Pima hoja za Mnyika na Nape juu ya shutuma za mauwaji ya wana-CHADEMA

Dec 11, 2010
3,321
6,328
Hivi karibuni chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kilielezea
kile ilichoeleza kuwa ni kutishwa na wimbi la mauaji yanayotishia
amani ya nchi kikidai kuwa jumla ya wanachama wake 15 wameuawa katika
wilaya ya Igunga peke yake.

Madai hayo ya CHADEMA, pamoja na wanachama wengine na mashabiki wao,
yalitolewa na Mwenyekiti wa chama hicho Freeman Mbowe, ambaye alidai
kuwa mauaji hayo yana mkono wa serikali ya CCM, ambayo kwa madai yao
imeona wazi kuwa upepo wa kisiasa umekiendea vibaya na sasa kinataka
kujiimarisha katika utawala kwa kuua watu wanaoipinga.

Akifungua kikao cha Baraza Kuu la chama hicho jijini Dar es Salaam
Aprili 29 mwaku huu mwenyekiti huyo alifafanua kuwa mbali na kuuawa
kwa watu wanne kwa pamoja na juzi kifo cha mwenyekiti wao wa tawi huko
Arumeru mkoani Arusha, jumla ya wanachama wake 15 wameuawa katika
wilaya ya Igunga peke yake tangu kumalizika kwa uchaguzi mdogo wa
jimbo hilo mwaka jana.

Mbowe katika maelezo yake alijaribu katika maeneo kadhaa kuihusisha
CCM na au serikali yake katika matukio kadhaa yaliyowakabili baadhi ya
wanachama na viongozi wa Chadema katika maeneo mbalimbali nchini
likiwemo lile la Mbunge Highness Kiwia ambaye Suala lake bado Lipo
mikononi mwa vyombo Vya dola likishughulikiwa.

Katika sehemu kubwa ya maelezo ya Ndg. Mbowe amejitahidi kuonesha kuwa
mauaji yote yaliyoikabili na yatakayokuwa yakiikabili Chadema kupitia
wafuasi wake yanafanyika kisiasa, Jambo ambalo ni la uzushi, kwani
Halina ushahidi wa kisheria hata kimazingira, wa Moja kwa Moja
unaoondosha ujinai au makosa hayo, na kuwa ni makosa yanayolenga
muktadha wa kisiasa.

Huku akitaka kuuaminisha umma kuwa huo ndio ukweli, Ndg. Mbowe
amesisitiza kuwa hilo lime kuwa likitekelezwa na CCM kwa lengo la
kuwatisha wananchi kujiunga na chama hicho hoja ambayo haina msingi
wowote wa kiutafiti.

Hivyo CCM kwa kutambua kuwa Suala la mauaji linabeba Kosa la jinai, na
kwa kuwa Ndg. Mbowe ameshutumu Moja kwa Moja CCM na serikali yake
kuihusisha na mauaji hayo, ni vema sasa nasi tukatoa msimamo wetu
dhidi ya tuhuma, hiyo.

Kwanza, si busara hata kidogo kuihusisha CCM katika matukio hayo,
kwani uchunguzi unaofanywa na vyombo vya dola umeshindwa mpaka sasa
kuhusisha matukio hayo na siasa, badala ya kuyahusisha na makosa ya
jinai ambayo hufanywa na watu kwa malengo tofauti na yale ambayo Ndg.
Mbowe anataka kuwaaminisha watu.

Pili, CCM haijawai, haiwezi, na haitakuja fanya jambo lolote lenye
lengo la kuvuruga Amani na Usalama wenye utulivu ndani ya taifa letu,
hivyo uzushi na usingiziaji uliofanywa na Mtu Kama Ndg. Mbowe, si vema
kuuacha kimya, badala yake nimetumia wasaa Huu muhimu Kujibu, na kutoa
ufafanuzi ili Kuupa umma wa watanzania habari sahihi.

Ni aibu kwa Chama kama Chadema kujitahidi kwa nguvu zote kujaribu
kuficha ukweli wa mauaji yanayotoa roho za watanzania wenzetu kwa
kuyapa sura ya kisiasa. Hizi ni juhudi za makusudi za kutaka kuficha
ukweli wa kinachotokea.

Ni aibu kwa chama kama Chadema kujaribu kutumia mauaji mabaya kama
haya kutafuta mtaji wa kisiasa. Huku ni kuonyesha jinsi gani
wamefilisika kisiasa mpaka wanafikia mahali pa kuamini kuwa wanaweza
kutumia chochote kama mtaji wa kisiasa, vikiwemo vifo vya watanzania
wenzetu. Huku si kufilisika tu ila kwakweli ni unyama unaotakiwa
kulaaniwa na kila muungwana.

