MwanaDiwani
JF-Expert Member
- Mar 22, 2013
- 5,536
- 2,264
Kwa kile ambacho tumekishuhudia Jijini Mwanza kinatoa ujumbe unaosema, Majimbo ambayo yako chini ya CHADEMA katika mikoa ya Kanda ya Ziwa yako mbioni kurudi CCM. Sina haja ya kuongelea Urais wa Tanzania kwa sababu Magufuli anasubiri kuapishwa tu.
SHUGHULI mbalimbali katika maeneo ya Barabara Kuu itokayo Uwanja wa Ndege wa Mwanza hadi mjini katikati, jana zilisimama kwa muda wa saa moja, huku wakazi wa jiji hilo wakishiriki kumpokea mgombea mteule wa urais wa CCM, Dk John Magufuli.
Mapokezi hayo ambayo yameacha historia ya pekee jijini hapa, yalianzia katika uwanja huo saa 8:00 mchana alipowasili akiongozana na mkewe Janeth Magufuli, Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye na Naibu Katibu Mkuu wa CCM, Rajabu Luhavi.
Uwanjani, mgombea huyo alipokewa na mamia ya wana CCM, viongozi mbalimbali wa Chama na Serikali kutoka mkoani hapa na mikoa ya jirani ya Kanda ya Ziwa, wakiwemo Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi, Dk Titus Kamani na Naibu Waziri Nishati na Madini, Charles Kitwanga.
Msafara wa Dk Magufuli ukiongozwa na pikipiki zaidi ya 150 ulianza safari kwenda mjini kati ya saa nane mchana, ambapo maelfu ya wananchi waliojipanga katika maeneo mbalimbali katika barabara hiyo wakiwemo akina mama, watoto na vijana, wakijitokeza kumlaki na kumpungia kwa khanga za CCM na matawi ya miti.
Maeneo hayo ni pamoja na Ilemela, Butuja, Sabasaba, Iloganzala, Pasiansi, Nyamanoro, Ghana na Mission ambapo alilazimika kusimama kwa muda katika baadhi ya maeneo hayo na kusalimia wananchi baada ya kumzuia kwa nguvu wakimtaka awasalimie.
Kote huko wananchi walikuwa wakimshangilia kwa makofi, vigelegele na vifijo wakimuita ‘Jembe, Jembe' huku baadhi wakipaza sauti na kumwambia "Wewe ndiye Rais wetu, wengine wanajisumbua."
Kutokana na muda mwingi kutumia barabarani akitokea uwanja wa ndege, ilibidi mkutano wake kwenye viwanja vya Furahisha uahirishwe kutokana na kukosekana kwa muda wa kutosha.
Wananchi wengi wamesikika wakisema CCM kwa sasa inarudi kwa wenyewe ambao ni wakulima na wafanyakazi na kwa maana hii, wako tayari kumpa ushirikiano Magufuli kwa kuchagua wabunge wachapa kazi kama yeye ili wamsaidie kuunda serikali yenye kuwajika kwa wananchi.
SHUGHULI mbalimbali katika maeneo ya Barabara Kuu itokayo Uwanja wa Ndege wa Mwanza hadi mjini katikati, jana zilisimama kwa muda wa saa moja, huku wakazi wa jiji hilo wakishiriki kumpokea mgombea mteule wa urais wa CCM, Dk John Magufuli.
Mapokezi hayo ambayo yameacha historia ya pekee jijini hapa, yalianzia katika uwanja huo saa 8:00 mchana alipowasili akiongozana na mkewe Janeth Magufuli, Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye na Naibu Katibu Mkuu wa CCM, Rajabu Luhavi.
Uwanjani, mgombea huyo alipokewa na mamia ya wana CCM, viongozi mbalimbali wa Chama na Serikali kutoka mkoani hapa na mikoa ya jirani ya Kanda ya Ziwa, wakiwemo Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi, Dk Titus Kamani na Naibu Waziri Nishati na Madini, Charles Kitwanga.
Msafara wa Dk Magufuli ukiongozwa na pikipiki zaidi ya 150 ulianza safari kwenda mjini kati ya saa nane mchana, ambapo maelfu ya wananchi waliojipanga katika maeneo mbalimbali katika barabara hiyo wakiwemo akina mama, watoto na vijana, wakijitokeza kumlaki na kumpungia kwa khanga za CCM na matawi ya miti.
Maeneo hayo ni pamoja na Ilemela, Butuja, Sabasaba, Iloganzala, Pasiansi, Nyamanoro, Ghana na Mission ambapo alilazimika kusimama kwa muda katika baadhi ya maeneo hayo na kusalimia wananchi baada ya kumzuia kwa nguvu wakimtaka awasalimie.
Kote huko wananchi walikuwa wakimshangilia kwa makofi, vigelegele na vifijo wakimuita ‘Jembe, Jembe' huku baadhi wakipaza sauti na kumwambia "Wewe ndiye Rais wetu, wengine wanajisumbua."
Kutokana na muda mwingi kutumia barabarani akitokea uwanja wa ndege, ilibidi mkutano wake kwenye viwanja vya Furahisha uahirishwe kutokana na kukosekana kwa muda wa kutosha.
Wananchi wengi wamesikika wakisema CCM kwa sasa inarudi kwa wenyewe ambao ni wakulima na wafanyakazi na kwa maana hii, wako tayari kumpa ushirikiano Magufuli kwa kuchagua wabunge wachapa kazi kama yeye ili wamsaidie kuunda serikali yenye kuwajika kwa wananchi.