Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,476
- 39,995
Unapokuwa vitani kuna suala moja ambalo mtu yeyote anayefuatilia mambo ya vita au jeshi analijua. Makamanda na Wapiganaji wote huvaa mavazi yanayofafa bila kujitofautisha. Kuna sababu kubwa mbili: Kwanza ni suala la uniformity (sare) wakati wa vita ili kuonesha ule umoja wa wapambanaji wote majemedari na wapiganaji wote wako katika vita vimoja - hivyo makamanda hawavai nishani zao au mavazi yao ya sherehe au mapambo bali huvaa mavazi ya wapiganaji wote. Sababu ya pili ni ya kiusalama zaidi - kamanda akiwa amejitofautisha kwa mavazi yake na wapiganaji wake ni rahisi adui kumlenga yeye hivyo wanapovaa mavazi yanayofafa ni vigumu kwa adui aliye mbali kujua kamanda ni yupi zaidi. Hapa kuna somo. Yote haya mawili yanatoa sababu ya tatu kwamba Kuna umoja wa kamandi toka walio juu kwenda walio chini katika mapambano ya pamoja.
Niliandika jambo hili zaidi ya mwaka mmoja uliopita sipendi mavazi ya mgambo ya Chadema ambayo yanawatenganisha viongozi wao na wanachama wao na hivyo kufanya wawepo "makamanda" ambao wako tofauti na wapiganaji wao. Haya mavazi ya mgambo kwangu ni kama mavazi ya mapambo ya wanajeshi ambayo wakipenda wanaweza kuvaa ofisini, wanapokutana wao wenyewe n.k lakini inapokuja kwenye kukutana na wananchi wao au kuhamasisha wananchi wao (wapiganaji) ni muhimu wakavaa mavazi ya rangi ya chama ili kutimiza malengo hayo matatu.
Na hili pia linanifanya nisielewe kabisa kwanini wanapoandamana wanazungukwa kwenye mduara na watu walioshikana mkono wakati wako kwenye mapambano!! Nani anawazunguka mkono wananchi wengine. Kuna utaratibu mzuri wa kusimamia ulinzi - kuweka mistari ya walinzi nyuma ya kidogo ambao nao wamefanana kimavazi na wanachama wao.
picha:
Gen. Tom Hobbins (left), U.S. Air Forces in Europe commander, and Chief Master Sgt. Gary Coleman (right), USAFE command chief, greet Senior Airman Kenyata Jenkins (second from right) and other members of 376 ESVS during the general's trip downrange July 5. (kuoka USAF)
Mkuu wa Majeshi Generali Davis Mwamunyange na Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya mambo ya nje Ulinzi na Usalama Wilison Masilingi (kushoto kwa afande Mwamunyange) wakipata maelezo mara baada ya ufunguzi wa maonesho na maadhimisho ya JWTZ kutimiza miaka 45. Mh. Masilingi alikuwa mgeni rasmi kwenye ufunguzi wa Maadhimisho hayo yanayoendelea katika kikosi cha 603 cha jeshi eneo la Airwing ,Ukonga jijini Dar (Kutoka Kadidi Blog)
Mwamunyange akiwa na Dr. Mwinyi baada ya milipuko ya Gongo la Mboto (angalia wapiganaji walio nyuma yake)
Nyerere akimvisha nishani Kanali Mahfoudh.
Kamanda Mkuu wa CCM na chipukizi - fikiria Chipukizi huyo anavyojiona ni sehemu ya CCM.
Inatuachia chaguzi mbili au tatu:
a. Makamanda wa Chadema na wanachama wavae rangi za chama wote
b. Wanachama wote wavae mavazi ya kikamanda
c. Kila mmoja ajivalie kivyake alimradi kila mmoja anapigana kivyake.
Kwa ufupi, ni lazima kuwe na uniformity of sort siyo katika ujumbe tu bali pia katika mwonekano. Ndio maana ya kuwa kwenye mapambano pamoja. Unless... ni mapambano ya makamanda.
My fifty cents.
Niliandika jambo hili zaidi ya mwaka mmoja uliopita sipendi mavazi ya mgambo ya Chadema ambayo yanawatenganisha viongozi wao na wanachama wao na hivyo kufanya wawepo "makamanda" ambao wako tofauti na wapiganaji wao. Haya mavazi ya mgambo kwangu ni kama mavazi ya mapambo ya wanajeshi ambayo wakipenda wanaweza kuvaa ofisini, wanapokutana wao wenyewe n.k lakini inapokuja kwenye kukutana na wananchi wao au kuhamasisha wananchi wao (wapiganaji) ni muhimu wakavaa mavazi ya rangi ya chama ili kutimiza malengo hayo matatu.
Na hili pia linanifanya nisielewe kabisa kwanini wanapoandamana wanazungukwa kwenye mduara na watu walioshikana mkono wakati wako kwenye mapambano!! Nani anawazunguka mkono wananchi wengine. Kuna utaratibu mzuri wa kusimamia ulinzi - kuweka mistari ya walinzi nyuma ya kidogo ambao nao wamefanana kimavazi na wanachama wao.
picha:
Gen. Tom Hobbins (left), U.S. Air Forces in Europe commander, and Chief Master Sgt. Gary Coleman (right), USAFE command chief, greet Senior Airman Kenyata Jenkins (second from right) and other members of 376 ESVS during the general's trip downrange July 5. (kuoka USAF)
Mkuu wa Majeshi Generali Davis Mwamunyange na Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya mambo ya nje Ulinzi na Usalama Wilison Masilingi (kushoto kwa afande Mwamunyange) wakipata maelezo mara baada ya ufunguzi wa maonesho na maadhimisho ya JWTZ kutimiza miaka 45. Mh. Masilingi alikuwa mgeni rasmi kwenye ufunguzi wa Maadhimisho hayo yanayoendelea katika kikosi cha 603 cha jeshi eneo la Airwing ,Ukonga jijini Dar (Kutoka Kadidi Blog)
Mwamunyange akiwa na Dr. Mwinyi baada ya milipuko ya Gongo la Mboto (angalia wapiganaji walio nyuma yake)
Nyerere akimvisha nishani Kanali Mahfoudh.
Kamanda Mkuu wa CCM na chipukizi - fikiria Chipukizi huyo anavyojiona ni sehemu ya CCM.
Inatuachia chaguzi mbili au tatu:
a. Makamanda wa Chadema na wanachama wavae rangi za chama wote
b. Wanachama wote wavae mavazi ya kikamanda
c. Kila mmoja ajivalie kivyake alimradi kila mmoja anapigana kivyake.
Kwa ufupi, ni lazima kuwe na uniformity of sort siyo katika ujumbe tu bali pia katika mwonekano. Ndio maana ya kuwa kwenye mapambano pamoja. Unless... ni mapambano ya makamanda.
My fifty cents.