Mwisho.

Imetolewa na:
Nape Moses Nnauye
Chama Cha Mapinduzi
Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi CCM

XXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXX

Taarifa hii ya CCM inadhihirisha masuala kadhaa ya msingi;

mosi, kwamba chama legelege huzaa serikali legelege. Ulegelege wa serikali katika kushughulikia masuala ya mauji ya raia ni matokeo ya CCM kushindwa kuonyesha kwa vitendo inavyothamini utu na uhai wa binadamu. CCM isingekuwa legelege ingeiwezesha serikali inayoongozwa na wanachama wake kufanya uchunguzi wa vifo vyenye utata (inquest) kupitia mahakama maalum (coronary court).

Pili, kwamba CCM imekosa uhalali wa kimaadili wa kukumea vitendo hivyo na kuchukua hatua zinazostahili kwa kuwa wanazungumza maneno matupu ya amani na utulivu huku viongozi na wanachama wake wanafanya matendo ya vurugu na umwahaji damu. Nape anasema hakuna ushahidi wa kimazingira, wakati anajua kwamba mpaka sasa kuna majalada yamefunguliwa dhidi ya viongozi wa CCM Kiteto, Busanda, Biharamulo kwa vitendo vya umwagaji damu kwenye kampeni za chaguzi ndogo. CCM inajua pia kifo cha kiongozi wa CHADEMA Arumeru mpaka sasa kuna viongozi wake wamekamatwa na kuhojiwa na polisi. CCM inajua kuwa makada wake wametajwa kwa majina kwenye tukio la kukatwa mapanga kwa wabunge wa CHADEMA Mwanza tukio ambalo mashahidi wameeleza kuwa hata Askari polisi wameshuhudia na kuachia litokee.

Na CCM inajua kilichomo mpaka sasa kwenye jalada la uchunguzi la mauji ya Mbwana Masudi kule Igunga. Orodha ni ndefu ya watu na matukio, hivyo taarifa ya CCM ya kutoa kanusho la ujumla ni ishara ya kufisha ukweli na kugeuza mjadala suala ambalo halitafanikiwa, tamko hili la Nape ni kama Al Sahaf kule Iraq, CCM ikae vikao vyake vya kikatiba itoe maamuzi ya chama hicho kuhusu suala hili la umwagaji damu na mauaji ambayo yanatuhumiwa kufanywa na viongozi wa chama hicho pamoja na vyombo vya dola sio kwa wanaCHADEMA tu bali hata kwa wananchi wa kawaida. Inapaswa kuwa kutoka kauli ya amiri jeshi mkuu na kiongozi wa serikali Rais Jakaya Kikwete. Tunachohitaji kusikia ni hatua kuchukuliwa kwa wahusika kama kweli hawajatumwa na CCM na serikali na sio propaganda.

Tatu, imekuwa ni kawaida ya CCM kuanza kwa kuukana ukweli unapotolewa lakini hatimaye hukiri sehemu ya ukweli huo kama zilivyokuwa kauli za CCM mara baada ya kutolewa hadharani kwa Orodha ya Mafisadi. Walianza kwa kanusho lakini hatimaye wakakubali kuna ufisadi ila wakadai mafisadi ni baadhi ya wanachama na sio chama, lakini mpaka leo wameshindwa kujivua gamba kama walivyodai. Hata hili, wameanza kwa kukukana baadaye wanatesema ni la wanachama wachache waliotenda jinai bila kutumwa na chama, lakini ukweli utabaki kwamba haiwezekani matendo yote haya yakajirudiarudia bila vyombo vya ulinzi na usalama kufahamu. Na tunazo taarifa juu ya mikakati ya CCM ya vurugu na vikundi wanavyotumia kufanya uharamia, na yapo majalada ambayo yamefunguliwa polisi. CCM inahitaji ushahidi gani zaidi toka kwa CHADEMA na umma?

John Mnyika
 
Hapa sasa ndo tunapata uhakika kwanini watu wa Ubungo walimchagua Mnyika na kumwacha huyu Nape, soma maandishi yao then utaona nani kichwa hapo!
 
mouddymtoi ni ndefu sana ntaipitia taratibu ila kifupi tu huwezi kuwalinganisha Nape na Mnyika kwani sera za vyama vyao zinatofautiana sana.
 
Last edited by a moderator:
Kumlinganisha Mnyika na Nape ni sawa na kulinganisha mlima Kilimanjaro na kichuguu. Uliangalia maelezo ya Mnyika ni mafupi, ya kueleweka na yenye mantiki wakati maelezo ya Nape ni marefu tu lakini hayaeleweki wala hayana mantiki.
 
