Jumakidogo
R I P
- Jul 16, 2009
- 1,851
- 417
Nimekitumikia chama changu kwa uaminifu mkubwa sana kwa miaka mingi sasa. Watu wenye wivu na maendeleo yangu wametumia kila mbinu kunichafua mbele ya watanzania. Lakini kwa nguvu za mungu hawata weza. Mimi ni muumini mzuri, tena sichagui kanisa katika kufanya ibada. Ni mtu wa watu, natoa harambee nyingi kuchangia miradi ya jamii hasa makanisa. Lakini imefikia wakati ajadiliwa, ajenda kubwa kila kona wabaya wangu wanataka nifukuzwe uanachama. Naamini, hata kama nikifukuzwa. Uwezo wa kuanzisha chama changu cha siasa ninao. Iwe isiwe, mbio za urais zijazo lazima nishiriki, iwe kwa chama hiki, au kile nitakachokianzisha baada ya kufukuzwa. Najua kwenye jamvi hili wapo watakaonitukana kwa sababu wengine akili zao zimepinda kama upinde wa mvua. Lakini kelele za chura hazimzuii tembo kunywa maji...Watu wangu hoyeee. Chama chetu hoyee, Chama changu hoyeeee. Ahsanteni sana.