Pinda ahitimisha mjadala wa hotuba ya rais bungeni

Nikuulize Waziri Mkuu yafuatayo
Muungano wa Tanzania nini mantiki yake wakati Zanzibar ni nchi inayotambuliwa na OAU, kwa hiyo Rais wa Jamhuri ya muungano hana nguvu Zanzibar. Zanzibar wana Bunge lao na wanashiriki Bunge la Muungano wa Tanzania, hivyo bunge la Tanganyika liko wapi? Wazanzibar wana nafasi ya ajira zaidi katika utumishi wa serikali kuliko wa bara kwa maana kwamba wana serikali ya zanzibar inayowapa ajira na wamo ndani ya serikali ya Muungano wanakopata ajira. Wa bara wamo ndani ya serikali ya Muungano tu kwa kutoundiwa serikali yao ya Tanganyika.

Kuhusu Hospitali ulizoorodhesha nyingi ni zile zilizoanzishwa na taasisi za dini si serikali kama uivyosema. KCMC na Bugando ni za Taasisi za dini si serikali na hivyo serikali haiwezi kujivunia kwamba ni matunda yao. Zahanati, vituo vya afya na hospitali nyingi zimejengwa na taasisi za dini kutokana na mashirika ya dini toka nchi za nje, hivyo ni jambo la aibu kwa serikali kuorodhesha huduma hizo kwamba zimefanya na serikali.

Takwimu za huduma za maji ulizoleta hata mtoto mdogo atakukatalia si kweli, kwani ni pungufu ya asilimia ulizoleta. Waulize tu wa hapo Dodoma wanavyohangaika na maji kama kweli wana 80% ya maji unayosema. Vijijini waziri Mkuu ningekuwa mie ningeona aibu hata kusema afadhali kunyamaa tu.

Elimu ni aibu tupu idadi kubwa ya wanafunzi kushindwa mitihani ambayo kwa Tanzania kiwango cha ufaulu ni chini sana ukilinganisha na mataifa mengine, sasa wanafunzi washindwa hata kupata dalaja la nne, inatisha.
Serikali imeanzisha shule kisiasa kama vile maskini anavyofikiria kuwa na watoto wengi ndio utajiri bila kufikiria malezi bora kwa watoto. Shule hazina maabara, hakuna vyumba vya madarasa, hakuna vitabu vya kiada, hakuna madawati, hakuna walimu, lakini waziri mkuu hukusema hayo. Vyuoni wengi tumesikia mengi yanayolalamikia na wanavyuo.

Huwezi kulinganisha mazingira ya Tanzania ya mwaka 1960 na Tanzania ya 2011, huku ni kuzidi kuwadanganya watanzania. Tanzania ya leo si ile ya kuwaimbia nyimbo za kuwasifu viongozi, bali ni Tanzania ya walioelimika na wenye uhakiki wa hali ya juu.

Hotuba ya Waziri mkuu imekuwa kama kuwapa darasa Watanzania wakati watanzania wanajua wana ufahamu wa hali ya juu sasa katika masuala ya kijamii, kisiasa nk.
Kwa maana hiyo Waziri Mkuu Mizengo Pinda anaendelea kudanganya Bunge na wananchi.
 
Huyu Mh amekaa ki-huruma huruma zaidi. Anakuwa kama babu anayesimulia wajukuu hekaya za alfu lela u-lela. Hana maamuzi; hana mawazo yanayoongeza thamani katika ufahamu zaidi ya kuelezea hisia zake tu. Kibaya zaidi, hajaamka kujua madhara ya kutumika kutoa kauli za ama kupima joto au kujaribu kufunika uozo wa mafisadi. Alipokuwa Waziri wa Nchi alikuwa na heshima yake nzuri (pengine kwa kutosikika sana) lakini sasa wanamharibia kweli kwa kumuweka mbele ya kila uozo unaofanywa na serikali ili angalau ajaribu kuupamba na kauli zake za taratibu. I really pity him.
 
