Picha ya Tabora jazz Band

Mar 29, 2011
55
18
Tabora+jazz+1971.jpg



Picha hii ya Tabora Jazz Band 1972/3 nimeitoa www.wanamuzikiwatanzania.blogspot.com blog ya John Kitime yenye picha nyingi sana za wanamuziki wa zamani
 
Dahhh, hizi Band za zamani na miziki yake ilikuwa poa sana. I wish ningeliweza kuwaona LIVE wakihangaika kucheza maana siku hizo hata kucheza hawajui labda hadi walewe wanaanza kujirusharusha na kujipinduapindua kama funza...

 
Last edited by a moderator:
Kaka Kichuguu , anaweza kutupa mengi kuhusu huu wimbo wa Tabora Jazz wa Alhamdullilah......

Tabora Jazz Band Alhamdulillah free mp3 music download mp3rocket.eu page 1

Asante sana ndugu yangu Sikonge.

Huu wimbo wa Alhamdulillahi ni wimbo nilioupenda sana kuliko hata ule wa Dada Asha. Wimbo huu ulitolewa mwaka 1972 muda mfupi sana baada ya Morogoro Jazz kusambaratika na kuundwa kwa Super Volcano. Kipindi hicho bendi iliyokuwa na ubavu wa kubanana na Tabora Jazz ilikuwa ni Morogoro Jazz tu, ambapo kipindi hicho Tabora Jazz ndiyo iliyokuwa inashikiria taji na bendi bora ya muziki Tanzania kabla hawajanyang'anywa taji hilo na sunburst na baadaye Afro Sabini. Tabora Jazz walikuwa wamepokonya taji hilo kutoka kwa Morogoro Jazz ambayo nayo ilikuwa imebadilishana taji hilo na Jamhuri Jazz ya Tanga mwaka mmoja tu nyuma yake.

Sasa wakati Morogoro Jazz inasambaratika na kuuundwa kwa Super Volcana, Jamhuri Jazz nayo ilikuwa aimeanza kusambaratika kwa vile wapigaji wake wakubwa akina George Kinyonga na Professor Omari walikuwa wamehamia kwenye bendi ya Kurugenzi ya Arusha ambako ndiko walikotokea na kwenda kuanzisha Simba wa Nyika.

Mzee Shem Kalenga aliona kuwa taji la ubingwa wa bendi lilkikuwa linafuatiwa na balaa la kuvunjika kwa bendi ndipo akatoa dua kwa kutunga wimbo huo wa Alhamdulilahi.

Sijui kama nimekusaidai kidogo
 
Kaka Kichuguu,

Nashukuru sana kwa majibu ambayo nafikiri jamaa wengi wa Blog hasa Mzee John Kitime wangelichukua kabisa hiki kipande kizuri cha historia na kukiweka kwenye Blog zao. Nategemea siku moja mtu atakuja kuandika historia nzima ya hizi Band tatu maarufu za mziki za mkoa wetu wa Tabora.

Ningelisoma zaidi na zaidi na hasa Band hizi nyingine mbili ambazo niseme ukweli sijawahi kabisa kufahamu historia yake yaani Nyanyembe Jazz na Kiko Kids ambazo nazo kwa aina moja au nyingine zilipata sifa kubwa mjini Tabora na hata nje ya Mkoa.



Asante sana ndugu yangu Sikonge.

Huu wimbo wa Alhamdulillahi ni wimbo nilioupenda sana kuliko hata ule wa Dada Asha. Wimbo huu ulitolewa mwaka 1972 muda mfupi sana baada ya Morogoro Jazz kusambaratika na kuundwa kwa Super Volcano. Kipindi hicho bendi iliyokuwa na ubavu wa kubanana na Tabora Jazz ilikuwa ni Morogoro Jazz tu, ambapo kipindi hicho Tabora Jazz ndiyo iliyokuwa inashikiria taji na bendi bora ya muziki Tanzania kabla hawajanyang'anywa taji hilo na sunburst na baadaye Afro Sabini. Tabora Jazz walikuwa wamepokonya taji hilo kutoka kwa Morogoro Jazz ambayo nayo ilikuwa imebadilishana taji hilo na Jamhuri Jazz ya Tanga mwaka mmoja tu nyuma yake.

Sasa wakati Morogoro Jazz inasambaratika na kuuundwa kwa Super Volcana, Jamhuri Jazz nayo ilikuwa aimeanza kusambaratika kwa vile wapigaji wake wakubwa akina George Kinyonga na Professor Omari walikuwa wamehamia kwenye bendi ya Kurugenzi ya Arusha ambako ndiko walikotokea na kwenda kuanzisha Simba wa Nyika.

Mzee Shem Kalenga aliona kuwa taji la ubingwa wa bendi lilkikuwa linafuatiwa na balaa la kuvunjika kwa bendi ndipo akatoa dua kwa kutunga wimbo huo wa Alhamdulilahi.

Sijui kama nimekusaidai kidogo
 
Last edited by a moderator:
Sasa wakati Morogoro Jazz inasambaratika na kuuundwa kwa Super Volcana, Jamhuri Jazz nayo ilikuwa aimeanza kusambaratika kwa vile wapigaji wake wakubwa akina George Kinyonga na Professor Omari walikuwa wamehamia kwenye bendi ya Kurugenzi ya Arusha ambako ndiko walikotokea na kwenda kuanzisha Simba wa Nyika.

Nausaka sana ule WIVU UKIZID MAPENZI YAPUNGUA
 
KUTOKA KWA KITIME GLOG:

Tabora+jazz+1971.jpg


Mkuu kitime kwenye picha hii ya Tabora Jazz,huyo aliyesimaa wa kwanza kulia(jacket ya track) ni mjomba wetu soloist wa kwanza kabisa kabla ya Shem Karenga Athmani Tembo(Baba Nyota)R.I.P,aliacha miziki akaingia kazi ya railway akafanya Shinyanga,Moshi,na kurudi Tabora alifariki muda mfupi tu baada ya kustaafu Railway,pia alipoacha miziki akawa mswalihina mtu wa swala tano,atakumbukwa sana kwa kuwa nae alikuwa guitarist mzuri sana.R.I.P uncle AthmaniTembo.
Abbu Omar,prof.Jnr.(Mwanamuziki)Tokyo,Japan .

Kijiwe cha KITIME: Chakula kwa jirani ya Tabora Jazz Band
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom