Miss Zomboko
JF-Expert Member
- May 18, 2014
- 4,498
- 9,279
Seneta Norma Durango aliwasilisha muswada bungeni ili kumfanya kiungo huyo, ambaye alifariki wiki mbili zilizopita akiwa na umri wa miaka 60, kuwa kwenye noti ya 1,000 sawa na dola ($ 12, £ 9), noti ya juu zaidi.
Noti hiyo itakuwa na uso wa Maradona upande mmoja na picha ya moja ya mabao yake maarufu, hususan dhidi ya England katika robo fainali ya 1986, kwa upande mwingine, alisema.
Seneta huyo pia alipendekeza kuweka picha yake kwenye mihuri ya kumbukumbu.
"Wazo sio tu kumtambua mtu huyu muhimu zaidi, lakini pia kufikiria suala la uchumi," Bi Durango alisema.
"Tunahisi watalii wanapokuja hapa watataka kumchukua 'Maradona' na kwenda naye.
" Alisema seneta huyoPicha ya marehemu nyota wa Argentina Diego Maradona, aliyeiongoza nchi yake kutwaa Kombe la Dunia mwaka 1986, inaweza kuwa ndio uso wa noti yenye thamani kubwa zaidi nchini Argentina hivi karibuni.
BBC
Noti hiyo itakuwa na uso wa Maradona upande mmoja na picha ya moja ya mabao yake maarufu, hususan dhidi ya England katika robo fainali ya 1986, kwa upande mwingine, alisema.
Seneta huyo pia alipendekeza kuweka picha yake kwenye mihuri ya kumbukumbu.
"Wazo sio tu kumtambua mtu huyu muhimu zaidi, lakini pia kufikiria suala la uchumi," Bi Durango alisema.
"Tunahisi watalii wanapokuja hapa watataka kumchukua 'Maradona' na kwenda naye.
" Alisema seneta huyoPicha ya marehemu nyota wa Argentina Diego Maradona, aliyeiongoza nchi yake kutwaa Kombe la Dunia mwaka 1986, inaweza kuwa ndio uso wa noti yenye thamani kubwa zaidi nchini Argentina hivi karibuni.
BBC