Hivi nani alisoma na Nape o level alipata div gani na A level alipata nini? Manaake msije mkawa mnaelezea mambo magumu!
 
Inawezekana alisoma shule nzuri na kafaulu vizuri lakini kwa kuwa ameamua kujitoa fahamu na kumeza utambi mchafu lazima atoe uchafu, maneno marahisi ya kumuelezea Nape unaweza kuyasoma kwenye michango ya wadau wengi jinsi wanavyomuelezea. Kuna mchangiaji mmoja aliwahi kusema kuwa "Kinachoingia kwenye uchafu ni uchafu"
 
Hoja zote mbili yaani ya Nape na ya Myika zina mashiko....... Ya Nape, si vema kuwaaminisha watu hata mwana CDM akiiba na kuuwawa na rai wema basi ameuwawa na CCM kwakuwa ni mwana CDM Ya Mnyika, ni kweli CCM imeshindwa wajibu wake kama mtawala
 
Kama Nape uwezo wako wa kuelezea mambo ndiyo huu basi ujue kuwa unathibitisha kile ambacho unadhani unakikana. Kwa kifupi ninapenda nichambue maelezo ya Nape kama nnilivyonukuu kama ifuatavyo:

Kwanza, si busara hata kidogo kuihusisha CCM katika matukio hayo,
kwani uchunguzi unaofanywa na vyombo vya dola umeshindwa mpaka sasa
kuhusisha matukio hayo na siasa, badala ya kuyahusisha na makosa ya
jinai ambayo hufanywa na watu kwa malengo tofauti na yale ambayo Ndg.
Mbowe anataka kuwaaminisha watu.

"My take 1.
Uchunguzi unaoendelea kushindwa kuhusisha matukio hayo kuwa ya kisiasa hauwezi kuamanisha wala haiwezi kuwa sawa na kusema kuwa hauna uhusiano na siasa. Kama mfano ulio wazi wa wabunge wa CDM kushambuliwa siku moja kabla ya uchaguzi wa diwani kule Kirumba - Mwanza hauna uhusiano wa kisiasa ni lini jambo litakuwa na uhusiano wa kisiasa? Sambamba na hilo, katika tukio la Kirumba - Mwanza, waliokumbwa na mkasa waliwataja watuhumiwa kuwa ni viongozi wa Umoja wa vijana wa CCM, je walikamatwa na kuhojiwa?

Ndugu Nape, ni kutokutumia akili kutuamisha kuwa makosa ya kijinai hayawezi kuwa na malengo ya kisiasa. "

Pili, CCM haijawai, haiwezi, na haitakuja fanya jambo lolote lenye
lengo la kuvuruga Amani na Usalama wenye utulivu ndani ya taifa letu,
hivyo uzushi na usingiziaji uliofanywa na Mtu Kama Ndg. Mbowe, si vema
kuuacha kimya, badala yake nimetumia wasaa Huu muhimu Kujibu, na kutoa
ufafanuzi ili Kuupa umma wa watanzania habari sahihi.

"My take 2:Kusema kuwa CCM haiwezi na haitakuja kufanya jambo lolote lenye lengo la kuvuruga amani na utulivu ni kushindwa kutumia mantiki kabisa. Kwanza, CCM haina kinga ya kutokufanya hivyo na pili siyo kitu kilicho nje ya hulka (nature) yake. Hata kama haijawahi kufanya huko nyuma, lakini hatuwezi haitaweza wala haitakuja kufanya hivyo, kwa sababu hatujui mambo yaliyo huko mbele.

Unapojibu hoja za Mbowe na kusema unataka kuwapa Watanzania habari sahihi, hiyo habari sahihi ni ipi? Ndiyo hiyo ya CCM kwamba "
haijawai, haiwezi, na haitakuja fanya jambo lolote lenye lengo la kuvuruga Amani na Usalama wenye utulivu ndani ya taifa letu..." Usahihi katika maelezo hayo upo wapi?"

Ni aibu kwa Chama kama Chadema kujitahidi kwa nguvu zote kujaribu
kuficha ukweli wa mauaji yanayotoa roho za watanzania wenzetu kwa
kuyapa sura ya kisiasa. Hizi ni juhudi za makusudi za kutaka kuficha
ukweli wa kinachotokea.

"My take 3:
CDM hawajaficha ukweli bali ndiyo wameutoa kwamba CCM wanahusika katika matukio ya mauaji ya Wanachadema. Na kama huo siyo ukweli basi Nape unaposema kuwa wanaficha ukweli kwa makusudi, huo ukweli unaofichwa uko wapi na mbona huutaji? Kwa hiyo Nape usizunguke tu na maneno bali ueleze kinachoeleweka."

