Pichani, Daraja Kigamboni hiloo... Kigamboni yakufikirika yawa kweli

jamani hicho mkionacho ni matayarisho ya njia itakayotumika kupitishia vifaa wakati wa ujenzi
 
Kwenye hiyo picha ya pili, upande wa kushoto kuna watu watatu wamesimama mmoja amevaa nguo nyeupe. Wamefuata nini?
 
Hiyo itatumika kama bypass kwa ajili ya kupitisha mitambo na mizigo ya wajenzi!!!! Kadili ya maongezi ya jamaa!!!!
 
kwenye michoro kuna madaraja zaidi ya mawili....huenda hilo ni mojawapo.....tusubiri mwisho wake litakuwaje.....maana hata fundi nguo ukimpelekea kitambaa akushonee suti buanza na kukikatakata..waweza dhani anaharibu kumbe ndo njia ya kuweka mambo sawa
Pia yaweza kua ni "diversion" manake engineers wana mambo kweli. ....wanajitengenezea njia yao ya kupita wakati wanawatengenezea yakwenu..!
NI MAWAZO YA MAHESABU
 
Kidogo kidogo tutafika tu. Ndo maana vigogo wakawahi plot za geza na kibada. Hiyo daraja ikikamilika mtanzania wa kawida hataweza tena kupata kiwanja pande hizo!
 
Ndio ukweli, na hata kama hili daraja lina uwezo huo si rahisi kuisoma picha kwa vile picha hajapigwa kwa kiwango cha vipimo vya kujua upanda wa daraja. Mpiga picha alijitahidi kuvuta lens ili kupata taswira ya hatua za ujenzi ilipofikia, huenda tunatoa hitimisho mapema kabla hatujawa na uhakika wa vipimo vya ukubwa huo.

images
images
images
images
images
images
images


Madaraja kama haya ambayo tunaona picha zake, si rahisi kujua yana lane ngapi, kwa vile picha haiwezi kutoa scale ya ukubwa.

thank u mkuu...
umepanua mawazo ya wengi...wazee wa kuponda...tayari walishasema ni kadogo...wanadamu hatuna jema!
 
jamani hili sio daraja hilo ni la muda tu . Msiwe wavivu wa kufikiri. Sawa.
 
Watu wanaogapa kumpongeza Ndugu Jakaya kisa eti Watavuliwa uanachama wa Chaga Jazz Band pale wanaukoo watapokutana!
 
Rami haifunikwi asili yake kwa kupakwa chokaaa J>K is Bomb lililodidimiza Tanzania, nakuitokomeza kabisa, itachukua miaka kama saba kusafisha uchafu alioweka huyu bwana ili tuanze kuwa na nchi iliyotukuka Mungu tusaidie! hata matango pori yamefanikiwa kuongoza vichwa mil zaidi ya arobaini..
 
Mchakato mzima wa kujenga daraja ulianza sometime back. JK amekamilisha tu. Tumpongeze kwa lipi? Siasa pendwa hizi...

Kuna michakato ya kila aina si ya kujenga daraja tu, ipo kwenye makaratasi na ndoto za mchana, kabla wewe na mimi hatujakuwepo, Jee, tuipongeze kwa kuwa ipo kwenye ndoto zao au tumpongeze aliyeifanya ikawa kweli na si ndoto tu? Fikiri.

Kikwete anafanya kweli.
 
Mchakato mzima wa kujenga daraja ulianza sometime back. JK amekamilisha tu. Tumpongeze kwa lipi? Siasa pendwa hizi...

Tumpongeze kwa kukamilisha kama ulivyosema,,, au hujui kama kukamilisha ni kazi pia?

Si unaona timu yetu wa Taifa wanasema haina UMALIZIAJI... teh teh teh
 
Tumechangia sana baada ya kuonekana miaka hii zikawa nyingi ndio ikaonekana kuna haja ya asilimia 60% ya michango yetu ichangie na serikali imalizie hiyo 40% (kwa hili kudos kwa serikali na si JK pekee si unajua mlolongo huu ni wa siku nyingi) ila na sie wenye hela pia utupongeze zomba kwani kuna shida gani.

Swali la kizushi; Kwani idea ya kujenga hilo daraja imetoka lini? na upembuzi yakinifu umefanyika lini?

