Pinda ahalalisha mgomo wa madaktari,huku wanaharakati wakimwaga mboga,haponi mtu kesho.

vimon

Senior Member
Apr 3, 2008
183
195
Pinda amekamilisha mkutano na waandishi wa habari hivi punde na meseji ya kubwa kwa madaktari ni kuwaambia kuwa serikali haiwezekani kushinikizwa na madaktari na kuwafukuza mawaziri Mponda na Nkya. Hivyo, kama wanataka kugoma, wagome tu.

Legal and Human Rights Centre
Mkutano wa Wanaharakati na Waandishi wa Habari: Sehemu ya tamko: "...kama kweli Rais Jakaya Kikwete ana nia ya dhati ya kutetea maisha ya Watanzania, tangu Jumamosi hadi leo angelikuwa amekwishachukua hatua ili kuzuia maafa yatakayotokea ikiwemo vifo zaidi vya Watanzania kutokana na mgomo mwingine wa Madaktari. Wananchi tunamtaka Rais atekeleze madai ya madaktari mara... moja, yakiwemo yafuatayo:

1. Waziri wa Afya na Naibu wake, ambao wameshindwa kujiuzulu hadi sasa wawajibishwe na Rais aliyewaweka madarakani ili wapishe mchakato wa kutatua mgogoro walioshindwa kuudhibiti, uweze kutatuliwa;

2. Huduma ya afya na mazingira ya kazi yaboreshwe haraka iwezekanavyo, kwani hali hiyo ndiyo inawafedhehesha madaktari katika kutumia taaluma walizo nazo;

3. Iwapo serikali haitatimiza hayo, italazimisha umma wa Watanzania kuchukua hatua dhidi ya wote wanaohusika kwa njia ya nguvu za umma, kuanzia Tarehe 07/03/2012;

4. Tunawasihi Watanzania wote wanaojali utu wao na utu wa Watanzania wenzao wawe tayari kuinuka kuchukua hatua itakayoifanya serikali kutimiza wajibu wake katika kuzuia watu zaidi kupoteza maisha. Ni sisi Watanzania wenye uchungu na nchi yetu na maisha yetu. Imesainiwa leo, Tarehe 06/03/2012"

Maswali ya kujiuliza je hawa viongozi wetu wanataka tufe,wakina mama wajawazito nani atawafanyia operesheni na watoto wasio na hatia nani atawahudumia. Tetesi madaktari wamekasirishwa na kauli ya pinda na wameapa kumwonyesha kuwa wao si watu wakupiga siasa.

Angalizo kama unaumwa na huna pesa za kwenda India,jitaidi uende hospitali leo hii. Ukipata Tangazo hili mwarifu na mwenzako.
 
Tunateseka kwa sababu Rais aliye madarakani hakuchaguliwa na watanzania, alitumia pesa yake kupata madaraka, viashiria ndio kama hivi, jifunzeni kwa mfano wa nabii suleiman alipoletewa kesi mbele yake kuwahusu wamama wawili wakivutania kitoto kichanga ki-hai na mwili wa kitoto kichanga kana kwamba mtoto yupi ni wa nani huku kila mmama akidai aliye hai ndiye wake!

(Mmama mmoja wao alifanya hila, alimlalia mwanae usiku akafa, akamchukua wa mwenzie na kumuweka wake aliyekufa ubavuni pa mwenzie. walipoamka tazama mwenzie alipomtazama kwa makini aligundua kitoto kilichokufa si chake mzozo ukaanzia hapo) mfalme suleiman alipoona kila mmoja anang'ang'ania kuwa mtoto mzima ndiye wake, aliamua aletewe shoka ili amcharange vipande viwili awagawanyishe wale wamama.

Yule mwenye mtoto hai aliposikia hivyo akamwambia mfalme akasema mpatie huyu mama mtoto huyu hai usimcharange! lakini yule aliyemlalia kichanga wake akamwambia mfalme akasema "bora umcharange tukose wote!!!"

Ndiposa mfalme suleiman alipotambua ya kuwa kichanga hai kilikuwa cha yule mama aliyebambikiwa na mwenziwe, na akaamuru akichukue kichanga chake. AMINI NAWAAMBIENI kikwete hakuchaguliwa na watanzania. Ni baba gani watoto wake wakimuomba samaki akawapa nyokaaaaaaaaaaaaa!!!!!!!!!
 
kwa kupuuza huku kwa serikali, ni dhahiri maumivu tunayopata wananchi yatashindwa kuvumilika siku za usoni
 
Hivi huyu Hadji mponda na Lucy nkya walizaliwa wakabatizwa kuwa mawaziri wa afya?

Ina maana Rais hayupo serikalini kuliona hili,
Je? ina maana maslahi ya mawaziri wawili wa serikali ni bora zaidi ya uhai wa watanzania wote,?
Je?maslahi ya madaktari si bora kusikilizwa dhidi ya mabosi wao wizarani?
Je? kama Rais yupo na amenyamaza kimya tangu sakata hili lilipoanza,sisi watanzania tumuelewe vipi?
 
Hii nchi,sijui inapokwenda...kama Pinda ndio katoa hiyo kauli basi amepinda na madaktari watamnyoosha.
 
Anatalii Mt. Kilimanjaro, tuliopigika hata tukifa haimhusu
JK hoyeeeee, CCM juuuu!
Na bado, mpaka tutakapokoma kupapatikia mapene ya mafisadi
 
Duh namsukiliza kupitia Radio anasema si busara kumpa Rais ultimutum.

Mimi Nakumbuka hili neno ultimutum lilimpa shida Rais Mwinyi hadi akawafukuza wasomi wote UDSM. Kuwapa viongozi ultimutum ni suala gumu manake kama atatekeleza hilo nini kitafuata.
 
Aisee mbona sielewi..........kama madaktari wamekwambia kuwa wanaoleta kauzibe ni mponda na nkya sasa inakuwaje?
 
capitalist at work..
TAJIRI ataenda AGHAKAN,MASKINI ATAKUFA/ATAENDA KWA MGANGA...
 
Mdaktari wataogoma wauliwe. Kwani hao ni wauwaji. Matatizo yao yalishasikilizwa na Pinda na wameahidiwa kuwa yatatimizwa. Sasa wanaingiza siasa, Katibu Mkuu alishasimishwa, na serikali isiwakubalie, wakigoma wauliwe kwa kila kifo kitachosabishwa na mgomo wao.

Kikwete wasikuendeshe hawa jamaa, waoneshe ni nani Rais, wewe au wao.
 
Wanaharakati hawana walijualo zumbukuku toka siku waliyosema nguvu ya umma mpaka leo nasikia wao tuu wakikololoma kama kisu butu. Na wao kama wameshindwa utetezi na harakati wakae kimya kwani ni lazima kuongea utumbo?
Pinda amekamilisha mkutano na waandishi wa habari hivi punde na meseji ya kubwa kwa madaktari ni kuwaambia kuwa serikali haiwezekani kushinikizwa na madaktari na kuwafukuza mawaziri Mponda na Nkya. Hivyo, kama wanataka kugoma, wagome tu.

Legal and Human Rights Centre
Mkutano wa Wanaharakati na Waandishi wa Habari: Sehemu ya tamko: "...kama kweli Rais Jakaya Kikwete ana nia ya dhati ya kutetea maisha ya Watanzania, tangu Jumamosi hadi leo angelikuwa amekwishachukua hatua ili kuzuia maafa yatakayotokea ikiwemo vifo zaidi vya Watanzania kutokana na mgomo mwingine wa Madaktari. Wananchi tunamtaka Rais atekeleze madai ya madaktari mara... moja, yakiwemo yafuatayo:

1. Waziri wa Afya na Naibu wake, ambao wameshindwa kujiuzulu hadi sasa wawajibishwe na Rais aliyewaweka madarakani ili wapishe mchakato wa kutatua mgogoro walioshindwa kuudhibiti, uweze kutatuliwa;

2. Huduma ya afya na mazingira ya kazi yaboreshwe haraka iwezekanavyo, kwani hali hiyo ndiyo inawafedhehesha madaktari katika kutumia taaluma walizo nazo;