Ni kweli hotuba ya pm ilikuwa nzuri na yenye mvuto kusikiliza ila ameweka kichefuchefu alipo anza kufanya comparison kati ya maendeleo yaliyo fanywa na wakoloni na yaliyopatikana na baada ya miaka hamsini ya uhuru, shule, wanafunzi huduma za afya, barabara nk.ni lazima pm ajue wakoloni wakuja Tanzania kuleta maendeleo ila kunyonya nakuondoka hivyo walivyo acha kwao ni sawa.sasa baada uhuru wenye nchi ndo sasa walitakiwa kufanya kazi kwa bidii kujiletea maendeleo yao wenyewe jambo ambalo serikali ya awamu ya kwanza ilitekeleza kwa dhati sana. Pm katika hotuba yake alitakiwa kufanya comparison ya maendeleo kati ya nchi zilizopata uhuru pamoja na Tanzania ndio aseme kwamba serikali imefanya kazi kubwa au haijafanya kazi yoyote. pia akumbuke serikali inayo lalamikwa ni hii ya jk. awamu ya kwanza ilifanya vizuri sana mbali na kuwa na changa moto nyingi. awamu ya kwanza ililenga katika kujenga misingi ya kuzalisha mali ndo maana kulikuwa na viwanda vingi.sasa hivi wanachakachua tu. Pm alitakiwa aseme dhahili serikari yake imefanya nini na wanatarajia kufanyia nini watanzania maskini.Tuangalie nchi za Asia ambazo zimepiga maendeleo wakati zilikuwa maskini kama sisi.
Wana Jf ejadilini.

Enzi za mkoloni zilikuwa bora kuliko sasa.

1. Ingawa shule zilikuwa chache lakini zilikuwa na ubora wake.

2. Wakulima walikuwa na soko la uhakika la mazao yao.

3. Viwanja vya ndege vidogo katika miji ya wilaya na vijijini kwa mfano wakati wa awamu ya kwanza Mkoa wa Arusha ulikuwa na viwanja Arusha, Oldeani, Mbulu, Haydom, Qurus (Oldeani), Babati, Manyara, Tarangire, Ngorongro, Loliondo Basotu na Magugu. Leo baadhi ya viwanja hivyo, vimetoweka.

5. Matibabu yalikuwa bure.

6. Miji yenye umeme ulikuwa ni wa uhakika.
 
Ni kweli hotuba ya pm ilikuwa nzuri na yenye mvuto kusikiliza ila ameweka kichefuchefu alipo anza kufanya comparison kati ya maendeleo yaliyo fanywa na wakoloni na yaliyopatikana na baada ya miaka hamsini ya uhuru, shule, wanafunzi huduma za afya, barabara nk.ni lazima pm ajue wakoloni wakuja Tanzania kuleta maendeleo ila kunyonya nakuondoka hivyo walivyo acha kwao ni sawa.sasa baada uhuru wenye nchi ndo sasa walitakiwa kufanya kazi kwa bidii kujiletea maendeleo yao wenyewe jambo ambalo serikali ya awamu ya kwanza ilitekeleza kwa dhati sana. Pm katika hotuba yake alitakiwa kufanya comparison ya maendeleo kati ya nchi zilizopata uhuru pamoja na Tanzania ndio aseme kwamba serikali imefanya kazi kubwa au haijafanya kazi yoyote. pia akumbuke serikali inayo lalamikwa ni hii ya jk. awamu ya kwanza ilifanya vizuri sana mbali na kuwa na changa moto nyingi. awamu ya kwanza ililenga katika kujenga misingi ya kuzalisha mali ndo maana kulikuwa na viwanda vingi.sasa hivi wanachakachua tu. Pm alitakiwa aseme dhahili serikari yake imefanya nini na wanatarajia kufanyia nini watanzania maskini.Tuangalie nchi za Asia ambazo zimepiga maendeleo wakati zilikuwa maskini kama sisi.
Wana Jf ejadilini.


Mpuuzi
 
.
Yeleuuuwi uwor'e meso phoe?
Eler'i tsikyeri kufoi, CRDB, NMB, NBC, BOA, CITY NK mabenki wa woose waichur'ie eler'i ipho makapatinyi wake. Suka ndaayo undekur'ikaho tsapho iwinyi.
.
mod nauliza ni lugha ngapi zinaruhusiwa hapa JF?
 
hizo takwimu ni wataalam wamempa au ni hisia zake?hana washauri wazuri huyo mzee,wadarisalama sijui wamelichukuliaje hilo tamko,anyway alakini kule wanakoishi wao hayo matatizo ya mgao wa maji na umeme ni sawa na hip hop yakichina ,hautokaa uisikie kamwe.

kaka yaleyale PM akiulizwa kuhusiana na hizo takwimu, atasema KAAMBIWA. Hivi hakai chini kusoma na ku analyse mambo kabla ya kupresent, kwani enzi hizi si zile za kudanganywa? Au ni kwa vile anajua kila atakaloongea bungeni kuna wapiga makofi wengi ambao hawajui hata wanapiga makofi kwa ajili gani?
 
ni mpuuzi tu, anachofanya ni kujaribu kupunguza hasira za vijana wasifanye yale ya Tunisia na Misri, ni wazi kengere ya hatari inagonga akilini mwao!
 
Back
Top Bottom