Picha: Watu wawili wanaofanana na Rais Rodrigo Duterte na Rais Kim Jong-un wazua vioja Hong Kong

BuletAngle

JF-Expert Member
Apr 15, 2017
689
555
_105463641_hi052073909.jpg


Huenda ukadhania kwamba rais wa Ufilipino Rodrigo Durtete na mwenzake wa Korea Kaskazini Kim Jong Un walikuwa pamoja katika barabara za mji wa Hong Kong, wakipiga picha na kula pamoja chakula cha jioni katika mgahawa mmoja.

Lakini uchunguzi wa kina ulibaini kwamba wawili hao walikuwa watu waliowaiga viongozi hao wawili.
Kutana na jamaa anayejiita Cresencio Extreme anayefanana na Durtete na Howard X anayefanana na Kim Jong un.

_105463672_tv052073919.jpg


Wawili hao waliobeba bunduki bandia walisalimiwa na wafanyikazi na raia walipowasili katika mgahawa huo wa kuku karanga au Fried Chicken Restaurant

_105463676_hi052073553.jpg


Walihudhuria ibada ya Jumapili katika kanisa la St Joseph's huku Cresencio Extreme (kushoto)akiwa amevalia shati jeupe ambalo hupendwa sana na rais Durtete

_105463720_hi052073540.jpg


Mtu huyo anayefanana na rais Durtete alizua kihoja na mkanganyiko katika kanisa hilo katikati ya mji wa Hong Kong baada ya kuzungukwa na waumini

_105463724_hi052073548.jpg


Je huyu ni Durtete?'' Wengine hawakukubaliana naye huku raia huyo akionekana kuwa mdogo kwa umri kuwa rais wa Ufilipino pamoja na mwenzake anayemuiga rais wa Korea Kaskazini Kim Jong Un.

_105462934_hi052073904.jpg


Wawili hao walizidi kuwakanganya raia waliopoonekana wakila chakula cha jioni katika mgahawa wa Hong Kong siku ya Jumapili.

_105462935_dudez2.jpg

Mr Duterte {kushoto) na muigaji wake

_105462937_kim-composites.jpg

Bwana Kim (kushoto) na muigaji .
 
Back
Top Bottom