3. Iwapo serikali haitatimiza hayo, italazimisha umma wa Watanzania kuchukua hatua dhidi ya wote wanaohusika kwa njia ya nguvu za umma, kuanzia Tarehe 07/03/2012;

4. Tunawasihi Watanzania wote wanaojali utu wao na utu wa Watanzania wenzao wawe tayari kuinuka kuchukua hatua itakayoifanya serikali kutimiza wajibu wake katika kuzuia watu zaidi kupoteza maisha. Ni sisi Watanzania wenye uchungu na nchi yetu na maisha yetu. Imesainiwa leo, Tarehe 06/03/2012"

Maswali ya kujiuliza je hawa viongozi wetu wanataka tufe,wakina mama wajawazito nani atawafanyia operesheni na watoto wasio na hatia nani atawahudumia. Tetesi madaktari wamekasirishwa na kauli ya pinda na wameapa kumwonyesha kuwa wao si watu wakupiga siasa.

Angalizo kama unaumwa na huna pesa za kwenda India,jitaidi uende hospitali leo hii. Ukipata Tangazo hili mwarifu na mwenzako.
 
Maamuzi ya kikao cha madaktari AMANA hospital kilichofanyika sa 6 mchana mpaka sa 8 hatimaye yamebarikiwa na PINDA.Nadhani hakutakuwa tamko lingine la serikali kwani PM ndo serikali mwenyewe...ALUTAAAA.
serikali isifanye utani
 
Hivi huyu Hadji mponda na Lucy nkya walizaliwa wakabatizwa kuwa mawaziri wa afya?

Ina maana Rais hayupo serikalini kuliona hili,
Je? ina maana maslahi ya mawaziri wawili wa serikali ni bora zaidi ya uhai wa watanzania wote,?
Je?maslahi ya madaktari si bora kusikilizwa dhidi ya mabosi wao wizarani?
Je? kama Rais yupo na amenyamaza kimya tangu sakata hili lilipoanza,sisi watanzania tumuelewe vipi?

Rais hashinikizwi na ma-dr vilaza wasiojua wajibu wao na kukalia kutetea matumbo yao.

To hell with madaktari wanaopanga kugoma.

Hongera Pinda, serikali haitishiwi nyau,.....so far imewavumilia sana hawa ma-dr katika kuwasikiliza.... pamoja na kwamba madai yao mengine ni ya kipuuzi, kihuni na kilafi.
 
Mdaktari wataogoma wauliwe. Kwani hao ni wauwaji. Matatizo yao yalishasikilizwa na Pinda na wameahidiwa kuwa yatatimizwa. Sasa wanaingiza siasa, Katibu Mkuu alishasimishwa, na serikali isiwakubalie, wakigoma wauliwe kwa kila kifo kitachosabishwa na mgomo wao.

Kikwete wasikuendeshe hawa jamaa, waoneshe ni nani Rais, wewe au wao.

Walllah tutawapiga mawe mitaani. Tumewachoka.
 
Pinda kweli wewe umedhihirisha jinsi usivyo kuwa na maamuzi na huna busara kwani katika makubaliano ya awali na madaktari, ulimwondoa katibu mkuu wa wizara ya afya na mganga mkuu kama madaktari walivyo pendekeza na ukakubaliana na pendekezo lao kuhusu waziri na naibu wake lakini kwakuwa jukumu hilo lilikuwa juu ya uwezo wako, uliahidi kuliwasilisha kwa rais na kumshauri ipasavyo, maana yake wafukuzwe. Leo unakuja na kauli ya kitoto kabisa kuwa serikali yako haishinikizwi? Wakati ule unachukua hatua za kuwaondoa Nyoni na Mtasiwa mbona ulikubali shinikizo? Huna maamuzi na busara zako ndogo. Rais anapaswa akutimue wewe ndo umeshindwa kazi kwani mawaziri wote wako chini yako na uozo wa wizara yeyote ni uzembe wako. Wajibika.
 
tgnp1.jpg tgnp2.jpg tgnp3.jpg tgnp4.jpg tgnp7.jpg tgnp5.jpg tgnp6.jpg
 
Wakuu anayeweza kuzikuza hizo image kwenye posti namba 19 ili zisomeke vizuri.
 
Back
Top Bottom