Idea ya kujenga hili daraja aliitowa babu yake babu yangu mwaka 1919 na ramani alichora. Mchoro wa kwanza ulikuwa ni wake lakini alichora itumike mianzi na udongo wa mfinyazi uliochanganywa na mayai ya kuku wa kienyeji kuufanya ukamatane vizuri na kuwa "salt water proof". Bahati mbaya ikaonekana kuku wanaoweza kutoa aina ya mayai yanayofaa kwa kazi hiyo wanapatikana Iguguno tu huko Singida na itachukuwa miaka 35 kupata kuku na mayai ya kutosha. Kwa hayo plan yake ikarudishwa kwa maboresho na re-design. Zikabaki ndoto na mawazo ya kila aina na kila watu mpaka hapa tulipofikia.

Michoro ya daraja la sasa na upembuzi yakinifu imeanza mwaka 2007 na kumalizika 2010. Na Jakaya Mrisho Kikwete kwa kushauriana na Dokta Ramadhan Dau wameweza kutimiza ndoto za muda mrefu na kazi imeanza kwa kasi zaidi kama picha zinavyoshuhudisha.
 
Kuna michakato ya kila aina si ya kujenga daraja tu, ipo kwenye makaratasi na ndoto za mchana, kabla wewe na mimi hatujakuwepo, Jee, tuipongeze kwa kuwa ipo kwenye ndoto zao au tumpongeze aliyeifanya ikawa kweli na si ndoto tu? Fikiri.

Kikwete anafanya kweli.

Ninachofahamu ni kuwa process ilianza muda mrefu. Akikamilisha katiba njoo na thread ya kumpa pongezi.
 
quote_icon.png
By Dr. Kupeng'e

Haka kadalaja sijui katakuwa kanapitwa vitz tu peke yake? kwanini plan isewe 4 ways?
tatizo planner wa kibongo wanaproject 2 years to come not 50 years to come
Dr. Kupeng'e nadhani ulijibu haraka, hata udaktari wa falsafa huanzia na elimu ya msingi na kupanda kidogo kufikia bachela kabla ya kuamua kuibukia graduate college yenye kukutuza PHD.

Little is better than nothing. Madaraja mengi kutokana na gharama kubwa iliyopo hujengwa kwa kusaidia tatizo la wakati uliopo, siku za usoni upo uwezekano wa kupanua kwani hakuna lisilowezekana.

Unataka Ulaya nao waige kujenga hotel ya kitalii kama ya Tanzania inayoongoza number one kwa miaka miwili mfululizo? Jibu hapana kwa sababu kila kifanyikacho hutegemea uchumi, mazingira na uwezo.
Yani nyie na utaalamu wenu wote hamjui kuwa kuna matayarisho ya ujenzi? hicho kinachoonekana pale ni maandalizi (Preliminaries & Mobilization) Daraja litajengwa kubwa la njia sita (3/3)
 
Ninachofahamu ni kuwa process ilianza muda mrefu. Akikamilisha katiba njoo na thread ya kumpa pongezi.

Idea ya kujenga hili daraja aliitowa babu yake babu yangu mwaka 1919 na ramani alichora. Mchoro wa kwanza ulikuwa ni wake lakini alichora itumike mianzi na udongo wa mfinyazi uliochanganywa na mayai ya kuku wa kienyeji kuufanya ukamatane vizuri na kuwa "salt water proof". Bahati mbaya ikaonekana kuku wanaoweza kutoa aina ya mayai yanayofaa kwa kazi hiyo wanapatikana Iguguno tu huko Singida na itachukuwa miaka 35 kupata kuku na mayai ya kutosha. Kwa hayo plan yake ikarudishwa kwa maboresho na re-design. Zikabaki ndoto na mawazo ya kila aina na kila watu mpaka hapa tulipofikia.

Michoro ya daraja la sasa na upembuzi yakinifu imeanza mwaka 2007 na kumalizika 2010. Na Jakaya Mrisho Kikwete kwa kushauriana na Dokta Ramadhan Dau wameweza kutimiza ndoto za muda mrefu na kazi imeanza kwa kasi zaidi kama picha zinavyoshuhudisha.
 
Daraja halijajengwa na kodi za wananchi, bali ni mwekezaji ambaye daraja hilo tutalivuka kwa kulipia. Sijajua itachukua miaka mingapi mwekezaji kurudisha gharama kisha tupate huduma bure.

Mimi hapa ndio nilishangazwa eti watu watavuka kwa kulipia...sielewi..!!

Na vipi ile habari ya kuwa Kigamboni imeuzwa??
 
Back
Top Bottom