Ni aibu kwa chama kama Chadema kujaribu kutumia mauaji mabaya kama
haya kutafuta mtaji wa kisiasa. Huku ni kuonyesha jinsi gani
wamefilisika kisiasa mpaka wanafikia mahali pa kuamini kuwa wanaweza
kutumia chochote kama mtaji wa kisiasa, vikiwemo vifo vya watanzania
wenzetu. Huku si kufilisika tu ila kwakweli ni unyama unaotakiwa
kulaaniwa na kila muungwana.

"My take 4:Ni kwa vipi CDM wanataka kutumia mauaji ya wanachama wake kama mtaji? Kwamba wanawaua wanachama wao ili wawasingizie CCM? Hivi CCM hawana watu wanaojua kupanga hoja zinazoeleweka? Ninachojua CDM hawaibuki tu wakati watu wanapouawa na kusema kuwa mauaji yana malengo ya kisiasa na kwamba CCM wanahusika bali wanatoa na maelezo ya kwamba kwa jinsi gani matukio yanahusiana na siasa."

Mwisho.

Imetolewa na:
Nape Moses Nnauye
Chama Cha Mapinduzi
Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi CCM
 
Kweli Nape ni senior state Vuvuzela kama mwana Jf mmoja aliyesema kwenye post moja humu jamvini,haiwekekani kama kuna watu hadi wamefunguliwa majalada na ni wana ccm,bado yeye anakanusha,sitashangaa siku akila kipigo toka kwa ... then akakana sijapigwa huku akiwa na manundu kibao!
Asubuhi njema wanabodi
 
mbona nape hajaweka wazi ukwel upi cdm wanaufcha? Ni nafas ipi wanataka kuitumia kama mtaj wa kisiasa? Au ndo habari za kishirikina za baba kumuua mwanae apate mali? Kama ukwel anao si autoe tuufaham.
 
Hoja zote mbili yaani ya Nape na ya Myika zina mashiko....... Ya Nape, si vema kuwaaminisha watu hata mwana CDM akiiba na kuuwawa na rai wema basi ameuwawa na CCM kwakuwa ni mwana CDM Ya Mnyika, ni kweli CCM imeshindwa wajibu wake kama mtawala
We Ndg. ni wa siku nyingi sana humu JF tangu 2009, sasa kama michango yote tangu wakati huo ndiyo hii basi huna mchango muhimu humu JF hivi mauaji yote yaliyo fanyika yanaendana na Uharifu? kumbuka Igunga wakala wa CDM alitekwa na kuokotwa baada ya siku kadhaa akiwa mfu, Mwenyekiti wa CDM huko Arumeru amachinjwa, Kibaha mtu aliyekuwa CCM baada ya kujiunga na CUF akauawa pia ukumbuke na wale vijana 4 wa Arumeru hawa nawafanisha na tukio la Igunga sasa swali la kujiuliza mbona CCM hawauawi?
 
We Ndg. ni wa siku nyingi sana humu JF tangu 2009, sasa kama michango yote tangu wakati huo ndiyo hii basi huna mchango muhimu humu JF hivi mauaji yote yaliyo fanyika yanaendana na Uharifu? kumbuka Igunga wakala wa CDM alitekwa na kuokotwa baada ya siku kadhaa akiwa mfu, Mwenyekiti wa CDM huko Arumeru amachinjwa, Kibaha mtu aliyekuwa CCM baada ya kujiunga na CUF akauawa pia ukumbuke na wale vijana 4 wa Arumeru hawa nawafanisha na tukio la Igunga sasa swali la kujiuliza mbona CCM hawauawi?
kibogo najua unapenda kusikia tu mtu akiipamba CDM au akiiponda CCM basi........kuna wengine hatuangalii mambo haya kwa jicho la upofu wa mahaba ya vyama., inawezekana hayo mauji yapo kweli lakini si sahihi pia kusema kila mauji yaliotajwa ya mwana CDM ni mbinu ya CCM kuwatisha eti wananchi wasiingie upinzani........
 
Last edited by a moderator:
Naona Nape Mwenyewe Hajui AU anaficha Ukweli!! Najua kuna Vijana wapo Trained kwa kazi Hizi!! Wala Hawapo kwenye green Guard!! Ila ni Vijana wa kiuni ambao wanapatikana maeneo ya Ubungo Maziwa Wakijifanya kufanya Kazi nyingine Huku kwenye Chaguzi wakienda Kutimiza Azma Zao!!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom