Picha yangu ya leo hii wakuu wenzangu........

Herbalist Dr MziziMkavu

JF-Expert Member
Feb 3, 2009
42,299
33,082
ccm na Chadema.jpg

Nani mshindi kati ya hizi helkopta mbili?
 
Mbona hakuna ya KAFU? Halafu hizo njia zilizopita ni noma, ya ccm imewazunguka kinamama, ya cdm ime piga sarakasi, hahaha.
 
Hii ya jembe na nyundo ni hatari sana inacheza na maisha ya hao wana igunga, angalia misele yake kwanza ilivyotaka kuondoka na masaburi ya hao watu, lol!!!!
 
Hii ya jembe na nyundo ni hatari sana inacheza na maisha ya hao wana igunga, angalia misele yake kwanza ilivyotaka kuondoka na masaburi ya hao watu, lol!!!!
Kwenye kampeni ya Uchaguzi ilipotea njia hahahahahahahah ndio maana inapiga misele mingi tuu
 
Tunataka wiki ya utulivu Igunga



KATUNI(541).jpg

Maoni ya katuni


Jumapili ya wiki hii, yaani siku sita kuanzia leo, wananchi wa jimbo la uchaguzi la Igunga wenye haki ya kupiga kura watatumia haki yao kupiga kura ya kumchagua mbunge wao katika uchaguzi mdogo wa kujaza nafasi ya kiti cha ubunge kilichoachwa wazi na mbunge wa zamani aliyejiuzulu.

Hii ni wiki ya kuhitimisha kampeni miongoni mwa wagombea mbalimbali wa vyama vya siasa vinane vinavyoshiki uchaguzi huu wa kwanza mdogo baada ya uchaguzi mkuu wa mwaka jana.

Harakati za kampeni za uchaguzi huu zimekuwa na hamasa ya kipekee kutoka kwa washiriki mbalimbali; vyama vya siasa, wagombea wake na wapambe wao kwa maana ya wapiga debe katika kampeni wamekuwa wakinguruma jimboni humo kwa takribani wiki tatu sasa tangu kampeni zianze.

Yapo matukio mazuri ya kujinadi katika kuomba kura, lakini pia yapo ya kusikitisha. Makubwa ambayo ni mazuri ni ukweli kwamba wagombea wote wamepata fursa ya kujinadi kwa wananchi kuomba kura; vyama vyao vimeendesha kampeni kwa madhumuni hayo hayo. Hali hii imetoa fursa kwa wananchi kusikiliza, kupima na mwishowe kuamua nani hasa anastahili kuwatumikia katika kipindi cha miaka minne ijayo.


Lakini pia kuna hitilafu nyingi katika kampeni hizi, yapo matukio ya vurugu, kama ya kupigwa kwa watu, kuharibiwa kwa mali kama vile kuchomwa nyumba, kuvunjwa vioo vya magari, kutaja matukio haya kwa uchache tu. Kadhalika kumekuwa na malalamiko ya wagombea na vyama vyao dhidi ya wagombea wengine na vyama vyao; kuna kesi imefunguliwa mahakamani dhidi ya baadhi ya wadau wa uchaguzi huu wakidaiwa kumteka mkuu wa wilaya.


Kuna suala la malalamiko dhidi ya Jeshi la Polisi kwamba wamekuwa wanaonyesha upendeleo wa dhahiri kwa mmoja wa wagombea na chama chake; haya yote yemezungumzwa kwa uwazi na bila uficho wahusika wamesikia na kuna nyakati wametoa ufafanuzi.


Tumekaa na kutafakati mwelekeo wa kampeni za kuomba kura na kujiridhisha kwamba wiki hii kama busara, hekima na ungalifu wa hali ya juu havitazingatiwa, kuna hatari kubwa ya kuzorota kwa hali ya usalama katika jimbo hili na kwa maana hiyo kuathiri uchaguzi wenywe kiasi cha kuufanya upoteze sifa ya kuwa huru na wa haki.


Ni kwa maana hiyo, kwanza tunawaomba wadau wote katika uchaguzi huu, yaani wagombea, vyama vyao pamoja na wapambe kwa upande mmoja na vyombo vya dola kwa maana ya Tume ya Uchaguzi na Jeshi la Polisi kwa upande mwingine kila mmoja kutambua wajibu wake na kuuzingatia ili kuepusha uwezekano wowote wa kuingia katika vurugu dakika hizi za lala salama katika uchaguzi huu.


Tunasema haya kwa kuwa wananchi kwa kawaida ni wasikilizaji tu wa hotuba, ahadi na kila aina ya mbwembwe kwenye uchaguzi, ni vigumu sana kusema wananchi wenyewe tu wanaweza kuanzisha vurugu. Vurugu zinaanzishwa moja, kwa walinzi wa usalama kushindwa kutenda haki kwa makundi yote yanayoshiriki uchaguzi; mbili, kwa wagombe, wapambe na vyama vyao kukataa kwa makusudi kuheshimu haki za wengine katika uchaguzi huo.


Haki hizi ni pamoja na kujiepusha na lugha ya matusi na kashfa ambazo zinaweza kuibua hisia mbaya; kuheshimu ratiba za mikutano ya wengine kama vile maeneo ya kufanya mikutano ya hadhara kulingana na ratiba ambayo imepitishwa na Tume ya Uchaguzi, kupenyeza wafuasi wa vyama katika mikutano ya wengine kwa nia ya kuivuruga kama vile kuzomea na kuleta usumbufu wowote ule usiokubalika.


Tumeona katika kipindi cha wiki hizi chache zilizopita joto la uchaguzi likipanda kwa kasi kubwa; tumesikia habari za risasi kurindima, lakini pia tumeshuhudia wapambe wa wagombea wakionyesha silaha hadharani.

Tunaamini katika kipindi hiki cha lala salama umakini wa hali ya juu unahitajika ili kuepusha joto hilo lisipande kiasi cha kubadili mwelekeo wa mambo ili badala ya kuwa na uchaguzi ifikapo Jumapili Okctoba 2, mwaka huu, tuwe na vurugu na umwagaji damu miongoni mwa wagombea na vyama vyao.

Hii ni wiki ya mwisho, tunaomba wagombea, vyama vyao, wapambe wao, na vyombo vya dola hususan Jeshi la Polisi watupe kampeni makini lakini za amani ili wananchi wajitokeze kwa wingi Jumapili ijayo kuamua nani wa kuwawakilisha bungeni katika kipindi cha kuanzia sasa hadi 2015. Tunatarajia uungwana na ustaarabu katika wiki hii ya lala salama katika kampeni Igunga.





SOURCE: NIPASHE

 
jamani tucheke na katuni na tukumbuke kukomboa nchi yetu dhidi ya haya majamaa yanayotumia mabilioni kusaka wanachikiita "uongozi",kuwaongoza watu wanaoona gari wakati wa kampeni za uchaguzi tu...............!!!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom