ngalikikinakiki
Member
- Mar 29, 2011
- 55
- 18
Picha hii ya Tabora Jazz Band 1972/3 nimeitoa www.wanamuzikiwatanzania.blogspot.com blog ya John Kitime yenye picha nyingi sana za wanamuziki wa zamani
Kaka Kichuguu , anaweza kutupa mengi kuhusu huu wimbo wa Tabora Jazz wa Alhamdullilah......
Tabora Jazz Band Alhamdulillah free mp3 music download mp3rocket.eu page 1
Asante sana ndugu yangu Sikonge.
Huu wimbo wa Alhamdulillahi ni wimbo nilioupenda sana kuliko hata ule wa Dada Asha. Wimbo huu ulitolewa mwaka 1972 muda mfupi sana baada ya Morogoro Jazz kusambaratika na kuundwa kwa Super Volcano. Kipindi hicho bendi iliyokuwa na ubavu wa kubanana na Tabora Jazz ilikuwa ni Morogoro Jazz tu, ambapo kipindi hicho Tabora Jazz ndiyo iliyokuwa inashikiria taji na bendi bora ya muziki Tanzania kabla hawajanyang'anywa taji hilo na sunburst na baadaye Afro Sabini. Tabora Jazz walikuwa wamepokonya taji hilo kutoka kwa Morogoro Jazz ambayo nayo ilikuwa imebadilishana taji hilo na Jamhuri Jazz ya Tanga mwaka mmoja tu nyuma yake.
Sasa wakati Morogoro Jazz inasambaratika na kuuundwa kwa Super Volcana, Jamhuri Jazz nayo ilikuwa aimeanza kusambaratika kwa vile wapigaji wake wakubwa akina George Kinyonga na Professor Omari walikuwa wamehamia kwenye bendi ya Kurugenzi ya Arusha ambako ndiko walikotokea na kwenda kuanzisha Simba wa Nyika.
Mzee Shem Kalenga aliona kuwa taji la ubingwa wa bendi lilkikuwa linafuatiwa na balaa la kuvunjika kwa bendi ndipo akatoa dua kwa kutunga wimbo huo wa Alhamdulilahi.
Sijui kama nimekusaidai kidogo
Sasa wakati Morogoro Jazz inasambaratika na kuuundwa kwa Super Volcana, Jamhuri Jazz nayo ilikuwa aimeanza kusambaratika kwa vile wapigaji wake wakubwa akina George Kinyonga na Professor Omari walikuwa wamehamia kwenye bendi ya Kurugenzi ya Arusha ambako ndiko walikotokea na kwenda kuanzisha Simba wa Nyika.
Nausaka sana ule WIVU UKIZID MAPENZI YAPUNGUA