la umeme nalo litakuwa historia'. (hapa najiandaa. muda wowote umeme utakatwa.)
- Mkuu hamna jipya hapa, unasema wanakopeshwa! halafu hela za kuyalipia zinalipwa nani? Hebu piga hesabu ya hela za mbunge in five years akiwa bungeni hivi kweli anaweza kuyalipia haya magari akamaliza in five years?
- Pole sana mkuu!
Kwa kweli mtoto wa nyoka ni nyoka. Yaani William unatuambia mbunge wa mahenge hawazi kufika kwake bila ya gari la milioni 300? Hivi mbona nyie watu mliokulia kwenye neema mna matatizo sana? Ni mahali gani hapa tanzania ambako Toyota Hardtop (mkonga) haifiki? Tena mkonga inaweza kuwa ya uhakika zaidi kuliko hata hilo shangingi! kwa uwezo wetu mdogo wa serikali, hakuna sababu yoyote ya msingi ya mtu kutumia gari la milioni 300 wakati kuna VX za milioni 120 ambazo na zenyewe zinaweza kufanya kazi sawasawa na hiyo Vx 8. Jamani, hebu wakati mwingine tuwahurumie na wale watu wa vijijini wanaoishi kwa mlo mmoja.
Kashakwambia hakushirikishwa kwenye mchakato..sasa unataka akuapieje?hizo gari zilinunuliwa 65 siku zinahamishwa toka makumbusho usalama wa taifa kwenda ikulu nilitamani kulia.yalikua meupe yote full tank diesel.na zimenunuliwa octoba 2010 swali pinda hakujua kuwa yatanunuliwa?
Sidhani kama huyo angemkataakichwa cha habari 'pinda akataa shangingi'.......sie wakuda tumeelewa vingine...teh teeeeeeeeh
tamko ameshatoa hebu soma vizuri na kwaumakini maeleze hapojuu pinda ameshatoa maagizo yakubana matumizi nakupunguza kwakiasi kikubwa matumizi yakifahari ya pesa zawalalahoi,hongera mkuu pinda kwakuonesha mfano,ila unatakiwa uwemkali kidogo ili agizolako la kubana matumizi lifanyiwe kazi kwavitendo,hakika ukilisimamia hilo kwa umakini nina iman utafanikiwa na utakumbukwa daima nawalalahoi wa nchi hii,na utaandikwa ktk vitabu vya kumbukumbu za histroria ya taifa hili,aluta continua mjomba pinda mimi nakukubalisana,hakika wewe ni muadilifu na usiependa makuu.