Picha za mbunge viti maalum joyce mukya (chadema) akitoa zawadi ya sikukuu kwa yatima

Rucho Ongiri

Member
Dec 23, 2011
7
3
Picha ya 1
Mbunge wa Viti maalumu mkoa wa Arusha Joyce Mukya (Chadema), kushoto, akikabidhi zawadi kwa mwakilishi wa kituo cha watoto yatima cha Medical Daughters of Mary Saint Joseph Health Orphanage cha Kiseriani wilayani Arumeru, Happines Antony na mtoto wa kituo hicho, Magereth John wakati alipokuwa akikabidhi zawadi kwa vituo vitano vya kulea watoto yatima vilivyoko wilayani Arumeru na Manispaa ya Arusha kwa ajili ya kusherehekea Sikukuu ya Krismas na mwaka mpya.
Picha ya 2
Kushoto ni Mbunge wa Viti maalumu mkoa wa Arusha Joyce Mukya (Chadema)akikabidhi zawadi kwa Katibu wa kituo cha watoto yatima cha Faraja Orphanage Children Home kilichopo eneo la Shangarai, wilayani Arumeru, Estomih Simon na mtoto wa kituo hicho, Emmanuel Faraja wakati alipokabidhi zawadi kwa vituo vitano katika hafla fupi iliyofanyika nje ya ofisi yake zilizopo jengo la ofisi za Mkuu wa wilaya ya Arusha hivi karibuni.
Picha ya 3
Watoto wa kituo cha watoto yatima cha Faraja Orphanage Children Home eneo la Shangarai, wilayani Arumeru, Emmanuel Faraja (kulia) na Elisha Paulo wakiwa wamemshikilia mbuzi waliopewa na mbunge wa viti maalumu Joyce Mukya kwa ajili ya sikukuu ya Krismass na mwaka mpya
 

Attachments

  • zawadi_1[1].JPG
    zawadi_1[1].JPG
    1 MB · Views: 635
  • Zawadi_II[1].JPG
    Zawadi_II[1].JPG
    1.1 MB · Views: 477
  • Zawadi_III[1].JPG
    Zawadi_III[1].JPG
    1.1 MB · Views: 322
Back
Top Bottom